< Waamuzi 20 >

1 Ndipo Waisraeli wote kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na wa kutoka nchi ya Gileadi wakatoka kama mtu mmoja wakakusanyika mbele za Bwana huko Mispa.
Alors tous les enfants d'Israël sortirent, et tout le peuple fut assemblé comme si ce n'eût été qu'un seul homme, depuis Dan jusqu'à Beersebah, et jusqu'au pays de Galaad, vers l'Eternel, en Mitspa.
2 Viongozi wote wa kabila za Israeli wakakaa kwenye nafasi zao katika kusanyiko la watu wa Mungu, askari 400,000 waendao kwa miguu wenye panga.
Et les Cantons de tout le peuple, toutes les Tribus d'Israël, se trouvèrent à l'assemblée du peuple de Dieu, [au nombre de] quatre cent mille hommes de pied dégainant l'épée.
3 (Wabenyamini wakasikia kuwa Waisraeli wamepanda kwenda Mispa.) Ndipo Waisraeli wakasema, “Tuelezeni jinsi jambo hili ovu lilivyotendeka.”
(Or les enfants de Benjamin apprirent que les enfants d'Israël étaient montés en Mitspa.) Les enfants donc d'Israël dirent: Qu'on nous récite comment ce mal est arrivé.
4 Hivyo yule Mlawi, mume wa yule mwanamke aliyeuawa, akasema, “Mimi na suria wangu tulifika Gibea ya Benyamini ili tulale huko.
Et le Lévite, mari de la femme tuée, répondit et dit: Etant arrivés à Guibha, qui est de Benjamin, moi et ma concubine, pour y passer la nuit;
5 Wakati wa usiku watu wa Gibea wakanijia na kuizingira nyumba, wakitaka kuniua. Wakambaka suria wangu mpaka akafa.
Les Seigneurs de Guibha se sont élevés contre moi, et ont environné de nuit la maison contre moi, prétendant me tuer; et ils ont tellement violé ma concubine qu'elle en est morte.
6 Ndipo nikamchukua suria wangu, nikamkatakata vipande vipande na kuvipeleka katika nchi yote ya urithi wa Israeli, kwa kuwa wametenda uasherati mkubwa na jambo la aibu katika Israeli.
C'est pourquoi ayant pris ma concubine, je l'ai mise en pièces, et je les ai envoyées par tous les quartiers de l'héritage d'Israël; car ils ont fait un crime énorme, et une action infâme en Israël.
7 Sasa, ninyi Waisraeli wote, semeni na mtoe uamuzi wenu.”
Vous voici tous, enfants d'Israël, délibérez-en ici entre vous, et donnez-en votre avis.
8 Watu wote wakainuka wakasema, kama mtu mmoja, “Hakuna hata mmoja wetu atakayekwenda nyumbani. Wala hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake.
Et tout le peuple se leva, comme si ce n'eût été qu'un seul homme, et ils dirent: Aucun de nous n'ira en sa tente, ni aucun de nous ne se retirera dans sa maison.
9 Sasa hili ndilo tutakaloitendea Gibea: Tutaikabili jinsi kura itakavyotuongoza.
Mais maintenant voici ce que nous ferons à Guibha, en procédant contr'elle par sort.
10 Tutatoa watu kumi katika kila 100 kutoka kwenye kabila zote za Israeli, watu 100 katika watu 1,000 na watu 1,000 katika 10,000, ili waende wakalete mahitaji kwa ajili ya jeshi. Basi wakati jeshi litakapofika Gibea ya Benyamini, watawatendea yale wanayostahili, kwa ajili ya uovu huu wa aibu waliotenda katika Israeli.”
Nous prendrons dix hommes de cent dans toutes les Tribus d'Israël, et cent de mille, et mille de dix mille, qui prendront de la provision pour le peuple, afin qu'étant entrés à Guibha de Benjamin, ils la traitent selon toute la turpitude qu'elle a commise en Israël.
11 Hivyo wanaume wote wa Israeli wakakutanika pamoja na kujiunga kama mtu mmoja dhidi ya huo mji.
Ainsi tous ceux d'Israël furent assemblés contre cette ville-là, étant unis comme s'ils n'eussent été qu'un seul homme.
12 Makabila ya Israeli yakatuma watu kwenda katika kabila la Benyamini lote na kuwaambia, “Ni uovu gani huu wa kutisha uliotendeka katikati yenu?
Alors les Tribus d'Israël envoyèrent des hommes par toute la tribu de Benjamin pour lui dire: Quelle méchante action a-t-on [commise] parmi vous?
13 Basi watoeni hao watu waovu kabisa walioko Gibea, ili tupate kuwaua na kuondoa uovu katika Israeli.” Lakini Wabenyamini hawakuwasikia ndugu zao, Waisraeli.
Maintenant donc livrez-nous ces méchants hommes qui sont à Guibha, afin que nous les fassions mourir, et que nous ôtions le mal du milieu d'Israël. Mais les Benjamites ne voulurent point écouter la voix de leurs frères les enfants d'Israël.
14 Wakatoka katika miji yao, wakakutanika Gibea ili kupigana na Waisraeli.
Mais les Benjamites sortant de leurs villes s'assemblèrent à Guibha, pour sortir en bataille contre les enfants d'Israël.
15 Siku ile Wabenyamini wakakusanya watu 26,000 kutoka miji yao, waliojifunga panga, mbali na hao 700 waliochaguliwa miongoni mwa hao waliokaa Gibea.
Et en ce jour-là on fit le dénombrement des enfants de Benjamin qui étaient dans ces villes, [et il se trouva] vingt-six mille hommes, tirant l'épée, sans les habitants de Guibha, dont on fit aussi le dénombrement, qui furent sept cents hommes d'élite.
16 Miongoni mwa hao askari wote kulikuwa na watu 700 bora waliochaguliwa watumiao mkono wa kushoto, kila mmoja wao aliweza kutupa jiwe kwa kombeo na kulenga unywele mmoja bila kukosa.
De tout ce peuple-là il y avait sept cents hommes d'élite, desquels la main droite était serrée, tous tirant la pierre avec la fronde à un cheveu près, et ils n'y manquaient point.
17 Nao watu wa Israeli, mbali na hao wa Benyamini, wakakusanya watu waume 400,000, wenye kutumia panga, wote hao walikuwa mashujaa.
Et les hommes d'Israël furent [tous] dénombrés, excepté ceux de Benjamin, et il s'en trouva quatre cent mille hommes tirant l'épée, tous gens de guerre.
18 Waisraeli wakapanda Betheli na kumuuliza Mungu, “Ni nani miongoni mwetu atakayetangulia mbele yetu ili kupigana na Wabenyamini?” Bwana akawajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia.”
Or ils partirent, et montèrent à la maison du [Dieu] Fort, et consultèrent Dieu. Les enfants donc d'Israël dirent: Qui est-ce d'entre nous qui montera le premier pour faire la guerre aux enfants de Benjamin? Et l'Eternel répondit: Juda [montera] le premier.
19 Asubuhi yake Waisraeli wakaamka na kupiga kambi karibu na Gibea.
Puis les enfants d'Israël se levèrent de bon matin, et campèrent près de Guibha.
20 Waisraeli wakatoka kupigana na Wabenyamini, nao Waisraeli wakajiweka kwenye nafasi zao katika vita dhidi yao huko Gibea.
Et ceux d'Israël sortirent en bataille contre Benjamin, et rangèrent contr'eux [leur] armée près de Guibha.
21 Wabenyamini wakatoka Gibea na kuwaua watu 22,000 wa Israeli siku ile.
Et les enfants de Benjamin sortirent de Guibha, et en ce jour-là ils mirent par terre de ceux d'Israël vingt-deux mille hommes.
22 Lakini Waisraeli wakatiana moyo kila mmoja na mwenzake, nao wakajiweka kwenye nafasi zao katika vile vita mara ya pili mahali pale walipokuwa wamejiweka mara ya kwanza.
Toutefois le peuple de ceux d'Israël reprit courage, et se rangea de nouveau en bataille au lieu où il s'était rangé le premier jour.
23 Waisraeli wakapanda mbele za Bwana na kulia mbele zake mpaka jioni, nao wakamuuliza Bwana wakisema, “Je, tupande tena kupigana vita na Wabenyamini, ndugu zetu?” Bwana akajibu, “Pandeni mkapigane nao.”
Parce que les enfants d'Israël étaient montés, et avaient pleuré devant l'Eternel jusqu'au soir, et avaient consulté l'Eternel en disant: M'approcherai-je encore pour combattre contre les enfants de Benjamin, mon frère? Et l'Eternel avait répondu: Montez contre lui.
24 Ndipo Waisraeli wakawakaribia Wabenyamini siku ya pili.
Les enfants d'Israël s'approchèrent des enfants de Benjamin pour la seconde journée.
25 Wakati huu, Wabenyamini walipotoka Gibea ili kupigana nao, wakawaua watu Waisraeli 18,000, wote wakiwa wamejifunga panga.
Benjamin aussi sortit de Guibha contr'eux en cette seconde journée, et ils mirent encore par terre dix-huit mille hommes des enfants d'Israël, tous tirant l'épée.
26 Ndipo Waisraeli, watu wote, wakapanda Betheli, huko wakakaa mbele za Bwana wakilia. Wakafunga siku ile mpaka jioni na kutoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya amani kwa Bwana.
Alors tous les enfants d'Israël, et tout le peuple montèrent, et vinrent à la maison du [Dieu] Fort, et y pleurèrent, et se tinrent là devant l'Eternel, et jeûnèrent ce jour-là jusqu'au soir, et offrirent des holocaustes, et des sacrifices de prospérités devant l'Eternel.
27 Nao Waisraeli wakauliza kwa Bwana. (Katika siku hizo Sanduku la Agano la Mungu lilikuwa huko
Ensuite les enfants d'Israël consultèrent l'Eternel, (or là était l'Arche de l'alliance de Dieu en ces jours-là.
28 na Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Aroni, alikuwa anahudumu mbele za hilo Sanduku.) Wakauliza, “Je, tupande kwenda vitani kupigana tena na Wabenyamini ndugu zetu, au la?” Bwana akajibu, “Nendeni, kwa kuwa kesho nitawatia mikononi mwenu.”
Et Phinées fils d'Eléazar, fils d'Aaron, se tenait devant l'Eternel en ces jours-là: ) [ils consultèrent donc l'Eternel] en disant: Sortirai-je encore une autre fois en bataille contre les enfants de Benjamin, mon frère, ou m'en désisterai-je? Et l'Eternel répondit: Montez, car demain je les livrerai entre vos mains.
29 Basi Waisraeli wakaweka waviziao kuizunguka Gibea.
Et Israël mit une embuscade à l'entour de Guibha.
30 Kisha Waisraeli wakapanda kupigana na Wabenyamini katika siku ya tatu na kujiweka kwenye nafasi zao dhidi ya Gibea kama walivyokuwa wamefanya hapo kwanza.
Et les enfants d'Israël montèrent pour la troisième journée contre les enfants de Benjamin, et ils se rangèrent contre Guibha, comme les autres fois.
31 Wabenyamini wakatoka ili kukabiliana nao, Waisraeli wakawavuta Wabenyamini watoke katika mji. Wakaanza kupigana na kuua watu wapatao thelathini wa Israeli, kama walivyofanya nyakati nyingine, katika njia kuu, moja iendayo Betheli na nyingine Gibea.
Alors les enfants de Benjamin étant sortis à la rencontre du peuple, furent attirés hors de la ville, et commencèrent à frapper quelques-uns du peuple, environ trente hommes d'Israël qui furent blessés à mort comme les autres fois, dans les chemins, dont l'un monte à la maison du [Dieu] Fort; et l'autre à Guibha, parmi les champs.
32 Wabenyamini wakafikiri, “Wanapigwa mbele yetu kama hapo kwanza.” Waisraeli wakasema, “Sisi na turudi nyuma ili tuwavute wauache mji waende kuelekea barabarani.”
Et les enfants de Benjamin dirent: Ils tombent battus devant nous, comme la première fois. Mais les enfants d'Israël disaient: Fuyons, attirons-les hors de la ville, dans les chemins.
33 Watu wote wa Israeli wakaondoka kwenye sehemu zao na kujipanga huko Baal-Tamari, nao wale waviziaji wa Waisraeli, wakatoka hapo walipokuwa kwenye uwanda wa magharibi ya Gibea.
Tous ceux d'Israël donc se levant de leur lieu, se rangèrent à Bahal-tamar; et les gens de l'embuscade aussi sortirent de leur lieu, [savoir de] la prairie de Guibha.
34 Ndipo watu 10,000 bora waliochaguliwa katika Israeli wote, wakaja kuishambulia Gibea. Vita vilikuwa vikali sana, hata Wabenyamini hawakutambua kuwa maangamizi yalikuwa karibu nao kwa kiasi hicho.
Et dix mille hommes d'élite de tout Israël vinrent contre Guibha, et la mêlée fut rude; et ceux de [Benjamin] ne s'aperçurent point que le mal les atteignait.
35 Bwana akawashinda Wabenyamini mbele ya Waisraeli na siku ile Waisraeli wakawaua Wabenyamini watu waume 25,100, wote wakiwa wenye kujifunga silaha za vita.
L'Eternel donc battit Benjamin devant les Israélites; et les enfants d'Israël mirent ce jour-là par terre vingt-cinq mille et cent hommes de Benjamin, tous tirant l'épée.
36 Hivyo Wabenyamini wakaona kuwa wamepigwa. Basi Waisraeli walikuwa wameondoka mbele ya Wabenyamini, kwa sababu Waisraeli waliwategemea hao waviziaji waliokuwa wamewaweka dhidi ya Gibea.
Les enfants de Benjamin donc virent qu'ils étaient battus. Or ceux d'Israël avaient fait place à ceux de Benjamin; car ils s'assuraient sur l'embuscade qu'ils avaient mise près de Guibha.
37 Wale waviziaji wakafanya haraka kuingia Gibea, wakasambaa na kuwaua watu wote wa mji kwa upanga.
Et ceux qui étaient en embuscade se jetèrent incontinent sur Guibha; ainsi ceux qui étaient en embuscade marchèrent à la file, et frappèrent toute la ville au tranchant de l'épée.
38 Waisraeli walikuwa wamepatana na hao waviziaji kuwa wangefanya lipande wingu kubwa la moshi kutoka huo mji,
Or ceux d'Israël avaient donné pour signal à ceux qui étaient en embuscade, qu'ils fissent monter beaucoup de fumée de la ville.
39 ndipo watu wa Waisraeli wangegeuka kupigana. Watu wa Benyamini walikuwa wameanza kuwapiga na kuua watu wa Israeli (wapatao thelathini), hivyo wakafikiri, “Hakika tutawapiga, kama tulivyowashinda katika vita hapo kwanza.”
Ceux d'Israël donc avaient tourné le dos en la bataille, et Benjamin avait commencé de frapper et de blesser à mort environ trente hommes de ceux d'Israël; car ils disaient: Quoi qu'il en soit, certainement ils tombent battus devant nous, comme à la première bataille.
40 Lakini wakati lile wingu la moshi lilipoanza kupanda kutoka ule mji, Wabenyamini wakageuka na kuona moshi wa mji mzima unapaa juu angani.
Mais quand la fumée qui avait été élevée, commença à monter de la ville comme une colonne de fumée, Benjamin regarda derrière soi, et voici toute la ville montait en feu vers le ciel.
41 Ndipo watu wa Israeli wakawageukia, nao Wabenyamini wakatiwa hofu, kwa kuwa walitambua kwamba maafa yamewajia.
Alors ceux d'Israël tournèrent visage et ceux de Benjamin furent épouvantés; car ils virent que le mal les avait atteints.
42 Basi wakakimbia mbele ya Waisraeli kuelekea nyikani, lakini hawakuweza kukwepa vile vita. Nao watu wa Israeli waliotoka katika ile miji wakawaua huko.
Et ils tournèrent le dos devant ceux d'Israël vers le chemin du désert; mais l'armée [d'Israël] les serra de près. Et quant à ceux des villes, ils les mirent par terre, les ayant enfermés au milieu d'eux.
43 Wakawazingira Wabenyamini pande zote, wakawafuatia na kuwapata hapo walipopumzika katika viunga vya Gibea upande wa mashariki.
Ils environnèrent [donc] ceux de Benjamin, [et] les poursuivirent, et les foulèrent aux pieds depuis Menuha jusqu'à l'opposite de Guibha, vers le soleil levant.
44 Wakaanguka Wabenyamini 18,000 ambao wote ni mashujaa.
Et il y eut de Benjamin dix-huit mille hommes tués, tous vaillants hommes.
45 Walipogeuka na kukimbia kuelekea nyikani hata kufikia mwamba wa Rimoni, Waisraeli wakawaua watu 5,000 wakiwa njiani. Wakawafuata kwa kasi mpaka Gidomu huko wakawaua watu wengine 2,000.
Alors [ceux de Benjamin] tournant le dos fuirent vers le désert au rocher de Rimmon, et [ceux d'Israël] en grappillèrent par les chemins cinq mille hommes, et les poursuivant de près jusqu'à Guidhom, ils en frappèrent deux mille hommes.
46 Siku ile wakawaua Wabenyamini 25,000 waliokuwa mashujaa wa vita.
Tous ceux donc qui tombèrent [morts] en ce jour-là de Benjamin, furent vingt-cinq mille hommes, tirant l'épée, [et] tous vaillants hommes.
47 Lakini watu 600 wakakimbia kuelekea nyikani katika mwamba wa Rimoni, na kukaa huko muda wa miezi minne.
Et il y eut six cents hommes de ceux qui avaient tourné le dos, qui échappèrent vers le désert au rocher de Rimmon, et qui demeurèrent au rocher de Rimmon quatre mois.
48 Waisraeli wakarudi na kuua watu wote wa Benyamini, pamoja na wanyama na kila walichokikuta. Pia kila mji waliouona waliuchoma moto.
Et ceux d'Israël retournèrent vers les enfants de Benjamin, et les frappèrent au tranchant de l'épée, tant les hommes de chaque ville que les bêtes, et tout ce qui s'y trouva. Ils brûlèrent aussi toutes les villes qui s'y trouvèrent.

< Waamuzi 20 >