< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Jesus spoke these things, raising His eyes to Heaven and saying: “Father, the hour has come! Glorify Your Son, so that Your Son also may glorify You,
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
just as You gave Him authority over all humanity, so that He will give eternal life to all those whom You have given Him. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
Now eternal life is this: that they may know You, the only true God, and the One whom You sent—Jesus Christ. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
I have glorified You on the earth. I have finished the work that You have given me to do.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
So now, Father, You glorify me by Your side with the glory that I had along with You before the world existed!
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
“I have revealed Your name to the men whom You have given me out of the world. They were Yours and You gave them to me, and they have kept Your word.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
They now know that everything You have given to me is from You;
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
because I have given them the sayings which You have given to me; and they have received and known for sure that I came forth from You, and they have believed that You sent me.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
I am praying for them; I am not praying for the world but for those whom You have given me, because they are yours.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
Actually, all my things are Yours and Yours are mine, and I have been glorified in them.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
Now I am no longer in the world, yet these are in the world, and I am coming to You. “Holy Father, keep them in Your name which You have given to me, so that they may be one just as we are.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
While I was with them in the world I kept them in Your name. I protected those whom You gave me, and not one of them was lost except the son of perdition, so that the Scripture might be fulfilled.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
But now I am coming to You, and I speak these things in the world so that they may have my joy made full in them.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
“I have given them Your word; and the world has hated them because they are not of the world, just as I am not of the world.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
I am not asking that You take them out of the world, but that You keep them from the malignant one.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
They are not of the world, just as I am not of the world.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctify them by Your Truth; Your Word is Truth.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
Just as You sent me into the world, I also have sent them into the world.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
And for their sakes I sanctify myself, so that they also may be sanctified in truth.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
“I pray not only for these, but also for those who believe into me through their word;
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
that they all may be one, just as You, Father, are in me and I in You; that in Us they also may be one, so that the world may believe that You sent me.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
In fact, the glory that You gave to me I have given to them, so that they may be one just as We are one:
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
I in them and You in me, so that they may be perfected into one; also so that the world may know that You sent me, and have loved them just as You have loved me.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
“Father, those whom You have given to me, I desire that they also may be with me where I am, so that they may observe my glory, which You have given me, because You loved me before the founding of the world.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Righteous Father! Indeed the world has not known You, but I have known You; and these have known that You sent me.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
Yes, I have made Your name known to them and will make it known, so that the love with which You have loved me may be in them, and I in them.”