< Yohana 16 >

1 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
“I have spoken these things to you to avoid your being caused to stumble
2 Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
—they will excommunicate you; indeed, a time is coming when anyone who kills you will think he is offering God service!
3 Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
And they will do these things because they have not known either the Father or me.
4 Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
Now I have told you these things so that when the time comes you may remember that I told you about them; I did not tell you these things from the beginning because I was with you.
5 “Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
“Now then, I am going away to Him who sent me, yet none of you asks me, ‘Where are you going?’
6 Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
But because I have said these things to you, sorrow has filled your heart.
7 Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
Nevertheless I am telling you the truth: it is to your advantage that I go away, because if I do not go away the Enabler will not come to you, but if I do go I will send Him to you.
8 Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
“Now when He comes he will convict the world about sin and about righteousness and about judgment:
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
first about sin, because they do not believe into me;
10 kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
then about righteousness, because I am going away to my Father and you will no longer see me;
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
then about judgment, because the ruler of this world has been judged.
12 “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
“I still have many things to say to you but you cannot bear it now.
13 Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
However, when He, the Spirit of the Truth, has come, He will guide you into all the truth; for He will not speak on His own, but He will speak whatever He hears. He will also communicate to you the things that are coming.
14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
He will glorify me because He will take of what is mine and communicate it to you.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
All that the Father has is mine; that is why I said that He takes from what is mine and will communicate it to you.
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
“In just a little you will not see me, and in another little you will see me, because I am going to the Father.”
17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
Then some of His disciples said among themselves: “What is this that He is telling us, ‘In just a little you will not see me, and in another little you will see me,’ and because ‘I am going to the Father’?”
18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
So they said: “What is this ‘little’ that He mentions? We do not know what He is talking about.”
19 Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
Well Jesus knew that they were wanting to question Him and said to them: “Are you inquiring among yourselves about what I said, ‘In just a little you will not see me, and in another little you will see me’?
20 Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
Most assuredly I say to you that you will weep and lament, but the world will rejoice; you will become grieved, but your grief will be turned into joy.
21 Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
When a woman gives birth she has pain, because her time has come; but when the child is born she no longer remembers the anguish, for joy that a human being has been born into the world.
22 Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
So in your turn you are now experiencing grief, but I will see you again and your heart will rejoice, and no one will take your joy from you.
23 Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
In that day you will not question me about anything. “Most assuredly I say to you that whatever you ask the Father in my name He will give you.
24 Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
Until now you have not asked anything in my name. Ask and you will receive, so that your joy may be made full.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
“I have told you these things using figures of speech, but a time is coming when I will no longer talk to you with figures of speech; rather I will tell you plainly about the Father.
26 Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
In that day you will ask in my name; I do not say to you that I will request the Father on your behalf,
27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
because the Father Himself is fond of you, in that you have become fond of me and have believed that I came forth from God.
28 Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
I did come forth from the Father and have come into the world. I am leaving the world again and am going to the Father.”
29 Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
His disciples say to Him: “Hey, now you are speaking plainly and using no figure of speech!
30 Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
Now we know that you know everything and don't need anyone to question you. By this we believe that you came forth from God.”
31 Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
Jesus answered them: “Do you believe now, really?
32 Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
Listen, an hour is coming, actually it has already arrived, that you will be scattered, each to his own, and you will leave me alone. Yet I am not alone, because the Father is with me.
33 Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”
I have spoken these things to you so that in me you may have peace. In the world you have oppression; but take heart, I have conquered the world!”

< Yohana 16 >