< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Et le Seigneur Dieu, continuant à parler à Job dit:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
Est-ce qu'il décline la justice du Tout-Puissant? Celui qui a adressé des reproches au Seigneur doit lui répondre.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Et Job, reprenant, dit au Seigneur:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
Pourquoi m'obstinerais-je à contester? Je me tiens pour averti; j'ai osé blâmer le Seigneur, et j'ai ouï de telles paroles, moi qui ne suis rien! Que pourrais-je répliquer? Je n'ai plus qu'à me mettre la main sur la bouche.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
J'ai parlé une fois; je me garderai bien de parler encore.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Et le Seigneur, continuant, dit à Job, à travers la nuée:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
Nullement, mais ceins-toi les reins comme un homme; je vais te questionner, tu me répondras.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Ne refuse pas mon jugement: crois-tu que j'aie conversé avec toi, sinon pour que tu apparaisses juste?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Ton bras est-il le bras du Seigneur? ta voix est-elle comme son tonnerre?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Revêts-toi de grandeur et de puissance; orne-toi d'honneur et de gloire.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Envoie des anges dans ta colère, humilie tout orgueilleux.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Eteins les vaines splendeurs, fais tomber soudain l'impie en pourriture.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Cache les pécheurs ensemble sous la terre; couvre leurs fronts de honte.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Je confesserai alors que ta main peut sauver.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Mais vois auprès de toi les bêtes fauves; elles se repaissent d'herbe comme les bœufs.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
La vigueur de la bête est dans ses reins; sa force dans ses entrailles.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Elle dresse sa queue comme un cyprès; ses nerfs sont liés entre eux.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
Ses côtes sont des côtes d'airain; son échine est de fer fondu.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
Elle est le commencement de l'œuvre du Seigneur, créée pour être raillée par les anges.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
Lorsqu'elle a gravi sur les cimes des monts, elle a réjoui les quadrupèdes dans le Tartare.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Elle se couche sous toute sorte d'arbre; auprès du papyrus, de l'herbe ou du roseau.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
L'ombre des grands rameaux la couvre, ou les jeunes tiges des champs.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Vienne le flux de la mer, elle ne le sentira pas; elle ne craint rien; le Jourdain même se briserait sur sa gueule.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
D'un coup d'œil elle réprimera son choc; pris au piège, il frémira jusqu'en ses narines.

< Ayubu 40 >