< Ayubu 38 >
1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
and to answer LORD [obj] Job (from *Q(K)*) ([the] tempest *Q(k)*) and to say
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
who? this to darken counsel in/on/with speech without knowledge
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
to gird please like/as great man loin your and to ask you and to know me
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
where? to be in/on/with to found I land: country/planet to tell if to know understanding
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
who? to set: make measurement her for to know or who? to stretch upon her line
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
upon what? socket her to sink or who? to shoot stone corner her
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
in/on/with to sing unitedness star morning and to shout all son: child God
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
and to fence in/on/with door sea in/on/with to burst/come out he from womb to come out: produce
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
in/on/with to set: make I cloud clothing his and cloud swaddling his
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
and to break upon him statute: allotment my and to set: make bar and door
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
and to say till here to come (in): come and not to add and here to set: appoint in/on/with pride heap: wave your
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
from day your to command morning (to know [the] dawn *Q(K)*) place his
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
to/for to grasp in/on/with wing [the] land: country/planet and to shake wicked from her
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
to overturn like/as homer signet and to stand like clothing
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
and to withhold from wicked light their and arm to exalt to break
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
to come (in): come till spring sea and in/on/with search abyss to go: walk
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
to reveal: reveal to/for you gate death and gate shadow to see: see
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
to understand till breadth land: country/planet to tell if to know all her
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
where? this [the] way: direction to dwell light and darkness where? this place his
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
for to take: take him to(wards) border: area his and for to understand path house: home his
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
to know for then to beget and number day your many
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
to come (in): come to(wards) treasure snow and treasure hail to see: see
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
which to withhold to/for time distress to/for day battle and battle
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
where? this [the] way: direction to divide light to scatter east upon land: country/planet
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
who? to divide to/for flood conduit and way: road to/for lightning voice: thunder
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
to/for to rain upon land: country/planet not man: anyone wilderness not man in/on/with him
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
to/for to satisfy devastation and desolation and to/for to spring exit grass
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
there to/for rain father or who? to beget drop dew
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
from belly: womb who? to come out: come [the] ice and frost heaven who? to beget him
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
like/as stone water to hide and face: surface abyss to capture
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
to conspire bond Pleiades or cord Orion to open
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
to come out: send Mazzaroth in/on/with time his and Bear upon son: child her to lead them
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
to know statute heaven if: surely no to set: make rule his in/on/with land: country/planet
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
to exalt to/for cloud voice your and abundance water to cover you
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
to send: depart lightning and to go: went and to say to/for you look! we
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
who? to set: put in/on/with inner parts wisdom or who? to give: give to/for heart understanding
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
who? to recount cloud in/on/with wisdom and bag heaven who? to lie down: lay down
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
in/on/with to pour: pour dust to/for casting and clod to cleave
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
to hunt to/for lion prey and living thing lion to fill
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
for to bow in/on/with habitation to dwell in/on/with booth upon ambush
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
who? to establish: prepare to/for raven food his for (youth his *Q(K)*) to(wards) God to cry to go astray to/for without food