< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
But the Lord, responding to Job from a whirlwind, said:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Who is this that wraps sentences in unskilled words?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gird your waist like a man. I will question you, and you must answer me.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where were you, when I set the foundations of the earth? Tell me, if you have understanding.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Who set its measurements, if you know, or who stretched a line over it?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Upon what have its bases been grounded, and who set forth its cornerstone,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
when the morning stars praised me together, and all the sons of God made a joyful noise?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Who enclosed the sea with doors, when it broke forth as if issuing from the womb,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
when I stationed a cloud as its garment and wrapped it in a mist as if swaddling an infant?
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
I encircled it with my limits, and I positioned its bars and doors.
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
And I said: “This far you will approach, and you will proceed no further, and here you will break your swelling waves.”
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Did you, after your birth, command the birth of the sun and show the sunrise its place?
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
And did you hold the extremities of the earth, shaking them, and have you shaken the impious out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
The seal will be restored like clay, and it will remain in place like a garment.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
From the impious, the light will be taken away, and the exalted arm will be broken.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Have you entered the depths of the sea, and have you taken a walk in the uttermost parts of the abyss?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been opened to you, and have you seen the doors of darkness?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Have you considered the breadth of the earth? If you know all things, reveal them to me.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Which is the way that holds the light, and which is the place of darkness?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
In this way, you might lead each thing to its final place, and understand the paths of its house.
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
So then, did you know when you were to be born? And did you know the number of your days?
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Have you been admitted into the storehouses of the snows, and have you gazed upon the stockpile of the brimstone,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
which I have prepared for the time of the enemy, for the day of the battle and the war?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
In what way is the light scattered, and the heat distributed, over the earth?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Who gave a course to the rainstorms, and a path to the resounding thunder,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
so that it would rain on the earth far from man, in the wilderness where no mortal lingers,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
so that it would fill impassable and desolate places, and would bring forth green plants?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Who is the father of rain, or who conceived the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
From whose womb did the ice proceed, and who created the frost from the air?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
The waters are hardened to become like stone, and the surface of the abyss freezes over.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Will you have the strength to join together the sparkling stars of the Pleiades, or are you able to disperse the circling of Arcturus?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Can you bring forth the morning star, in its time, and make the evening star rise over the sons of the earth?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Do you know the order of heaven, and can you explain its rules here on the earth?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Can you lift up your voice to the clouds, so that an onslaught of waters will cover you?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Can you send forth lightning bolts, and will they go, and on returning, say to you: “Here we are?”
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Who placed discernment in the guts of man, or who gave the rooster intelligence?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Who can describe the rules of the heavens, or who can put to rest the harmony of heaven?
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
When was the dust cast to become the earth, and when were its clods fastened together?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Will you seize prey for the lioness, and will you sustain the lives of her young,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
as they rest in their dens or lie in wait in pits?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Who provides the raven with its meal, when her chicks cry out to God, as they wander around because they have no food?

< Ayubu 38 >