< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
Ta, over dette forfærdes mit Hjerte og farer op fra sit Sted.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Hører, ja hører hans Røsts Drøn og Bulderet, der udgaar af hans Mund.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Han lader det fare ud under al Himmelen og sit Lys over Jordens Flige.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Efter ham brøler Røsten, han tordner med sin Højheds Røst; og han holder dem ikke tilbage, naar hans Røst høres.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Gud tordner vidunderligt med sin Røst; han gør store Ting, og vi kunne ikke kende dem.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Thi han siger til Sneen: Fald til Jorden! og ligesaa til Regnskyllene, ja til hans Vældes Regnskyl.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Han forsegler hver Mands Haand, at alle Folk, som ere hans Skabning, skulle kende det.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Da gaa de vilde Dyr i Hule og blive i deres Boliger.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Fra Syden kommer Stormen, og med Nordenvindene kommer Kulden.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Ved Guds Aande kommer Is, og det brede Vand snævres ind.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Ja, med Fugtighed fylder han Skyen; han udbreder sin lysopfyldte Sky.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Og den vender sig i Kredse, alt som han styrer den til dens Gerning, til alt, hvad han byder den, hen over Jordens Kreds:
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Enten til Revselse eller til hans Lands Bedste eller til Velgerning lader han den ramme.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Job, vend dine Øren til dette; staa stille og agt paa Guds underfulde Ting!
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Ved du, naar Gud tænker derpaa, og naar han lader sin Skys Lys skinne?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Ved du hvorledes Skyerne svæve? de underfulde Ting af ham, som er fuldkommen i al Kundskab?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
du, hvis Klæder blive varme, naar han gør Landet lummert fra Sønden?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Udspænder du med ham de øverste Skyer, der ere faste som et støbt Spejl?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Lad os vide, hvad vi skulle sige til ham! vi kunne ikke fremføre noget ud fra Mørket.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Skal det fortælles ham, at jeg taler? eller mon nogen har ønsket, at han maatte blive opslugt?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Og nu, ser man ikke Lyset, som straaler i de øverste Skyer: Saa farer et Vejr frem og renser dem.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Af Norden kommer Guld; over Gud er der forfærdelig Majestæt.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
Den Almægtige, ham kunne vi ikke naa til, ham, som er stor i Kraft; Ret og Retfærdigheds Fylde undertrykker han ikke.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Derfor frygte Folkene ham; han ser ikke til nogen, som er viis i Hjertet.

< Ayubu 37 >