< Ayubu 35 >

1 Ndipo Elihu akasema:
厄里烏又接著說:
2 “Je, unadhani hili ni haki? Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’
你說過:「我在天主前是正義的。」你想這話合理嗎﹖
3 Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata, na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’
你還說過:「這與你何干﹖我若犯罪,我對你做了什麼﹖」
4 “Ningependa nikujibu wewe pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.
我今答覆你,以及和你在一起的友人。
5 Tazama juu mbinguni ukaone; yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.
請你仰視上天,且要靜觀,細看高於你的蒼天。
6 Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu? Kama dhambi zako zikiwa nyingi, hilo linamfanyia nini Mungu?
你若犯罪,為他有什麼害處﹖你若作惡多端,又能加害他什麼﹖
7 Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini, au yeye anapokea nini mkononi kwako?
如果你為人正義,為他又有何益﹖或者他由你手中獲得什麼﹖
8 Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe, nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.
你的惡行只能加害與你類似的人,你的正義也只能有益於世人。
9 “Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso; huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.
人因受暴虐過甚,必要哀號;因受強權的壓迫,必要呼籲。
10 Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu, yeye anifanyaye niimbe usiku,
但是沒有人說:「那造成我們,使人夜間歡唱,
11 yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia, na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’
使我們比地上的走獸更聰明,使我們比天上的飛鳥更有智慧的天主在那裏﹖」
12 Yeye hajibu wakati watu waliapo kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.
他們雖呼喊,天主卻不答應,這是因為惡人傲慢的原故。
13 Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili; Mwenyezi hayazingatii.
他們空喊亂叫,天主決不俯聽,全能者決不垂視。
14 Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza wewe usemapo humwoni, tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake na wewe lazima umngojee,
何況你說過:「你看不見他;但你的案件已放在他面前,你應等待他!」
15 pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu wala haangalii uovu hata kidogo?
你還說過:「他沒有發怒施罰,似乎不很理會罪過。」
16 Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana; anaongea maneno mengi bila maarifa.”
的確,約伯開口盡說空話;由於無知,說了許多妄言。

< Ayubu 35 >