< Ayubu 34 >
2 “Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
« Écoutez mes paroles, sages. Écoutez-moi, vous qui avez la connaissance.
3 Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
Car l'oreille juge les mots, comme le palais goûte la nourriture.
4 Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
Choisissons pour nous ce qui est juste. Connaissons entre nous ce qui est bon.
5 “Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
Car Job a dit: « Je suis juste », Dieu m'a enlevé mon droit.
6 Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
Malgré mon droit, je suis considéré comme un menteur. Ma blessure est incurable, bien que je sois sans désobéissance.
7 Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
Quel homme est comme Job, qui boit le mépris comme de l'eau,
8 Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
qui fréquente les ouvriers de l'iniquité, et marche avec des hommes méchants?
9 Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
Car il a dit: « Il ne sert à rien à un homme pour qu'il se complaise en Dieu.
10 “Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
« Écoutez-moi donc, hommes d'intelligence: loin de Dieu, qu'il fasse le mal, du Tout-Puissant, pour qu'il commette l'iniquité.
11 Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
Car le travail d'un homme, il le lui rendra, et faire en sorte que chacun trouve selon ses voies.
12 Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
Oui, certainement, Dieu ne fera pas le mal, Le Tout-Puissant ne pervertira pas non plus la justice.
13 Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
Qui l'a mis en charge de la terre? Ou qui l'a établi sur le monde entier?
14 Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
S'il mettait son cœur sur lui-même, s'il rassemblait en lui son esprit et son souffle,
15 wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
toute chair périrait ensemble, et l'homme redeviendrait poussière.
16 “Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
« Si maintenant vous avez de l'intelligence, écoutez ceci. Écoutez la voix de mes mots.
17 Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
Celui qui déteste la justice doit-il gouverner? Condamnerez-vous celui qui est juste et puissant,
18 Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
qui dit à un roi: « Infâme! ou aux nobles, « Méchant! »?
19 yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
Il ne respecte pas la personne des princes, ni respecter les riches plus que les pauvres, car ils sont tous l'œuvre de ses mains.
20 Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
En un instant, ils meurent, même à minuit. Le peuple est ébranlé et disparaît. Les puissants sont emportés sans ménagement.
21 “Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
« Car ses yeux sont sur les voies de l'homme. Il voit toutes ses allées et venues.
22 Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
Il n'y a ni ténèbres, ni obscurité épaisse, où les ouvriers de l'iniquité peuvent se cacher.
23 Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
Car il n'a pas besoin de considérer un homme plus avant, qu'il devrait aller devant Dieu en jugement.
24 Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
Il met en pièces les puissants d'une manière insoupçonnable, et met les autres à leur place.
25 Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
C'est pourquoi il prend connaissance de leurs œuvres. Il les renverse dans la nuit, pour qu'ils soient détruits.
26 Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
Il les frappe comme des méchants à la vue des autres;
27 kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
parce qu'ils se sont détournés de lui, et n'a pas voulu prêter attention à ses manières,
28 Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
et ils ont fait en sorte que le cri des pauvres parvienne jusqu'à lui. Il a entendu le cri des affligés.
29 Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
Quand il donne le calme, qui donc peut condamner? Quand il cache son visage, qui donc peut le voir? Il est au-dessus d'une nation ou d'un homme,
30 ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
afin que l'impie ne règne pas, pour qu'il n'y ait personne pour piéger le peuple.
31 “Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
« Car quelqu'un a-t-il dit à Dieu, Je suis coupable, mais je n'offenserai plus personne.
32 Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
Enseigne-moi ce que je ne vois pas. Si j'ai commis l'iniquité, je ne la commettrai plus »?
33 Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
Sa rétribution sera-t-elle telle que tu la désires, pour que tu la refuses? Car c'est vous qui devez choisir, et non moi. Par conséquent, parlez de ce que vous savez.
34 “Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
Les hommes doués de discernement me le diront, oui, tout homme sage qui m'écoute:
35 ‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
« Job parle sans savoir. Ses paroles sont sans sagesse.
36 Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
Je souhaite que Job soit jugé jusqu'au bout, parce qu'il a répondu comme les méchants.
37 Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”
Car il ajoute la rébellion à son péché. Il frappe ses mains parmi nous, et multiplie ses paroles contre Dieu. »