< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
« Cependant, Job, écoutez mon discours, et écoutez toutes mes paroles.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Voici, j'ai ouvert ma bouche. Ma langue a parlé dans ma bouche.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Mes paroles exprimeront la droiture de mon cœur. Ce que mes lèvres savent, elles le diront sincèrement.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
L'Esprit de Dieu m'a fait, et le souffle du Tout-Puissant me donne la vie.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Si tu peux, réponds-moi. Mettez de l'ordre dans vos paroles devant moi, et levez-vous.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Voici, je suis envers Dieu comme vous l'êtes. Je suis aussi formé à partir de l'argile.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Voici, ma terreur ne vous effraie pas, ma pression ne sera pas non plus lourde pour vous.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
« Tu as parlé à mon oreille, J'ai entendu la voix de tes paroles, disant,
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
Je suis pur, sans désobéissance. Je suis innocent, il n'y a pas d'iniquité en moi.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Voici, il trouve des occasions contre moi. Il me considère comme son ennemi.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
Il met mes pieds dans les ceps. Il marque tous mes chemins.
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
« Voici, je vais te répondre. En cela, tu n'es pas juste, car Dieu est plus grand que l'homme.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Pourquoi vous battez-vous contre lui? parce qu'il ne rend compte d'aucune de ses affaires?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Car Dieu parle une fois, oui deux fois, bien que l'homme n'y prête pas attention.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
Dans un rêve, dans une vision de la nuit, quand le sommeil profond tombe sur les hommes, en somnolant sur le lit,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
alors il ouvre les oreilles des hommes, et scelle leur instruction,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
afin qu'il retire l'homme de son dessein, et cacher l'orgueil de l'homme.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
Il préserve son âme de la fosse, et sa vie de périr par l'épée.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
« Il est aussi châtié par la douleur sur son lit, avec une lutte continuelle dans ses os,
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
de sorte que sa vie a horreur du pain, et son âme une nourriture délicate.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Sa chair est tellement consumée qu'on ne la voit plus. Ses os qui n'ont pas été vus ressortent.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Oui, son âme s'approche de la fosse, et sa vie aux destructeurs.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
« S'il y a à côté de lui un ange, un interprète, un parmi mille, pour montrer à l'homme ce qui est bon pour lui,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
alors Dieu lui fait grâce, et dit, « Délivre-le de la descente dans la fosse. J'ai trouvé une rançon.
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Sa chair sera plus fraîche que celle d'un enfant. Il retourne aux jours de sa jeunesse.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
Il prie Dieu, et il lui est favorable, pour qu'il voie son visage avec joie. Il rend à l'homme sa justice.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Il chante devant les hommes, et dit, J'ai péché, j'ai perverti ce qui était juste, et ça ne m'a pas profité.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
Il a racheté mon âme pour qu'elle n'entre pas dans la fosse. Ma vie va voir la lumière.
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
« Voici que Dieu fait toutes ces choses, deux fois, oui trois fois, avec un homme,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
pour ramener son âme de la fosse, afin qu'il soit éclairé par la lumière des vivants.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Marque bien, Job, et écoute-moi. Gardez le silence, et je parlerai.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Si tu as quelque chose à dire, réponds-moi. Parlez, car je désire vous justifier.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Si ce n'est pas le cas, écoutez-moi. Garde le silence, et je t'enseignerai la sagesse. »