< Ayubu 33 >
1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
“Escucha ahora, oh Job, mi palabra, y a todos mis argumentos presta oído.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
He aquí que abro mi boca; se mueve mi lengua para formar palabras en mi paladar.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
Lo que diré viene de un corazón recto, mis labios profieren la pura verdad.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
El Espíritu de Dios me hizo, y el soplo del Omnipotente me dio vida.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Respóndeme, si puedes; prepárate para (contender) conmigo; tente dispuesto.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Mira, yo soy creatura de Dios, igual que tú; también yo fui formado del barro.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Por eso nada tienes que temer de mí, ni te abrumará el peso de mi persona.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
Ahora bien, tú has dicho oyéndolo yo —bien escuché el son de tus palabras—:
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
«Inocente soy, sin pecado, limpio soy, no hay iniquidad en mí.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
Pero Él busca pretextos contra mí, me considera como enemigo suyo;
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
pone en el cepo mis pies, observa todos mis pasos.»
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
Precisamente en esto no tienes razón; te lo explicaré. Si Dios es más grande que el hombre,
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
¿por qué contiendes con Él, ya que Él no da cuenta de ninguno de sus actos?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
Porque de una manera habla Dios, y también de otra, pero (el hombre) no le hace caso.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
En sueños, en visiones nocturnas, cuando cae letargo sobre los hombres, recostados en sus camas,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
entonces Él abre el oído del hombre, y le instruye en forma secreta,
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
para apartarle de su obra. Así le retrae de la soberbia,
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
salva su alma de la perdición, y su vida del filo de la espada.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
Corrige también al hombre con dolores en su lecho, y con continua angustia dentro de sus huesos;
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
de modo que tiene asco del pan y del bocado más exquisito.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Vase consumiendo su carne hasta desaparecer, y aparecen sus huesos que no se veían.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
Se acerca su vida al sepulcro, y su existencia a los que la quitan.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
Pero si hay para él un ángel, un intercesor de entre mil, que explique al hombre su deber;
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
y que se compadezca de él y diga (a Dios): «Líbrale para que no baje al sepulcro; yo he hallado el rescate (de su alma).»
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Entonces se vuelve más fresca que la de un niño su carne; será como en los días de su juventud;
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
implora a Dios, y Este le es propicio. Así contemplará con júbilo su rostro, y (Dios) le devuelve su justicia.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
Cantará entonces entre los hombres, y dirá: «Yo había pecado, había pervertido la justicia, y no me fue retribuido según merecía;
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
pues Él me libró del paso al sepulcro, y mi alma ve todavía la luz.»
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Mira, todo esto hace Dios, dos y aun tres veces con el hombre,
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
a fin de retraerlo de la muerte, y alumbrarlo con la luz de la vida.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Atiende, Job; escúchame; calla, que yo hablaré.
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
Si tienes algo que decir, respóndeme; habla, pues mi deseo es verte justo.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
Si no, escúchame en silencio, y yo te enseñaré sabiduría.”