< Ayubu 33 >

1 “Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
Now listen to me, Job. Pay attention to everything I have to say.
2 Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
Look, I'm about to speak; my mouth is ready to talk.
3 Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
My words come from my upright heart; my lips speak sincerely of what I know.
4 Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
The spirit of God made me, and the breath of the Almighty gives me life.
5 Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
Answer me, if you can. Stand in front of me and prepare to defend yourself.
6 Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
Look, before God we are both the same. I was also made from a piece of clay.
7 Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
See here, you don't need to be frightened of me. I won't be too hard on you.
8 “Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
You spoke in my hearing and I have listened to everything you had to say.
9 ‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
You say, ‘I'm clean, I've done nothing wrong; I'm pure, I have not sinned.
10 Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
See how God finds fault with me and treats me as his enemy.
11 Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
He puts my feet in the stocks and watches everything I do.’
12 “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
But look, you are wrong—let me explain. God is greater than any human being.
13 Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
Why are you fighting against him, complaining that God isn't answering your questions?
14 Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
God speaks over and over again, but people don't notice.
15 Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
Through dreams and visions in the night, when people fall into deep sleep, resting on their beds,
16 anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
God speaks to them with solemn warnings
17 ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
to turn them away from doing wrong and to stop them from becoming proud.
18 kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
He saves them from the grave and spares them from violent death.
19 Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
People are also disciplined on a bed of pain with constant aching in their bones.
20 kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
They have no desire to eat; they do not even want their favorite dishes.
21 Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
Their flesh wastes away to nothing; all that's left is skin and bones.
22 Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
They are close to death; their lives approaching the executioner.
23 “Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
But if an angel appears, a mediator, one of God's thousands of angels, to tell someone the right way for them,
24 kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
he will be gracious to them. He will say, ‘Save them from going down into the grave, for I have found a way to free them.’
25 ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
Then their bodies will be renewed as if they were young again; they will be as strong as when they were in their prime.
26 Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
They will pray to God, and he will accept them; they come into God's presence with joy, and he will set things right for them.
27 Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
They sing, and tell others, ‘I sinned, I distorted what is right, but it did not do me any good.
28 Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
He saved me from going down into the grave and I will live in the light.’
29 “Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
Look, God does this time and again for people;
30 ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
he saves them from the grave so they might see the light of life.
31 “Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
Pay attention Job, and listen to me! Be quiet—let me speak!
32 Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
But if you have anything to say, then speak up.
33 Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”
If not, listen to me. Keep quiet and I will teach you wisdom.”

< Ayubu 33 >