< Ayubu 24 >
1 “Kwa nini Mwenyezi asiweke nyakati kwa ajili ya hukumu? Kwa nini wale wamjuao wazitafute siku kama hizo bila mafanikio?
Why doesn't the Almighty set a definite time to punish the wicked? Why don't those who follow him never see him act in judgment?
2 Watu husogeza mawe ya mpaka; huchunga makundi ya wanyama waliyonyangʼanya kwa nguvu.
The wicked move boundary stones; they seize other people's flocks and move them to their own pastures.
3 Huwanyangʼanya yatima punda wao, na kumchukua rehani fahali wa mjane.
They steal the orphan's donkey; they take the widow's ox as security for a debt.
4 Humsukuma mhitaji kutoka njia, na kuwafanya maskini wote wa nchi kulazimika kujificha.
They push the poor out of their way; the destitute are forced to hide from them.
5 Kama punda-mwitu jangwani, maskini huzunguka katika kazi zao za kutafuta chakula; mahali palipo jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
Like wild donkeys in the desert, the poor have to scavenge for their food, looking for anything to feed their children in the wasteland.
6 Hukusanya chakula mashambani na kuokota masazo katika mashamba ya mizabibu ya waovu.
They are forced to find what they can in other people's fields, to glean among the vineyards of the wicked.
7 Kwa kukosa nguo, usiku kucha hukaa uchi; hawana chochote cha kujifunika baridi.
They spend the night naked because they have no clothes; they have nothing to cover themselves against the cold.
8 Hutota kwa mvua za mlimani, nao huikumbatia miamba kwa ajili ya kukosa pa kujisitiri.
They are soaked by the cold mountain storms, and huddle beside the rocks for shelter.
9 Mtoto yatima hupokonywa matitini; mtoto wachanga wa maskini hunyakuliwa kwa ajili ya deni.
Fatherless children are snatched from their mother's breasts, taking the babies of the poor as security for a debt.
10 Kwa kukosa nguo, hutembea uchi; hubeba miganda ya ngano, lakini huwa na njaa.
Because they have no clothes to wear they have to go naked, harvesting sheaves of grain while they themselves are hungry.
11 Hukamua zeituni katika mawe ya kusagia; hukanyaga mashinikizo, lakini wanaona kiu.
In the olive groves they work to produce oil, but do not taste it; they tread the winepress, but are thirsty.
12 Kilio cha huzuni cha wanaokufa kinapaa kutoka mjini, nazo nafsi za waliojeruhiwa zinalilia msaada. Lakini Mungu hamlaumu mtu yeyote kwa kutenda mabaya.
In the city the dying groan, and the wounded cry for help, but God ignores their prayers.
13 “Wako wale wanaoiasi nuru, wasiofahamu njia zake wala hawakai katika mapito yake.
These are people who rebel against the light. They do not want to know its ways, or to stay on its paths.
14 Wakati mwanga wa mchana unapotoweka, muuaji huinuka naye huwaua maskini na mhitaji; wakati wa usiku hunyemelea kama mwizi.
The murderer gets up at dawn to kill the poor and needy, and when night falls he becomes a thief.
15 Jicho la mzinzi hungojea wakati wa giza, naye hufikiri, ‘Hakuna jicho litakaloniona,’ naye huuficha uso wake.
The adulterer waits for dusk, saying to himself, ‘No one will see me now,’ and he covers his face.
16 Katika giza, huvunja majumba, lakini wakati wa mchana hujifungia ndani; hawataki kufanya lolote nuruni.
Thieves break into houses during the night and they sleep during the day. They don't even know what the light is like!
17 Kwa wote hawa, giza nene ndiyo asubuhi yao; hujifanya rafiki na vitisho vya gizani.
Total darkness is like light to them, for they are familiar with the night.
18 “Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.
Like bubbles on the surface of a river they are quickly carried away. The land they own is cursed by God. They don't enter their own vineyards.
19 Kama vile joto na hari vinyakuavyo theluji iliyoyeyuka, ndivyo kuzimu kuwanyakuavyo waliotenda dhambi. (Sheol )
Just as heat and drought dry up snowmelt, so Sheol takes away those who have sinned. (Sheol )
20 Tumbo lililowazaa huwasahau, nao huwa karamu ya mabuu; watu waovu hawakumbukwi tena, lakini huvunjika kama mti.
Even their mothers forget them, maggots feast on them, they are no longer remembered, and their wickedness becomes like a tree that is broken into pieces.
21 Huwafanya mawindo wanawake tasa na wasio na watoto, nao hawaonyeshi huruma kwa wajane.
They mistreat childless women and are mean to widows.
22 Lakini Mungu huwakokota wenye nguvu kwa uwezo wake; ingawa wamestawi, hawana hakika ya maisha.
God prolongs the life of the wicked by his power; but when they arise, they have no assurance of life.
23 Aweza akawaacha wakapumzika wakijihisi salama, lakini macho yake yanaona njia zao.
He supports them and gives them security, but he is always watching what they're doing.
24 Kwa kitambo kidogo hutukuka, hatimaye hutoweka; hushushwa na kukusanywa kama wengine wote, hukatwa kama masuke ya nafaka.
Though they may be illustrious for a while, soon they are gone. They are brought down like all others, cut off like the heads of grain.
25 “Kama hili sivyo, ni nani awezaye kunithibitisha kuwa mwongo, na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?”
If this isn't so, who can prove I'm a liar and there's nothing to what I say?”