< Ayubu 30 >

1 “Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
But now they that are younger than I have me in derision, whose fathers I would have disdained to have set with the dogs of my flock.
2 Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
Yea, whereto might the strength of their hands profit me, in whom old age was perished?
3 Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
For lack and famine they were solitary; fleeing into the wilderness in former time desolate and waste.
4 Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
Who cut up mallows by the bushes, and juniper roots for their food.
5 Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
They were driven forth from among men, (they cried after them as after a thief; )
6 Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
To dwell in the cliffs of the valleys, in caves of the earth, and in the rocks.
7 Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
Among the bushes they brayed; under the nettles they were gathered together.
8 Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
They were children of fools, yea, children of base men: they were viler than the earth.
9 “Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
And now am I their song, yea, I am their byword.
10 Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
They detest me, they flee far from me, and spare not to spit in my face.
11 Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
Because he has loosed my cord, and afflicted me, they have also let loose the bridle before me.
12 Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
Upon my right hand rise the youth; they push away my feet, and they raise up against me the ways of their destruction.
13 Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
They ruin my path, they set forward my calamity, they have no helper.
14 Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
They came upon me as a wide breaking in of waters: in the desolation they rolled themselves upon me.
15 Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
Terrors are turned upon me: they pursue my soul as the wind: and my welfare passes away as a cloud.
16 “Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
And now my soul is poured out upon me; the days of affliction have taken hold upon me.
17 Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
My bones are pierced in me in the night season: and my sinews take no rest.
18 Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
By the great force of my disease is my garment changed: it binds me about as the collar of my coat.
19 Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
He has cast me into the mire, and I am become like dust and ashes.
20 “Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
I cry unto you, and you do not hear me: I stand up, and you regard me not.
21 Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
You are become cruel to me: with your strong hand you oppose yourself against me.
22 Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
You lift me up to the wind; you cause me to ride upon it, and dissolve my substance.
23 Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
For I know that you will bring me to death, and to the house appointed for all living.
24 “Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
Nevertheless he will not stretch out his hand to the grave, though they cry in his destruction.
25 Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
Did not I weep for him that was in trouble? was not my soul grieved for the poor?
26 Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
When I looked for good, then evil came unto me: and when I waited for light, there came darkness.
27 Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
My bowels boiled, and rested not: the days of affliction prevented me.
28 Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
I went mourning without the sun: I stood up, and I cried in the congregation.
29 Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
I am a brother to dragons, and a companion to owls.
30 Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
My skin is black upon me, and my bones are burned with heat.
31 Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.
My harp also is turned to mourning, and my organ into the voice of them that weep.

< Ayubu 30 >