< Ayubu 32 >

1 Basi watu hawa watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa kuwa alikuwa mwadilifu machoni pake mwenyewe.
So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
2 Lakini Elihu mwana wa Barakeli, wa kabila la Buzi wa jamaa ya Ramu, akamkasirikia sana Ayubu, kwa sababu ya kujihesabia haki mwenyewe badala ya Mungu.
Then was kindled the wrath of Elihu the son of Barachel the Buzite, of the kindred of Ram: against Job was his wrath kindled, because he justified himself rather than God.
3 Pia aliwakasirikia hao rafiki watatu wa Ayubu, kwa sababu hawakuweza kupata njia ya kuthibitisha ya kuwa hayo maneno ya Ayubu hayakuwa ya kweli, nao bado walikuwa wamemlaumu.
Also against his three friends was his wrath kindled, because they had found no answer, and yet had condemned Job.
4 Basi Elihu alikuwa amesubiri kwanza waongee na Ayubu kwa sababu walikuwa na umri mkubwa kumliko yeye.
Now Elihu had waited till Job had spoken, because they were elder than he.
5 Lakini alipoona watu hao watatu hawakuwa na kitu zaidi cha kusema, hasira yake ikaamka.
When Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, then his wrath was kindled.
6 Basi Elihu mwana wa Barakeli wa kabila la Buzi akasema: “Mimi ni mdogo kwa umri, nanyi ni wazee; ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua.
And Elihu the son of Barachel the Buzite answered and said, I am young, and all of you are very old; wherefore I was afraid, and durst not show you mine opinion.
7 Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’
I said, Days should speak, and multitude of years should teach wisdom.
8 Lakini ni Roho iliyoko ndani ya mwanadamu, pumzi ya Mwenyezi, ndiyo impayo yeye ufahamu.
But there is a spirit in man: and the inspiration of the Almighty gives them understanding.
9 Sio wazee peke yao walio na hekima, sio wenye umri mkubwa peke yao wanaofahamu lililo sawa.
Great men are not always wise: neither do the aged understand judgment.
10 “Kwa hiyo nasema: Nisikilizeni mimi; mimi nami nitawaambia lile ninalojua.
Therefore I said, Hearken to me; I also will show mine opinion.
11 Nilingojea mlipokuwa mnaongea, nilizisikiliza hoja zenu; mlipokuwa mkitafuta maneno ya kusema,
Behold, I waited for your words; I gave ear to your reasons, whilst all of you searched out what to say.
12 niliwasikiliza kwa makini. Lakini hakuna hata mmoja wenu aliyethibitisha kwamba Ayubu amekosa; hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kujibu hoja zake.
Yea, I attended unto you, and, behold, there was none of you that convinced Job, or that answered his words:
13 Msiseme, ‘Tumepata hekima; Mungu na amthibitishe kuwa mwongo, wala si mwanadamu.’
Lest all of you should say, We have found out wisdom: God thrusts him down, not man.
14 Lakini Ayubu hajayapanga maneno yake dhidi yangu, nami sitamjibu kwa kutumia hoja zenu.
Now he has not directed his words against me: neither will I answer him with your speeches.
15 “Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
They were amazed, they answered no more: they left off speaking.
16 Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
When I had waited, (for they spoke not, but stood still, and answered no more; )
17 Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
I said, I will answer also my part, I also will show mine opinion.
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
For I am full of matter, the spirit within me constrains me.
19 ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
Behold, my belly is as wine which has no vent; it is ready to burst like new bottles.
20 Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
I will speak, that I may be refreshed: I will open my lips and answer.
21 Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
Let me not, I pray you, accept any man's person, neither let me give flattering titles unto man.
22 kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
For I know not to give flattering titles; in so doing my maker would soon take me away.

< Ayubu 32 >