< Ayubu 29 >
1 Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
Siguió Job explicando y dijo:
2 “Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
“¡Ojalá volviera a ser como en los meses pasados, como en los días en que Dios me protegía,
3 wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
cuando su luz brillaba sobre mi cabeza, y su luz me guiaba en las tinieblas!
4 Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
¿Cuál era en la madurez de mi vida, cuando era amigo de Dios y Este guardaba mi morada;
5 wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
cuando el Todopoderoso estaba conmigo, y me rodeaban mis hijos;
6 wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
cuando lavaba mis pies con leche, y de la roca me brotaban ríos de aceite.
7 “Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
(En aquel tiempo) cuando yo salía a la puerta de la ciudad, y en la plaza establecía mi asiento,
8 vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
los jóvenes al verme se retiraban, y los ancianos se levantaban, y se mantenían en pie.
9 wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
Los príncipes contenían la palabra, y ponían su mano sobre la boca.
10 wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
Se callaba la voz de los magnates y su lengua se pegaba a su paladar.
11 Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
El que me escuchaba, me llamaba dichoso, y el ojo que me veía, daba señas en favor mío.
12 kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
Yo libraba al pobre que pedía auxilio, y al huérfano que no tenía sostén.
13 Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
Sobre mí venía la bendición del que hubiera perecido, y yo alegraba el corazón de la viuda.
14 Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
Me revestía de justicia, y esta me revestía a mí, mi equidad me servía de manto y tiara.
15 Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
Era yo ojo para el ciego, y pie para el cojo,
16 Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
padre de los pobres, que examinaba con diligencia aun la causa del desconocido.
17 Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
Quebraba los colmillos del malvado, y de sus dientes arrancaba la presa.
18 “Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
Por lo cual me decía: «Moriré en mi nido, y mis días serán tan numerosos como la arena;
19 Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
mi raíz se extenderá hacia las aguas, y el rocío pasará la noche en mis hojas.
20 Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
Será siempre nueva en mí la gloria mía, y mi arco se renovará en mi mano.»
21 “Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
A mí me escuchaban sin perder la paciencia, aguardando silenciosamente mi consejo.
22 Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
Después de hablar ya no respondía nadie, porque (cual rocío) caían sobre ellos mis palabras.
23 Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
Me esperaban como se espera la lluvia, abrían su boca como a la lluvia tardía.
24 Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
Si les sonreía estaban admirados, y se alegraban de esa luz de mi rostro.
25 Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.
Yo decidía su conducta y me sentaba a la cabecera, habitaba como un rey entre sus tropas, cual consolador un medio de los afligidos.”