< Ayubu 26 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Alors Job prit la parole et dit:
2 “Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
Comme tu sais venir en aide à la faiblesse, prêter secours au bras sans force!
3 Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
Comme tu conseilles bien l'ignorant! Quelle abondance de sagesse tu fais paraître!
4 Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
A qui adresses-tu des paroles? Et de qui est l'esprit qui sort de ta bouche?
5 “Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
Devant Dieu, les ombres tremblent sous les eaux et leurs habitants.
6 Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
Le schéol est à nu devant lui, et l'abîme n'a point de voile. (Sheol h7585)
7 Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
Il étend le septentrion sur le vide, il suspend la terre sur le néant.
8 Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
Il renferme les eaux dans ses nuages, et les nues ne se déchirent pas sous leur poids.
9 Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
Il voile la face de son trône, il étend sur lui ses nuées.
10 Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
Il a tracé un cercle à la surface des eaux, au point de division de la lumière et des ténèbres.
11 Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
Les colonnes du ciel s'ébranlent, et s'épouvantent à sa menace.
12 Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
Par sa puissance il soulève la mer, par sa sagesse il brise l'orgueil.
13 Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
Par son souffle le ciel devient serein, sa main a formé le serpent fuyard.
14 Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”
Tels sont les bords de ses voies, le léger murmure que nous en percevons; mais le tonnerre de sa puissance, qui pourra l'entendre?

< Ayubu 26 >