< Ayubu 20 >

1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
納阿瑪人左法爾答覆說:
2 “Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu, kwa sababu nimehangaika sana.
因我的思潮起伏,叫我答覆,為此我內心十分急躁。
3 Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima, nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.
斥責辱罵我的話,我已聽到,我的理智催迫我答覆。
4 “Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
你豈不知道,自古以來,自從世上有人以來,
5 macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
惡人的歡欣決不久長,無神者的喜樂瞬息即逝﹖
6 Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
他的驕傲雖高頂蒼天,他的頭雖插入青雲,
7 ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
但他必像幻像,永歸無有;見過他的人必說:「他那裏去了﹖」
8 Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
他又像夢境消散,無蹟可尋;又像夜夢,消失無蹤。
9 Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
見過他的眼,再也見不到他;他的住所,再也不認識他。
10 Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.
他的兒子要賠償窮人的損害,他要親手把財物交還。
11 Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
他的骨骸雖富有魄力,但要同他一起埋於塵埃。
12 “Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
邪惡在他口中雖覺甘甜,藏在他的舌下,
13 ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
他雖愛惜不捨,久久含在口中;
14 Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.
但那食物在他腹中要起變化,在他五內要變成蛇的毒汁。
15 Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.
他併吞的財富,必要吐出,天主必使之由他腹中嘔出。
16 Atanyonya sumu za majoka; meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.
他原吸入了蛇的毒汁,毒蛇的舌頭必將他殺死。
17 Hatafurahia vijito, mito inayotiririsha asali na siagi.
他不得觀賞油流如溪,也看不到那流蜜流奶的小河。
18 Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila; hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.
他勞力之所得,應該退還,不得吞下;賺來的財富,不得享用。
19 Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu; amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.
因為它壓搾了窮人,使他們無依;強佔了人家的房屋,不得再建。
20 “Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana; hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.
因為他口腹之慾總不知足,他所喜愛之物,也救不了他。
21 Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale; kufanikiwa kwake hakutadumu.
沒有什麼能逃脫他的吞噬,他的幸福決不久長。
22 Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.
他財產富足時,卻不免拮据,各種的困苦齊集他身。
23 Atakapokuwa amelijaza tumbo lake, Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake, na kumnyeshea mapigo juu yake.
當他肚腹飽滿時,天主的怒火突然降到,箭如雨點射在他身上。
24 Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma, mshale wa shaba utamchoma.
他逃避過鐵器,銅矢必將他射穿。
25 Atauchomoa katika mgongo wake, ncha ingʼaayo kutoka ini lake. Vitisho vitakuja juu yake;
一箭由他的脊背穿透,光亮的箭矢由他的膽囊穿出,死亡的恐怖已落在他身上。
26 giza nene linavizia hazina zake. Moto usiopepewa na mtu utamteketeza, na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.
層層黑暗留作他的寶藏,非人燃起的火要焚燒他,吞盡留在他帳幕的人。
27 Mbingu zitaweka wazi hatia yake, nayo nchi itainuka kinyume chake.
天要彰顯他的罪惡,地也起來攻擊他。
28 Mafuriko yataichukua nyumba yake, maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
洪水沖走他的住宅,在天主義怒之日要全被沖去。
29 Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu, urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”
這是惡人由天主所應得的一份,是天主為他所注定的產業。

< Ayubu 20 >