< Ayubu 19 >
2 “Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
“¿Hasta cuándo afligiréis mi alma, y queréis majarme con palabras?
3 Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
Ya diez veces me habéis insultado, y no os avergonzáis de ultrajarme.
4 Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
Aunque yo realmente haya errado, soy yo quien pago mi error.
5 Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
Si queréis alzaros contra mí, alegando en mi desfavor mi oprobio,
6 basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
sabed que es Dios quien me oprime, y me ha envuelto en su red.
7 “Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
He aquí que alzo el grito por ser oprimido, pero nadie me responde; clamo, pero no hay justicia.
8 Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
Él ha cerrado mi camino, y no puedo pasar; ha cubierto de tinieblas mis sendas.
9 Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
Me ha despojado de mi gloria, y de mi cabeza ha quitado la corona.
10 Amenibomoa kila upande hadi nimeisha; amelingʼoa tegemeo langu kama mti.
Me ha arruinado del todo, y perezco; desarraigó, como árbol, mi esperanza.
11 Hasira yake imewaka juu yangu; amenihesabu kuwa miongoni mwa adui zake.
Encendió contra mí su ira, y me considera como enemigo suyo.
12 Majeshi yake yananisogelea kwa nguvu; yamenizingira, yamepiga kambi kulizunguka hema langu.
Vinieron en tropel sus milicias, se abrieron camino contra mí y pusieron sitio a mi tienda.
13 “Amewatenga ndugu zangu mbali nami; wale tunaojuana nao wamefarakana nami kabisa.
A mis hermanos los apartó de mi lado, y mis conocidos se retiraron de mí.
14 Watu wa jamaa yangu wamekwenda mbali; rafiki zangu wamenisahau.
Me dejaron mis parientes, y mis íntimos me han olvidado.
15 Wageni wangu na watumishi wangu wa kike wananiona kama mgeni; wananitazama kama mgeni.
Los que moran en mi casa, y mis criadas me tratan como extraño; pues soy un extranjero a sus ojos.
16 Namwita mtumishi wangu, wala haitiki, ingawa namwomba kwa kinywa changu mwenyewe.
Llamo a mi siervo, y no me responde, por más que le ruegue con mi boca.
17 Pumzi ya kinywa changu ni kinyaa kwa mke wangu; nimekuwa chukizo mno kwa ndugu zangu mwenyewe.
Mi mujer tiene asco de mi hálito, y para los hijos de mis entrañas no soy más que hediondez.
18 Hata watoto wadogo hunidhihaki; ninapojitokeza, hunifanyia mzaha.
Me desprecian hasta los niños; si intento levantarme se mofan de mí.
19 Rafiki zangu wa moyoni wote wananichukia kabisa; wale niwapendao wamekuwa kinyume nami.
Todos los que eran mis confidentes me aborrecen, y los que yo más amaba se han vuelto contra mí.
20 Mimi nimebaki mifupa na ngozi tu; nimeponea nikiwa karibu kufa.
Mis huesos se pegan a mi piel y a mi carne, y tan solo me queda la piel de mis dientes.
21 “Nihurumieni, rafiki zangu, kuweni na huruma, kwa kuwa mkono wa Mungu umenipiga.
¡Compadeceos de mí, compadeceos de mí, a lo menos vosotros, amigos míos, pues la mano de Dios me ha herido!
22 Kwa nini mnanifuatia kama Mungu afanyavyo? Hamtosheki kamwe na mwili wangu?
¿Por qué me perseguís como Dios, y ni os hartáis de mi carne?
23 “Laiti maneno yangu yangewekwa kwenye kumbukumbu, laiti kwamba yangeandikwa kwenye kitabu,
¡Oh! que se escribiesen mis palabras y se consignaran en un libro,
24 kwamba yangechorwa kwenye risasi kwa kifaa cha chuma, au kuyachonga juu ya mwamba milele!
que con punzón de hierro y con plomo se grabasen en la peña para eterna memoria!
25 Ninajua kwamba Mkombozi wangu yu hai, naye kwamba mwishoni atasimama juu ya nchi.
Mas yo sé que vive mi Redentor, y que al fin se alzará sobre la tierra.
26 Nami baada ya ngozi yangu kuharibiwa, bado nikiwa na mwili huu nitamwona Mungu;
Después, en mi piel, revestido de este (mi cuerpo) veré a Dios (de nuevo) desde mi carne.
27 mimi nitamwona kwa macho yangu mwenyewe: mimi, wala si mwingine. Tazama jinsi moyo wangu unavyomtamani sana!
Yo mismo le veré; le verán mis propios ojos, y no otro; por eso se consumen en mí mis entrañas.
28 “Kama mkisema, ‘Tazama tutakavyomwinda, maadamu mzizi wa tatizo uko ndani yake,’
Vosotros diréis entonces: «¿Por qué lo hemos perseguido?» Pues quedará descubierta la justicia de mi causa.
29 ninyi wenyewe uogopeni upanga, kwa kuwa ghadhabu italeta adhabu kwa upanga, nanyi ndipo mtakapojua kwamba kuna hukumu.”
Temed la espada, porque terribles son las venganzas de la espada; para que sepáis que hay un juicio.”