< Ayubu 16 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Y respondió Job, y dijo:
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
Muchas veces he oído cosas como estas; consoladores molestos sois todos vosotros.
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
¿Tendrán fin las palabras ventosas? O ¿qué es lo que te anima a responder?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
También yo hablaría como vosotros. Deseo que vuestra alma estuviera en lugar de la mía, que yo os tendría compañía en las palabras, y sobre vosotros movería mi cabeza.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
Pero yo os alentaría con mis palabras, y la consolación de mis labios detendría el dolor.
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
Mas si hablo, mi dolor no cesa; y si dejo de hablar, no se aparta de mí.
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
Pero ahora me ha fatigado; has tú asolado toda mi compañía.
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
Tú me has arrugado; el testigo es mi magrez, que se levanta contra mí para testificar en mi rostro.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
Su furor me arrebató, y me ha sido contrario; crujió sus dientes contra mí; contra mí aguzó sus ojos mi enemigo.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
Abrieron contra mí su boca; hirieron mis mejillas con afrenta; contra mí se juntaron todos.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
Me ha entregado Dios al mentiroso, y en las manos de los impíos me hizo temblar.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
Próspero estaba, y me desmenuzó; y me arrebató por la cerviz, y me despedazó, y me puso por blanco suyo.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
Me cercaron sus flecheros, partió mis riñones, y no perdonó; mi hiel derramó por tierra.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
Me quebrantó de quebranto sobre quebranto; corrió contra mí como un gigante.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
Yo cosí saco sobre mi piel, y cargué mi cabeza de polvo.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
Mi rostro está enlodado con lloro, y mis párpados entenebrecidos;
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
a pesar de no haber iniquidad en mis manos, y de haber sido limpia mi oración.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
¡Oh tierra! No cubras mi sangre, y no haya lugar donde se esconda mi clamor.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Por cierto aún ahora en los cielos está mi testigo, y mi testigo en las alturas.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
Mis disputadores son mis amigos; mas a Dios destilarán mis ojos.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
¡Deseo que pudiese disputar el hombre con Dios, como puede con su prójimo!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
Mas los años contados vendrán, y yo andaré el camino por donde no volveré.

< Ayubu 16 >