< Ayubu 16 >
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
“Ya he oído todo esto antes. ¡Son consoladores que sólo causan problemas!
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
¿No cesarán sus discursos que son como el viento? ¿Qué les molesta tanto como para que tengan que responderme?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
Podría hablar como si ustedes estuvieran en mi lugar, encadenando palabras para criticarlos, ridiculizándolos con un movimiento de cabeza.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
Podría edificarlos con mi boca diciendo palabras; el movimiento de mis labios aliviaría su dolor.
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
Para mí, si hablo no se alivia mi dolor, y si no hablo el dolor sigue ahí.
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
“Dios, me has agotado. Has destruido a toda mi familia.
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
Me has hecho marchitar, lo cual es un testimonio contra mí; mi cuerpo delgado atestigua contra mí.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
Me ha desgarrado en su cólera; en su hostilidad ha rechinado los dientes contra mí; mi enemigo me atraviesa con su mirada feroz.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
La gente me mira con la boca abierta, me abofetean en las mejillas para burlarse de mí, se agolpan a mi alrededor para atacarme.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
Dios me ha entregado a la gente malvada; me ha arrojado en sus manos.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
“Yo vivía en paz y él me hizo pedazos. Me agarró por el cuello y me hizo pedazos. Me ha convertido en su blanco.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
Sus arqueros me rodean. Sus flechas atraviesan mis riñones sin piedad. Derrama mi hiel por el suelo.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
Como un muro me derriba, brecha tras brecha, se abalanza sobre mí como un guerrero.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
He sembrado tela de silicio para cubrir mi piel; mi fuerza yace rota en el polvo.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
Mi cara está roja de tanto llorar y sombras oscuras rodean mis ojos,
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
aunque no he hecho nada malo y mi oración es pura.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
“Tierra, no cubras mi sangre. Que mi grito no encuentre lugar para esconderse.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Mira, ahora mismo mi testigo está en el cielo; el que habla por mí está en las alturas.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
Mis amigos me desprecian, pero mis ojos derraman lágrimas ante Dios.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
Quiero que mi testigo hable por mí ante Dios como quien habla por su amigo.
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
Porque dentro de pocos años andaré por ese camino del que no volveré”.