< Ayubu 16 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
Then Job answered and said,
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
“I have heard many such things; you are all miserable comforters.
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Will useless words ever have an end? What is wrong with you that you answer like this?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also could speak as you do, if you were in my place; I could collect and join words together against you and shake my head at you in mockery.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
I would strengthen you with my mouth, and the quivering of my lips will bring you relief!
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
If I speak, my grief is not lessened; if I keep from speaking, how am I helped?
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
But now, God, you have made me weary; you have made all my family desolate.
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
You have made me dry up, which itself is a witness against me; the leanness of my body rises up against me, and it testifies against my face.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
God has torn me in his wrath and persecuted me; He grinds his teeth in rage; my enemy fastens his eyes on me as he tears me apart.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
People have gaped with open mouth at me; they have hit me reproachfully on the cheek; they have gathered together against me.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
God hands me over to ungodly people, and throws me into the hands of wicked people.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
I was at ease, and he broke me apart. Indeed, he has taken me by the neck and dashed me to pieces; he has also set me up as his target.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
His archers surround me all around; God pierces my kidneys and does not spare me; he pours out my bile on the ground.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He smashes through my wall again and again; he runs upon me like a warrior.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
I have sewn sackcloth on my skin; I have thrust my horn into the ground.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face is red with weeping; on my eyelids is the shadow of death
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
although there is no violence in my hands, and my prayer is pure.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
Earth, do not cover up my blood; let my cry have no resting place.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Even now, see, my witness is in heaven; he who vouches for me is on high.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
My friends scoff at me, but my eye pours out tears to God.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
I ask for that witness in heaven to argue for this man with God as a man does with his neighbor!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
For when a few years have passed, I will go to a place from where I will not return.

< Ayubu 16 >