< Ayubu 16 >
Then responded Job, and said: —
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
I have heard many such things, Wearisome comforters, are ye all!
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Is there to be an end to windy words? Or what so strongly exciteth thee, that thou must respond?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also, like you, could speak, —If your soul were in the place of my soul, I could string together words against you, and could therewith shake over you my head.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
I could make you determined, by my mouth, and then my lip-solace should restrain you.
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
Though I do speak, unassuaged is my stinging pain, —And, if I forbear, of what am I relieved?
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
But, now, hath he wearied me, thou hast destroyed all my family;
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
And, having captured me, it hath served, as a witness; and so my wasting away hath risen up against me, in my face, it answereth.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
His anger, hath torn and persecuted me, He hath gnashed upon me with his teeth, Mine adversary, hath sharpened his eyes for me.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
They have gaped upon me with their mouth, With reproach, have they smitten my cheek, Together, against me, have they closed their ranks.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
GOD doth abandon me to him that is perverse, and, into the hands of the lawless, he throweth me headlong.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
At ease, was I when he shattered me, Yea he seized me by my neck, and dashed me in pieces, then set me up for himself as a mark:
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
His archers came round against me, He clave asunder my reins, and spared not, He poured out, on the earth, my gall:
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He made a breach in me, breach upon breach, He ran upon me, like a mighty man.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
Sackcloth, sewed I on my skin, and rolled—in the dust—my horn:
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face, is reddened from weeping, and, upon mine eyelashes, is the death-shade: —
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
Though no violence was in my hands, and, my prayer, was pure.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
O earth! do not cover my blood, and let there be no place for mine outcry.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Even now, lo! in the heavens, is my witness,
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
And, he that voucheth for me is on high. My friends are, they who scorn me, Unto GOD, hath mine eye shed tears: —
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
That one might plead, for a man, with GOD, —Even a son of man, for his friend!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
When, a few years, come, then, by a path by which I shall not return, shall I depart.