< Ayubu 16 >
Then Job answered and said,
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
I have heard many such things: miserable comforters are ye all.
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Shall vain words have an end? or what provoketh thee that thou answerest?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also could speak as ye do; if your soul were in my soul’s stead, I could join words together against you, and shake mine head at you.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
[But] I would strengthen you with my mouth, and the solace of my lips should assuage [your grief].
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
Though I speak, my grief is not assuaged: and though I forbear, what am I eased?
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
But now he hath made me weary: thou hast made desolate all my company.
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
And thou hast laid fast hold on me, [which] is a witness [against me]: and my leanness riseth up against me, it testifieth to my face.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
He hath torn me in his wrath, and persecuted me; he hath gnashed upon me with his teeth: mine adversary sharpeneth his eyes upon me.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
They have gaped upon me with their mouth; they have smitten me upon the cheek reproachfully: they gather themselves together against me.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
God delivereth me to the ungodly, and casteth me into the hands of the wicked.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
I was at ease, and he brake me asunder; yea, he hath taken me by the neck, and dashed me to pieces: he hath also set me up for his mark.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
His archers compass me round about, he cleaveth my reins asunder, and doth not spare; he poureth out my gall upon the ground.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He breaketh me with breach upon breach; he runneth upon me like a giant.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
I have sewed sackcloth upon my skin, and have laid my horn in the dust.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face is foul with weeping, and on my eyelids is the shadow of death;
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
Although there is no violence in mine hands, and my prayer is pure.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
O earth, cover not thou my blood, and let my cry have no [resting] place.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Even now, behold, my witness is in heaven, and he that coucheth for me is on high.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
My friends scorn me: [but] mine eye poureth out tears unto God;
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
That he would maintain the right of a man with God, and of a son of man with his neighbour!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
For when a few years are come, I shall go the way whence I shall not return.