< Ayubu 16 >
But Job answered and said:
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
Of such things as these I have heard enough! Miserable comforters are ye all!
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Will there ever be an end to words of wind? What stirreth thee up, that thou answerest?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also might speak like you, If ye were now in my place; I might string together words against you, And shake my head at you.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
I would strengthen you with my mouth, And the consolation of my lips should sustain you.
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
If I speak, my grief is not assuaged; And if I forbear, it doth not leave me.
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
For now He hath quite exhausted me; Thou hast desolated all my house!
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
Thou hast seized hold of me, and this is a witness against me; My leanness riseth up and testifieth against me to my face.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
His anger teareth my flesh, and pursueth me; He gnasheth upon me with his teeth; My adversary sharpeneth his eyes upon me.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
They gape for me with their mouths; In scorn they smite me on the cheek; With one consent they assemble against me.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
God hath given me a prey to the unrighteous, And delivered me into the hands of the wicked.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
I was at ease, but he hath crushed me; He hath seized me by the neck, and dashed me in pieces; He hath set me up for his mark.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
His archers encompass me around; He pierceth my reins, and doth not spare; He poureth out my gall upon the ground.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He breaketh me with breach upon breach; He rusheth upon me like a warrior.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
I have sewed sackcloth upon my skin, And thrust my horn into the dust.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face is red with weeping, And upon my eyelids is deathlike darkness.
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
Yet is there no injustice in my bands. And my prayer hath been pure.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
O earth! cover not thou my blood, And let there be no hiding-place for my cry!
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Yet even now, behold, my witness is in heaven, And he who knoweth me is on high.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
My friends have me in derision, But my eye poureth out tears unto God.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
O that one might contend for a man with God, As a man contendeth with his neighbor!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
For when a few years shall have passed, I shall go the way whence I shall not return.