< Ayubu 16 >
Then Job answered, and said:
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
I have often heard such things as these: you are all troublesome comforters.
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Shall windy words have no end? or is it any trouble to thee to speak?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also could speak like you: and would God your soul were for my soul. I would comfort you also with words, and would wag my head over you.
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
I would strengthen you with my mouth, and would move my lips, as sparing you.
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
But what shall I do? If I speak, my pain will not rest: and if I hold my peace, it will not depart from me.
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
But now my sorrow hath oppressed me, and all my limbs are brought to nothing.
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
My wrinkles bear witness against me, and a false speaker riseth up against my face, contradicting me.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
He hath gathered together his fury against me, and threatening me he hath gnashed with his teeth upon me: my enemy hath beheld me with terrible eyes.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
They have opened their mouths upon me, and reproaching me they have struck me on the cheek, they are filled with my pains.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
God hath shut me up with the unjust man, and hath delivered me into the hands of the wicked.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
I that was formerly so wealthy, am all on a sudden broken to pieces: he hath taken me by my neck, he hath broken me, and hath set me up to be his mark.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
He hath compassed me round about with his lances, he hath wounded my loins, he hath not spared, and hath poured out my bowels on the earth.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He hath torn me with wound upon wound, he hath rushed in upon me like a giant.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
I have sowed sackcloth upon my skin, and have covered my flesh with ashes.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face is swollen with weeping, and my eyelids are dim.
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
These things have I suffered without the iniquity of my hand, when I offered pure prayers to God.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
O earth, cover not thou my blood, neither let my cry find a hiding place in thee.
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
For behold my witness is in heaven, and he that knoweth my conscience is on high.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
My friends are full of words: my eye poureth out tears to God.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
And O that a man might so be judged with God, as the son of man is judged with his companion!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
For behold short years pass away and I am walking in a path by which I shall not return.