< Ayubu 16 >
And Job answered and said,
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
I have heard many such things: grievous comforters are ye all.
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
Shall words of wind have an end? or what provoketh thee that thou answerest?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
I also could speak as ye: if your soul were in my soul's stead, I could join together words against you, and shake my head at you;
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
[But] I would encourage you with my mouth, and the solace of my lips should assuage [your pain].
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
If I speak, my pain is not assuaged; and if I forbear, what am I eased?
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
But now he hath made me weary; ...thou hast made desolate all my family;
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
Thou hast shrivelled me up! it is become a witness; and my leanness riseth up against me, it beareth witness to my face.
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
His anger teareth and pursueth me; he gnasheth with his teeth against me; [as] mine adversary he sharpeneth his eyes at me.
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
They gape upon me with their mouth; they smite my cheeks reproachfully; they range themselves together against me.
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
God hath delivered me over to the iniquitous man, and hurled me into the hands of the wicked.
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
I was at rest, but he hath shattered me; he hath taken me by the neck and shaken me to pieces, and set me up for his mark.
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
His arrows encompass me round about, he cleaveth my reins asunder and doth not spare; he poureth out my gall upon the ground.
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
He breaketh me with breach upon breach; he runneth upon me like a mighty man.
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
I have sewed sackcloth upon my skin, and rolled my horn in the dust.
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
My face is red with weeping, and on my eyelids is the shadow of death;
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
Although there is no violence in my hands, and my prayer is pure.
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
O earth, cover not my blood, and let there be no place for my cry!
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
Even now, behold, my Witness is in the heavens, and he that voucheth for me is in the heights.
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
My friends are my mockers; mine eye poureth out tears unto God.
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
Oh that there were arbitration for a man with God, as a son of man for his friend!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
For years [few] in number shall pass, — and I shall go the way [whence] I shall not return.