< Ayubu 16 >
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
這樣的話我聽了許多; 你們安慰人,反叫人愁煩。
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
虛空的言語有窮盡嗎? 有甚麼話惹動你回答呢?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
我也能說你們那樣的話; 你們若處在我的境遇, 我也會聯絡言語攻擊你們, 又能向你們搖頭。
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
但我必用口堅固你們, 用嘴消解你們的憂愁。
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
我雖說話,憂愁仍不得消解; 我雖停住不說,憂愁就離開我嗎?
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
但現在上帝使我困倦, 使親友遠離我,
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
又抓住我,作見證攻擊我; 我身體的枯瘦也當面見證我的不是。
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
主發怒撕裂我,逼迫我, 向我切齒; 我的敵人怒目看我。
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
他們向我開口, 打我的臉羞辱我, 聚會攻擊我。
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
上帝把我交給不敬虔的人, 把我扔到惡人的手中。
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
我素來安逸,他折斷我, 掐住我的頸項,把我摔碎, 又立我為他的箭靶子。
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
他的弓箭手四面圍繞我; 他破裂我的肺腑,並不留情, 把我的膽傾倒在地上,
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
將我破裂又破裂, 如同勇士向我直闖。
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
我縫麻布在我皮膚上, 把我的角放在塵土中。
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
我的臉因哭泣發紫, 在我的眼皮上有死蔭。
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
我的手中卻無強暴; 我的祈禱也是清潔。
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
地啊,不要遮蓋我的血! 不要阻擋我的哀求!
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
現今,在天有我的見證, 在上有我的中保。
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
我的朋友譏誚我, 我卻向上帝眼淚汪汪。
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
願人得與上帝辯白, 如同人與朋友辯白一樣;
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
因為再過幾年, 我必走那往而不返之路。