< Ayubu 16 >

1 Kisha Ayubu akajibu:
約伯回答說:
2 “Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
像這樣的話,我聽了許多;你們的安慰反使人煩惱。
3 Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
這些風涼話何時了﹖或者有什麼事迫你非說不可﹖
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
若是你們處在我的境遇中,我也會說像你們所說的話,也會花言巧語譏笑你們,向你們搖頭。
5 Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
我也會以口舌寬慰你們,搖唇鼓舌來減輕你們的痛苦。
6 “Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
我若講話,痛苦並不停止;我若閉口不言,難道痛苦就離開我﹖
7 Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
現今天主的確叫我厭倦,使我每個親人都遠離了我;
8 Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
使我憔悴,以指證我;使我消瘦,當面非難我。
9 Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
他在憤怒中撕裂我,窘迫我,向我咬牙切齒;我仇人鋒利的眼睛常盯著我。
10 Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
他們張開大口想吞噬我,責罵著打我的面頰,一起擁上前來攻擊我。
11 Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
天主將我交於不義之人,將我丟在惡人手中。
12 Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
我原來安寧,他卻折磨我,抓住我的脖子,粉碎我,又拿我當作他的箭靶。
13 wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
他的箭矢四面射擊我,射穿我的腰,毫不留情,使我的膽傾流於地。
14 Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
他將我撕裂粉碎,有如武士向我跑來。
15 “Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
我縫麻衣包裹我的皮膚,使我額角插入塵土。
16 Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
我的臉因哭泣發紅,我睫眉間滿是暗影;
17 Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
我的手雖沒有行過殘暴的事,而我的祈禱,又往往純正。
18 “Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
地啊! 不要掩蓋我的血。願我的呼聲無休息的餘地!
19 Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
看啊! 連現今在天上有我的見證,在高處有我的中保。
20 Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
我的哀號上徹於天,在天主前我的雙目流淚不止。
21 kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
惟願人與天主之間有一中人,猶如人與人之間一樣!
22 “Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.
因為我的年數將盡,快要走上那條一去不返的路途。

< Ayubu 16 >