< Ayubu 11 >

1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
そこでナアマびとゾパルは答えて言った、
2 “Je, maneno haya yote yapite bila kujibiwa? Je, huyu mnenaji athibitishwe kuwa na haki?
「言葉が多ければ、答なしにすまされるだろうか。口の達者な人は義とされるだろうか。
3 Je, maneno yako ya upuzi yawafanye watu wanyamaze kimya? Je, mtu asikukemee unapofanya dhihaka?
あなたのむなしい言葉は人を沈黙させるだろうか。あなたがあざけるとき、人はあなたを恥じさせないだろうか。
4 Unamwambia Mungu, ‘Imani yangu ni kamili nami ni safi mbele zako.’
あなたは言う、『わたしの教は正しい、わたしは神の目に潔い』と。
5 Aha! Laiti kwamba Mungu angesema, kwamba angefungua midomo yake dhidi yako,
どうぞ神が言葉を出し、あなたにむかってくちびるを開き、
6 naye akufunulie siri za hekima, kwa kuwa hekima ya kweli ina pande mbili. Ujue hili: Mungu amesahau hata baadhi ya dhambi zako.
知恵の秘密をあなたに示されるように。神はさまざまの知識をもたれるからである。それであなたは知るがよい、神はあなたの罪よりも軽くあなたを罰せられることを。
7 “Je, waweza kujua siri za Mungu? Je, waweza kuyachunguza mambo yote kumhusu Mwenyezi?
あなたは神の深い事を窮めることができるか。全能者の限界を窮めることができるか。
8 Ni juu mno kuliko mbingu: waweza kufanya nini? Kina chake ni kirefu kuliko kuzimu: wewe waweza kujua nini? (Sheol h7585)
それは天よりも高い、あなたは何をなしうるか。それは陰府よりも深い、あなたは何を知りうるか。 (Sheol h7585)
9 Kipimo chake ni kirefu kuliko dunia, nacho ni kipana kuliko bahari.
その量は地よりも長く、海よりも広い。
10 “Kama akija na kukufunga gerezani, na kuitisha mahakama, ni nani awezaye kumpinga?
彼がもし行きめぐって人を捕え、さばきに召し集められるとき、だれが彼をはばむことができよう。
11 Hakika anawatambua watu wadanganyifu; naye aonapo uovu, je, haangalii?
彼は卑しい人間を知っておられるからだ。彼は不義を見る時、これに心をとめられぬであろうか。
12 Mpumbavu aweza kuwa mwenye hekima, endapo mtoto wa punda-mwitu atazaliwa mwanadamu.
しかし野ろばの子が人として生れるとき、愚かな者も悟りを得るであろう。
13 “Hata sasa ukiutoa moyo wako kwake na kumwinulia mikono yako,
もしあなたが心を正しくするならば、神に向かって手を伸べるであろう。
14 ukiiondolea mbali ile dhambi iliyo mkononi mwako wala usiuruhusu uovu ukae hemani mwako,
もしあなたの手に不義があるなら、それを遠く去れ、あなたの天幕に悪を住まわせてはならない。
15 ndipo utainua uso wako bila aibu; utasimama imara bila hofu.
そうすれば、あなたは恥じることなく顔をあげることができ、堅く立って、恐れることはない。
16 Hakika utaisahau taabu yako, utaikumbuka tu kama maji yaliyokwisha kupita.
あなたは苦しみを忘れ、あなたのこれを覚えることは、流れ去った水のようになる。
17 Maisha yako yatangʼaa kuliko adhuhuri, nalo giza litakuwa kama alfajiri.
そしてあなたの命は真昼よりも光り輝き、たとい暗くても朝のようになる。
18 Utakuwa salama, kwa kuwa lipo tumaini; utatazama pande zote na kupumzika kwa salama.
あなたは望みがあるゆえに安んじ、保護されて安らかにいこうことができる。
19 Utalala, wala hakuna atakayekuogofya, naam, wengi watajipendekeza kwako.
あなたは伏してやすみ、あなたを恐れさせるものはない。多くの者はあなたの好意を求めるであろう。
20 Bali macho ya waovu hayataona, wokovu utawaepuka; tarajio lao litakuwa ni hangaiko la mtu anayekata roho.”
しかし悪しき者の目は衰える。彼らは逃げ場を失い、その望みは息の絶えるにひとしい」。

< Ayubu 11 >