< Yeremia 8 >

1 “‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao.
in/on/with time [the] he/she/it utterance LORD (to come out: send *Q(K)*) [obj] bone king Judah and [obj] bone ruler his and [obj] bone [the] priest and [obj] bone [the] prophet and [obj] bone to dwell Jerusalem from grave their
2 Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi.
and to spread them to/for sun and to/for moon and to/for all army [the] heaven which to love: lover them and which to serve: minister them and which to go: follow after them and which to seek them and which to bow to/for them not to gather and not to bury to/for dung upon face: surface [the] land: soil to be
3 Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
and to choose death from life to/for all [the] remnant [the] to remain from [the] family [the] bad: evil [the] this in/on/with all [the] place [the] to remain which to banish them there utterance LORD Hosts
4 “Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “‘Je, watu wanapoanguka hawainuki? Je, mtu anapopotea harudi?
and to say to(wards) them thus to say LORD to fall: fall and not to arise: rise if to return: turn back and not to return: return
5 Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanangʼangʼania udanganyifu na wanakataa kurudi.
why? to return: turn back [the] people [the] this Jerusalem faithlessness to conduct to strengthen: hold in/on/with deceitfulness to refuse to/for to return: return
6 Nimewasikiliza kwa makini, lakini hawataki kusema lililo sawa. Hakuna anayetubia makosa yake akisema, “Nimefanya nini?” Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe kama farasi anayekwenda vitani.
to listen and to hear: hear not right to speak: speak nothing man: anyone to be sorry: relent upon distress: evil his to/for to say what? to make: do all his to return: turn back (in/on/with running their *Q(K)*) like/as horse to overflow in/on/with battle
7 Hata korongo aliyeko angani anayajua majira yake yaliyoamriwa, nao njiwa, mbayuwayu na koikoi hufuata majira yao ya kurudi. Lakini watu wangu hawajui Bwana anachotaka kwao.
also stork in/on/with heaven to know meeting: time appointed her and turtledove (and swallow *Q(K)*) and crane to keep: obey [obj] time to come (in): come they and people my not to know [obj] justice: judgement LORD
8 “‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,” wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi imeandika kwa udanganyifu?
how? to say wise we and instruction LORD with us surely behold to/for deception to make stylus deception secretary
9 Wenye hekima wataaibika, watafadhaika na kunaswa. Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana, hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?
be ashamed wise to to be dismayed and to capture behold in/on/with word LORD to reject and wisdom what? to/for them
10 Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao, na mashamba yao kwa wamiliki wengine. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
to/for so to give: give [obj] woman: wife their to/for another land: country their to/for to possess: take for from small and till great: large all his to cut off: to gain unjust-gain from prophet and till priest all his to make: do deception
11 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, “Amani, amani,” wakati hakuna amani.
and to heal [obj] breaking daughter people my upon to lighten to/for to say peace peace and nothing peace
12 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo, hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini watakapoadhibiwa, asema Bwana.
be ashamed for abomination to make also be ashamed not be ashamed and be humiliated not to know to/for so to fall: kill in/on/with to fall: kill in/on/with time punishment their to stumble to say LORD
13 “‘Nitayaondoa mavuno yao, asema Bwana. Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu. Hapatakuwepo na tini kwenye mtini, majani yake yatanyauka. Kile nilichowapa watanyangʼanywa.’”
to gather to cease them utterance LORD nothing grape in/on/with vine and nothing fig in/on/with fig and [the] leaf to wither and to give: give to/for them to pass them
14 “Kwa nini tunaketi hapa? Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie kwenye miji yenye maboma, tukaangamie huko! Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu ametuhukumu kuangamia, na kutupa maji yenye sumu tunywe, kwa sababu tumemtenda dhambi.
upon what? we to dwell to gather and to come (in): come to(wards) city [the] fortification and to silence: destroyed there for LORD God our to silence: destroyed us and to water: drink us water poison for to sin to/for LORD
15 Tulitegemea amani, lakini hakuna jema lililokuja, tulitegemea wakati wa kupona, lakini kulikuwa hofu tu.
to await to/for peace and nothing good to/for time healing and behold terror
16 Mkoromo wa farasi za adui umesikika kuanzia Dani, kwa mlio wa madume yao ya farasi, nchi yote inatetemeka. Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo, mji na wote waishio ndani yake.”
from Dan to hear: hear snorting horse his from voice: sound neighing mighty: stallion his to shake all [the] land: country/planet and to come (in): come and to eat land: country/planet and fullness her city and to dwell in/on/with her
17 “Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu, fira ambao hawawezi kulogwa, nao watawauma,” asema Bwana.
for look! I to send: depart in/on/with you serpent serpent which nothing to/for them charm and to bite [obj] you utterance LORD
18 Ee Mfariji wangu katika huzuni, moyo wangu umezimia ndani yangu.
cheer my upon sorrow upon me heart my faint
19 Sikia kilio cha watu wangu kutoka nchi ya mbali: “Je, Bwana hayuko Sayuni? Je, Mfalme wake hayuko tena huko?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao, kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”
behold voice cry daughter people my from land: country/planet distance LORD nothing in/on/with Zion if: surely yes king her nothing in/on/with her why? to provoke me in/on/with idol their in/on/with vanity foreign
20 “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha, nasi hatujaokolewa.”
to pass harvest to end: finish summer and we not to save
21 Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia; ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.
upon breaking daughter people my to break be dark horror: appalled to strengthen: hold me
22 Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi? Je, hakuna tabibu huko? Kwa nini basi hakuna uponyaji wa majeraha ya watu wangu?
balsam nothing in/on/with Gilead if: surely yes to heal nothing there for why? not to ascend: establish health daughter people my

< Yeremia 8 >