< Isaya 36 >

1 Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
And it was don in the fourtenthe yeer of kyng Ezechie, Sennacherib, the kyng of Assiriens, stiede on alle the stronge citees of Juda, and took tho.
2 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wa jeshi pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Jemadari wa jeshi akasimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
And the kyng of Assiriens sente Rapsases fro Lachis to Jerusalem, to kyng Ezechie, with greet power; and he stood at the watir cundit of the hiyere sisterne, in the weie of the feeld of a fullere.
3 Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakamwendea.
And Eliachym, the sone of Elchie, that was on the hous, yede out to hym, and Sobna, the scryuen, and Joae, the sone of Asaph, the chaunceler.
4 Jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia, “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
And Rapsases seide to hem, Seie ye to Ezechie, The greet king, the king of Assiriens, seith these thingis, What is the trist, in which thou tristist?
5 Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
ethir bi what councele ether strengthe disposist thou for to rebelle? on whom hast thou trist, for thou hast go awei fro me?
6 Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
Lo! thou tristist on this brokun staf of rehed, on Egipt, on which if a man restith, it schal entre in to his hoond, and schal perse it; so doith Farao, the kyng of Egipt, to alle men that tristen in hym.
7 Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya”?
That if thou answerist to me, We tristen in oure Lord God; whether it is not he, whose hiye places and auteris Esechie dide awei, and he seide to Juda and to Jerusalem, Ye schulen worschipe bifore this auter?
8 “‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
And now bitake thee to my lord, the kyng of Assiriens, and Y schal yyue to thee twei thousynde of horsis, and thou maist not yyue of thee stieris of tho horsis.
9 Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
And hou schalt thou abide the face of the iuge of o place of the lesse seruauntis of my lord? That if thou tristist in Egipt, and in cartis, and in knyytis;
10 Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza nchi hii bila Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
and now whethir Y stiede to this lond with out the Lord, that Y schulde distrie it? The Lord seide to me, Stie thou on this lond, and distrie thou it.
11 Ndipo Eliakimu, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
And Eliachym, and Sobna, and Joae, seiden to Rapsaces, Speke thou to thi seruauntis bi the langage of Sirie, for we vndurstonden; speke thou not to vs bi the langage of Jewis in the eeris of the puple, which is on the wal.
12 Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
And Rapsaces seide to hem, Whether mi lord sente me to thi lord, and to thee, that Y schulde speke alle these wordis, and not rathere to the men that sitten on the wal, that thei ete her toordis, and drynke the pisse of her feet with you?
13 Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni maneno ya mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
And Rapsaces stood, and criede with greet vois in the langage of Jewis, and seide, Here ye the wordis of the greet kyng, the kyng of Assiriens.
14 Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa!
The kyng seith these thingis, Esechie disseyue not you, for he may not delyuere you;
15 Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
and Ezechie yyue not to you trist on the Lord, and seie, The Lord delyuerynge schal delyuere vs; this citee schal not be youun in to the hoond of the kyng of Assiriens.
16 “Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
Nyle ye here Ezechie. For whi the kyng of Assiriens seith these thingis, Make ye blessyng with me, and go ye out to me; and ete ye ech man his vyner, and ech man his fige tre, and drynke ye ech man the water of his cisterne,
17 mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na ya mashamba ya mizabibu.
til Y come, and take awei you to a lond which is as youre lond; to a lond of whete and of wyn, to a lond of looues and of vyneris.
18 “Msikubali Hezekia awapotoshe asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’ Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
Ezechie disturble not you, and seie, The Lord schal delyuere vs. Whether the goddis of folkis delyuereden ech his lond fro the hond of the kyng of Assiriens?
19 Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
Where is the god of Emath, and of Arphat? Where is the god of Sepharuaym? Whethir thei delyueriden Samarie fro myn hond?
20 Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
Who is of alle goddis of these londis, that delyueride his lond fro myn hond, that the Lord delyuere Jerusalem fro myn hond?
21 Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
And thei weren stille, and answeriden not to hym a word. For whi the kyng comaundide to hem, and seide, Answere ye not to him.
22 Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.
And Eliachym, the sone of Elchie, that was on the hous, and Sobna, the scryueyn, and Joae, the sone of Asaph, chaunceler, entriden with to-rent clothis to Ezechie, and telde to hym the wordis of Rapsaces.

< Isaya 36 >