< Isaya 29 >

1 Ole wako, wewe Arieli, Arieli, mji alimokaa Daudi! Ongezeni mwaka kwa mwaka, na mzunguko wa sikukuu zenu uendelee.
Wo! Ariel, Ariel, the citee which Dauid ouercam; yeer is addid to yeer, solempnytees ben passyd.
2 Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.
And Y schal cumpasse Ariel, and it schal be soreuful and morenynge; and Jerusalem schal be to me as Ariel.
3 Nitapiga kambi pande zote dhidi yako, nitakuzunguka kwa minara na kupanga mazingirwa yangu dhidi yako.
And Y schal cumpasse as a round trendil in thi cumpasse, and Y schal caste erthe ayens thee, and Y schal sette engynes in to thi bisegyng.
4 Utakaposhushwa, utanena kutoka ardhini, utamumunya maneno yako kutoka mavumbini. Sauti yako itatoka katika nchi kama vile ya mzimu, utanongʼona maneno yako toka mavumbini.
Thou schalt be maad low, thou schalt speke of erthe, and thi speche schal be herd fro the erthe; and thi vois schal be as the vois of a deed man reisid bi coniuring, and thi speche schal ofte grutche of the erthe.
5 Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,
And the multitude of hem that wyndewen thee, schal be as thynne dust; and the multitude of hem that hadden the maistrie ayens thee, schal be as a deed sparcle passynge.
6 Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuja na ngurumo, tetemeko la ardhi, na kwa sauti kuu, atakuja na dhoruba, tufani na miali ya moto iteketezayo.
And it schal be sudenli, anoon it schal be visitid of the Lord of oostis, in thundur, and in mouyng of the erthe, and in greet vois of whirlwynd, and of tempest, and of flawme of fier deuowrynge.
7 Kisha makundi ya mataifa yote yale yapiganayo dhidi ya Arieli, yale yanayomshambulia yeye na ngome zake, na kumzunguka kwa jeshi, watakuwa kama ilivyo ndoto, kama maono wakati wa usiku:
And the multitude of alle folkis that fouyten ayens Ariel schal be as the dreem of a nyytis visioun; and alle men that fouyten, and bisegiden, and hadden the maistrie ayens it.
8 kama vile mtu aliye na njaa aotavyo kuwa anakula, lakini huamka, bado njaa yake ingalipo, kama vile mtu mwenye kiu aotavyo kuwa anakunywa maji, lakini huamka akiwa anazimia, akiwa bado angali ana kiu. Hivyo ndivyo itakavyokuwa kwa makundi yote ya mataifa yanayopigana dhidi ya Mlima Sayuni.
And as an hungry man dremyth, and etith, but whanne he is awakid, his soule is voide; and as a thirsti man dremeth, and drynkith, and after that he is awakid, he is weri, and thirstith yit, and his soule is voide, so schal be the multitude of alle folkis, that fouyten ayens the hil of Sion.
9 Duwaeni na kushangaa, jifanyeni vipofu wenyewe na msione, leweni, lakini si kwa mvinyo, pepesukeni lakini si kwa kileo.
Be ye astonyed, and wondre; wake ye, and douyte ye; be ye drunken, and not of wyn; be ye moued, and not with drunkenesse.
10 Bwana amewaleteeni usingizi mzito: Ameziba macho yenu (ninyi manabii); amefunika vichwa vyenu (ninyi waonaji).
For the Lord hath meddlid to you the spirit of sleep; he schal close youre iyen, and schal hile youre profetis, and princes that sien visiouns.
11 Kwa maana kwenu ninyi, maono haya yote si kitu ila maneno yaliyotiwa lakiri katika kitabu. Kama mkimpa mtu yeyote awezaye kusoma kitabu hiki, nanyi mkamwambia, “Tafadhali kisome,” yeye atajibu, “Mimi siwezi, kwa kuwa kimetiwa lakiri.”
And the visioun of alle profetis schal be to you as the wordis of a book aseelid; which whanne thei schulen yyue to hym that kan lettris, thei schulen seie, Rede thou this book; and he schal answere, Y may not, for it is aseelid.
12 Au kama mkimpa mtu yeyote kitabu hiki asiyeweza kusoma na kumwambia, “Tafadhali kisome,” atajibu, “Mimi sijui kusoma.”
And the book schal be youun to him that kan not lettris, and it schal be seid to hym, Rede thou; and he schal answere, Y kan no lettris.
13 Bwana anasema: “Watu hawa hunikaribia kwa vinywa vyao na kuniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. Ibada yao kwangu inatokana na maagizo waliyofundishwa na wanadamu.
And the Lord seide, For that this puple neiyeth with her mouth, and glorifieth me with her lippis, but her herte is fer fro me; and thei dredden me for the comaundement and techyngis of men, therfor lo!
14 Kwa hiyo mara nyingine tena nitawashangaza watu hawa, kwa ajabu juu ya ajabu. Hekima ya wenye hekima itapotea, nayo akili ya wenye akili itatoweka.”
Y schal adde, that Y make wondryng to this puple, in a greet myracle and wondurful; for whi wisdom schal perische fro wise men therof, and the vndurstondyng of prudent men therof schal be hid.
15 Ole kwa wale wanaokwenda kwenye vilindi virefu kumficha Bwana mipango yao, wafanyao kazi zao gizani na kufikiri, “Ni nani anayetuona? Ni nani atakayejua?”
Wo to you that ben hiye of herte, that ye hide counsel fro the Lord; the werkis of whiche ben in derknessis, and thei seien, Who seeth vs, and who knowith vs?
16 Mnapindua mambo juu chini, kana kwamba mfinyanzi aweza kufikiriwa kuwa kama udongo wa mfinyanzi! Je, kile kilichofinyangwa chaweza kumwambia yule aliyekifinyanga, “Wewe hukunifinyanga mimi?” Je, chungu kinaweza kumwambia mfinyanzi, “Wewe hujui chochote?”
This thouyt of you is weiward, as if cley thenke ayens a pottere, and the werk seie to his makere, Thou madist not me; and a thing `that is maad, seie to his makere, Thou vndurstondist not.
17 Kwa muda mfupi sana, je, Lebanoni haitageuzwa kuwa shamba lenye rutuba, na shamba lenye rutuba liwe kama msitu?
Whether not yit in a litil time and schort the Liban schal be turned in to Chermel, and Chermel schal be arettid in to the forest?
18 Katika siku ile viziwi watasikia maneno ya kitabu, na katika utusitusi na giza macho ya kipofu yataona.
And in that dai deef men schulen here the wordis of the book, and the iyen of blynde men schulen se fro derknessis and myisty;
19 Mara nyingine tena wanyenyekevu watafurahi katika Bwana, wahitaji watafurahi katika yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
and mylde men schulen encreesse gladnesse in the Lord, and pore men schulen make ful out ioie in the hooli of Israel.
20 Wakatili watatoweka na wenye kudhihaki watatokomea, nao wote wenye jicho la uovu watakatiliwa mbali,
For he that hadde the maistrie, failide, and the scornere is endid, and alle thei ben kit doun that walkiden on wickidnesse;
21 wale ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mwenye hatia, wamtegeao mtego mtetezi katika mahakama, na kwa ushuhuda wa uongo humnyima haki yeye asiye na hatia.
whiche maden men to do synne in word, and disseyueden a repreuere in the yate, and bowiden awey in veyn fro a iust man.
22 Kwa hiyo hili ndilo Bwana, aliyemkomboa Abrahamu, analosema kwa nyumba ya Yakobo: “Yakobo hataaibishwa tena, wala nyuso zao hazitabadilika sura tena.
For this thing the Lord, that ayen bouyte Abraham, seith these thingis to the hous of Jacob, Jacob schal not be confoundid now, nether now his cheer schal be aschamed; but whanne he schal se hise sones,
23 Wakati watakapoona watoto wao miongoni mwao, kazi ya mikono yangu, watalitakasa Jina langu takatifu; wataukubali utakatifu wa yeye Aliye Mtakatifu wa Yakobo, nao watamcha Mungu wa Israeli.
the werkis of myn hondis, halewynge my name in the myddis of hym. And thei schulen halewe the hooli of Jacob, and thei schulen preche God of Israel;
24 Wale wanaopotoka rohoni watapata ufahamu, nao wale wanaolalamika watayakubali mafundisho.”
and thei that erren in spirit, schulen knowe vndurstondyng, and idil men schulen lerne the lawe.

< Isaya 29 >