< Mwanzo 29 >

1 Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki.
Jacob reprit sa marche et s'en alla au pays des fils de l'Orient.
2 Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa mdomoni mwa kisima lilikuwa kubwa.
Il regarda, et voici, il y avait un puits dans la campagne, et voici, il y avait à côté trois troupeaux de brebis qui étaient couchés, car c'était à ce puits qu'on abreuvait les troupeaux, et la pierre qui était sur l'ouverture du puits était grande.
3 Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, wachungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima.
Là se réunissaient tous les troupeaux; on roulait la pierre de dessus l'ouverture du puits, on faisait boire les troupeaux, et l'on remettait la pierre à sa place sur l'ouverture du puits.
4 Yakobo aliwauliza wachungaji, “Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka Harani.”
Jacob dit aux bergers: " Mes frères, d'où êtes-vous? " ils répondirent: " Nous sommes de Haran. "
5 Aliwaambia, “Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori?” Wakamjibu, “Ndiyo, tunamfahamu.”
Il leur dit: " Connaissez-vous Laban, fils de Nachor? " Ils répondirent: " Nous le connaissons. "
6 Kisha Yakobo akawauliza, “Je, yeye ni mzima?” Wakasema, “Ndiyo, ni mzima, na hapa yuaja Raheli binti yake akiwa na kondoo.”
Il leur dit: " Est-il en bonne santé? " Ils répondirent: " Il est en bonne santé, et voici Rachel, sa fille, qui vient avec les brebis. "
7 Akasema, “Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya mifugo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.”
Il dit: " Voici, il est encore grand jour, et ce n'est pas le moment de rassembler les troupeaux; abreuvez les brebis et retournez les faire paître. "
8 Walijibu, “Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.”
Ils répondirent: " Nous ne le pouvons pas jusqu'à ce que tous les troupeaux soient rassemblés et qu'on roule la pierre de dessus l'ouverture du puits; alors nous abreuverons les brebis. "
9 Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo.
Il s'entretenait encore avec eux, lorsque Rachel arriva avec les brebis de son père; car elle était bergère.
10 Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake.
Dès que Jacob vit Rachel, fille de Laban, frère de sa mère, et les brebis de Laban, frère de sa mère, il s'approcha, roula la pierre de dessus l'ouverture du puits, et abreuva les brebis de Laban, frère de sa mère.
11 Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti.
Et Jacob baisa Rachel, et il éleva la voix et pleura.
12 Yakobo alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake, na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake.
Jacob apprit à Rachel qu'il était frère de son père, qu'il était fils de Rebecca; et elle courut l'annoncer à son père.
13 Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu, halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote.
Quand Laban eut entendu parler de Jacob, fils de sa sœur, il courut au-devant de lui, et l'ayant pris dans ses bras, il lui donna des baisers et l'amena dans sa maison. Jacob raconta à Laban toutes ces choses,
14 Ndipo Labani akamwambia, “Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.” Baada ya Yakobo kukaa kwa Labani mwezi mzima,
et Laban lui dit: " Oui, tu es mes os et ma chair. " Et Jacob demeura avec lui un mois entier.
15 Labani akamwambia, “Kwa vile wewe ni jamaa yangu, ndiyo sababu unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.”
Alors Laban dit à Jacob: " Est-ce que, parce que tu es mon frère, tu me serviras pour rien? Dis-moi quel sera ton salaire. "
16 Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli.
Or Laban avait deux filles; l'aînée se nommait Lia, et la cadette Rachel.
17 Lea alikuwa na macho dhaifu, lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura.
Lia avait les yeux malades; mais Rachel était belle de taille et belle de visage.
18 Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, “Nitakutumikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.”
Comme Jacob aimait Rachel, il dit: " Je te servirai sept ans pour Rachel, ta fille cadette. "
19 Labani akasema, “Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.”
Et Laban dit: " Mieux vaut te la donner que la donner à un autre; reste avec moi. "
20 Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli.
Et Jacob servit pour Rachel sept années, et elles furent à ses yeux comme quelques jours, parce qu'il l'aimait.
21 Ndipo Yakobo akamwambia Labani, “Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.”
Jacob dit à Laban: " Donne-moi ma femme, car mon temps est accompli, et j'irai vers elle. "
22 Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu.
Laban réunit tous les gens du lieu et fit un festin;
23 Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili.
et le soir, prenant Lia, sa fille, il l'amena à Jacob, qui alla vers elle.
24 Naye Labani akamtoa Zilpa, mtumishi wake wa kike, kuwa mtumishi wa Lea, binti yake.
Et Laban donna sa servante Zelpha pour servante à Lia, sa fille.
25 Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, “Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, sivyo? Kwa nini umenidanganya?”
Le matin venu, voilà que c'était Lia. Et Jacob dit à Laban: " Que m'as-tu fait? N'est-ce pas pour Rachel que j'ai servi chez toi? Pourquoi m'as-tu trompé? "
26 Labani akajibu, “Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa.
Laban répondit: " Ce n'est point l'usage dans notre pays de donner la cadette avant l'aînée.
27 Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.”
Achève la semaine de celle-ci, et nous te donnerons aussi l'autre pour le service que tu feras encore chez moi pendant sept autres années. "
28 Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake.
Jacob fit ainsi, et il acheva la semaine de Lia; puis Laban lui donna pour femme Rachel, sa fille.
29 Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake.
Et Laban donna sa servante Bala pour servante à Rachel, sa fille.
30 Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.
Jacob alla aussi vers Rachel et il l'aima aussi plus que Lia; il servit encore chez Laban sept autres années.
31 Bwana alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa.
Yahweh vit que Lia était haïe, et il la rendit féconde, tandis que Rachel était stérile.
32 Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, “Ni kwa sababu Bwana ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.”
Lia conçut et enfanta un fils, et elle le nomma Ruben, car elle dit: " Yahweh a regardé mon affliction; maintenant mon mari m'aimera. "
33 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Kwa sababu Bwana alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.” Kwa hiyo akamwita Simeoni.
Elle conçut encore et enfanta un fils, et elle dit: " Yahweh a entendu que j'étais haïe, et il m'a encore donné celui-là ". Et elle le nomma Siméon.
34 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.” Kwa hiyo akamwita Lawi.
Elle conçut encore et enfanta un fils, et elle dit: " Cette fois mon mari s'attachera à moi car je lui ai enfanté trois fils. " C'est pourquoi on le nomma Lévi.
35 Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, “Wakati huu nitamsifu Bwana.” Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.
Elle conçut encore et enfanta un fils, et elle dit: " Cette fois je louerai Yahweh. " C'est pourquoi elle le nomma Juda. Et elle cessa d'avoir des enfants.

< Mwanzo 29 >