< Mwanzo 41 >

1 Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
Deux ans s'étant écoulés, Pharaon eut un songe. Voici, il se tenait près du fleuve,
2 wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
et voici que du fleuve montaient sept vaches belles à voir et grasses de chair, et elles se mirent à paître dans la verdure.
3 Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
Et voici qu'après elles montaient du fleuve sept autres vaches, laides à voir et maigres de chair, et elles vinrent se mettre à côté des vaches qui étaient sur le bord du fleuve.
4 Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
Et les vaches laides à voir et maigres de chair dévorèrent les sept vaches belles à voir et grasses. Alors Pharaon s'éveilla.
5 Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
Il se rendormit, et il eut un second songe. Et voici, sept épis s'élevaient d'une même tige, gras et beaux.
6 Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
Et sept épis maigres et brûlés par le vent d'orient poussaient après ceux-là.
7 Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
Et les épis maigres engloutirent les sept épis gras et pleins. Alors Pharaon s'éveilla. Et voilà, c'était un songe.
8 Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
Le matin, Pharaon eut l'esprit agité, et il fit appeler tous les scribes et tous les sages d'Egypte. Il leur raconta ses songes, mais personne ne put les expliquer à Pharaon.
9 Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
Alors le chef des échansons, prenant la parole, dit à Pharaon: " Je vais rappeler aujourd'hui mes fautes.
10 Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
Pharaon était irrité contre ses serviteurs, et il m'avait mis en prison dans la maison du chef des gardes, moi et le chef des panetiers.
11 Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
Nous eûmes un songe dans la même nuit, moi et lui, nous révâmes chacun selon la signification de son songe.
12 Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
Il y avait là avec nous un jeune Hébreu, serviteur du chef des gardes. Nous lui racontâmes nos songes, et il nous en donna l'interprétation; à chacun il interpréta son songe,
13 Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
et les choses se passèrent comme il avait interprété: moi, Pharaon me rétablit dans mon poste, et lui, on le pendit. "
14 Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
Pharaon envoya appeler Joseph, et on le fit sortir en hâte de la prison. Il se rasa, mit d'autres vêtements et se rendit vers Pharaon.
15 Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
Et Pharaon dit à Joseph: " J'ai eu un songe que personne ne peut interpréter; et j'ai entendu dire de toi que, quand tu entends un songe, tu l'interprètes. "
16 Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
Joseph répondit à Pharaon en disant: " Ce n'est pas moi, c'est Dieu qui donnera une réponse favorable à Pharaon. "
17 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
Pharaon dit alors à Joseph: " Dans mon songe, voici, je me tenais sur le bord du fleuve,
18 nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
et voici que du fleuve montaient sept vaches grasses de chair et de belle apparence, et elles se mirent à paître dans la verdure.
19 Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
Et voici qu'après elles montaient sept autres vaches, maigres, fort laides d'aspect et décharnées; je n'en ai point vu de pareilles en laideur dans tout le pays d'Egypte.
20 Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
Les vaches maigres et laides dévorèrent les sept premières vaches, celles qui étaient grasses;
21 Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
celles-ci entrèrent dans leur ventre, sans qu'il parût qu'elles y fussent entrées; leur aspect était aussi laid qu'auparavant. Et je m'éveillai.
22 “Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
Je vis encore en songe, et voici sept épis qui s'élevaient sur une même tige, pleins et beaux;
23 Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
et voici, sept épis chétifs, maigres et brûlés par le vent d'orient, qui poussaient après ceux-là.
24 Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
Et les épis maigres engloutirent les sept beaux épis. J'ai raconté cela aux scribes, et aucun d'eux ne me l'explique. "
25 Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Joseph dit à Pharaon: " Le songe de Pharaon est un; Dieu a fait connaître à Pharaon ce qu'il va faire.
26 Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
Les sept belles vaches sont sept années, et les sept beaux épis sont sept années, c'est un seul songe.
27 Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
Les sept vaches chétives et laides qui montaient après elles sont sept années, et les sept épis vides, brûlés par le vent d'orient, seront sept années de famine.
28 “Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
Telle est la parole que j'ai dite à Pharaon: Dieu a fait voir à Pharaon ce qu'il va faire.
29 Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
Voici, sept années de grande abondance vont venir dans tout le pays d'Egypte.
30 lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
Sept années de famine viendront ensuite, et l'on oubliera toute cette abondance dans le pays d'Egypte, et la famine consumera le pays.
31 “Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
On ne s'apercevra plus de l'abondance à cause de cette famine qui suivra dans le pays; tant elle sera grande.
32 Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
Et si le songe a été répété à Pharaon deux fois, c'est que la chose est décidée de la part de Dieu, et que Dieu se hâtera de l'exécuter.
33 “Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
Maintenant, que Pharaon trouve un homme intelligent et sage, et qu'il l'établisse sur le pays d'Egypte.
34 Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
Que Pharaon établisse en outre des intendants sur le pays, pour lever un cinquième des récoltes du pays d'Egypte pendant les sept années d'abondance.
35 Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
Qu'ils rassemblent tout le produit de ces bonnes années qui viennent; qu'ils fassent des amas de blé à la disposition de Pharaon, comme provisions dans les villes, et qu'ils les conservent.
36 Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
Ces provisions seront pour le pays une réserve pour les sept années de famine qui arriveront au pays d'Egypte, et le pays ne sera pas consumé par la famine. "
37 Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
Ces paroles plurent à Pharaon et à tous ses serviteurs.
38 Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
Et Pharaon dit à ses serviteurs: " Pourrions-nous trouver un homme pareil à celui-ci, ayant en lui l'esprit de Dieu? "
39 Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
Et Pharaon dit à Joseph: " Puisque Dieu t'a fait connaître toutes ces choses, il n'y a personne qui soit aussi intelligent et sage que toi.
40 Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
C'est toi qui gouverneras ma maison, et tout mon peuple obéira à ta bouche; par le trône seulement je serai plus grand que toi. "
41 Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
Et Pharaon dit à Joseph: " Voici que je t'établis sur tout le pays d'Egypte. "
42 Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
Et Pharaon ôta son anneau de sa main et le mit à la main de Joseph, et il le fit revêtir d'habits de fin lin et lui mit au cou un collier d'or.
43 Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
Il le fit monter sur le second de ses chars, et on criait devant lui: " A genoux! " C'est ainsi qu'il fut établi sur tout le pays d'Egypte.
44 Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
Et Pharaon dit à Joseph: " Je suis Pharaon, et sans toi nul ne lèvera la main ni le pied dans tout le pays d'Egypte. "
45 Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
Pharaon nomma Joseph Tsaphnath-Panéach, et il lui donna pour femme Aseneth, fille de Putiphar, prêtre d'On. Et Joseph partit pour visiter le pays d'Egypte.
46 Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
Joseph était âgé de trente ans lorsqu'il se présenta devant Pharaon, roi d'Egypte; et il quitta Pharaon pour parcourir tout le pays d'Egypte.
47 Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
La terre rapporta à pleines mains pendant les sept années d'abondance.
48 Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
Joseph rassembla tous les produits des sept bonnes années qu'il y eut au pays d'Egypte, et il fit des approvisionnements dans les villes, déposant dans l'intérieur de chaque ville les productions des champs d'alentour.
49 Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
Joseph amassa du blé comme le sable de la mer, en si grande quantité, qu'on cessa de compter, parce qu'il était sans nombre.
50 Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
Avant qu'arrivât l'année de famine, il naquit à Joseph deux fils, que lui enfanta Aseneth, fille de Putiphar, prêtre d'On.
51 Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
Joseph donna au premier-né le nom de Manassé, " car, dit-il, Dieu m'a fait oublier toute ma peine et toute la maison de mon père. "
52 Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
Il donna au second le nom d'Ephraïm, " car, dit-il, Dieu m'a fait fructifier dans le pays de mon affliction. "
53 Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
Les sept années d'abondance qu'il y eut en Egypte étant achevées,
54 nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
les sept années de famine commencèrent à venir, comme Joseph l'avait annoncé. Il y eut famine dans tous les pays, tandis qu'il y avait du pain dans tout le pays d'Egypte.
55 Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
Puis tout le pays d'Egypte fut aussi affamé, et le peuple cria à Pharaon pour avoir du pain. Et Pharaon dit à tous les Egyptiens: " Allez vers Joseph, faites ce qu'il vous dira. "
56 Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
La famine étant sur toute la face du pays, Joseph ouvrit tous les greniers qu'on y avait établis et vendit du blé aux Egyptiens; et la famine s'accrut dans le pays d'Egypte.
57 Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.
De toute la terre on venait en Egypte pour acheter du blé auprès de Joseph; car la famine s'était aggravée sur toute la terre.

< Mwanzo 41 >