< Mwanzo 18 >
1 Bwana akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri.
Gospod se mu je prikazal na Mamrejevih ravninah, on pa je sedel pri šotorskih vratih, v vročini dneva
2 Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.
in povzdignil svoje oči in pogledal in glej, pri njem so stali trije možje in ko jih je zagledal, je stekel od šotorskih vrat, da jih sreča in se priklonil proti tlom
3 Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako.
ter rekel: »Moj Gospod, če sem torej našel naklonjenost v tvojih očeh, te prosim, ne odidi proč od svojega služabnika.
4 Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu.
Naj bo prineseno, prosim te, malo vode in umijte svoja stopala in se spočijte pod drevesom.
5 Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.”
Prinesel bom grižljaj kruha in potolažite svoja srca. Nató boste šli dalje, kajti zato ste prišli k svojemu služabniku.« In rekli so: »Stôri tako, kakor si rekel.«
6 Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara, akamwambia, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”
Abraham se je podvizal v šotor k Sari ter ji rekel: »Brž pripravi tri mere fino mlete moke, zamesi jo in na ognjišču pripravi kolače.«
7 Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye kundi, akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha.
Abraham je stekel k čredi, vzel nežno in dobro tele ter ga dal mladeniču in ta je pohitel, da ga pripravi.
8 Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.
Vzel je maslo, mleko in tele, ki ga je pripravil in to postavil prednje, in stal je poleg njih, pod drevesom, oni pa so jedli.
9 Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?” Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.”
Rekli so mu: »Kje je tvoja žena Sara?« Rekel je: »Glejte, v šotoru.«
10 Kisha Bwana akasema, “Hakika nitakurudia tena majira kama haya mwakani na Sara mkeo atakuwa ana mwana.” Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema, lililokuwa nyuma yake.
In on je rekel: »Zagotovo se bom vrnil k tebi glede na čas življenja in glej, tvoja žena Sara bo imela sina.« Sara pa je to slišala pri vratih šotora, ki je bil za njim.
11 Abrahamu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.
Torej Abraham in Sara sta bila stara in zelo zvrhana v letih in s Saro je prenehalo biti po običaju žensk.
12 Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, “Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?”
Zato se je Sara v sebi zasmejala, rekoč: »Bom še imela užitek, potem ko sem se postarala [in] je tudi moj gospod postal star?«
13 Ndipo Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Kweli nitazaa mtoto nami sasa ni mzee?’
Gospod je rekel Abrahamu: »Zakaj se je Sara zasmejala, rekoč: ›Bom zares rodila otroka jaz, ki sem stara?‹
14 Je, kuna jambo lolote gumu lisilowezekana kwa Bwana? Nitakurudia mwakani majira kama haya, naye Sara atakuwa na mwana.”
Je za Gospoda katerakoli stvar pretežka? Ob določenem času se bom vrnil k tebi, glede na čas življenja in Sara bo imela sina.«
15 Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”
Potem je Sara zanikala, rekoč: »Nisem se zasmejala, « kajti bila je prestrašena. On pa je rekel: »Ne, toda zasmejala si se.«
16 Wakati watu hao waliposimama ili waondoke, walielekeza nyuso zao Sodoma, Abrahamu akawatoa kitambo kidogo ili awasindikize.
Možje so vstali od tam in pogledali proti Sódomi in Abraham je odšel z njimi, da jih pospremi na pot.
17 Ndipo Bwana akasema, “Je, nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya?
Gospod je rekel: »Mar naj pred Abrahamom prikrijem to stvar, ki jo počnem,
18 Hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, kupitia kwake mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.
glede na to, da bo Abraham zagotovo postal velik in mogočen narod in bodo v njem blagoslovljeni vsi narodi zemlje?
19 Kwa maana nimemchagua yeye, ili awaongoze watoto wake na jamaa yake kufuata njia ya Bwana, kwa kuwa waadilifu na kutenda haki, ili Bwana atimize ahadi yake kwa Abrahamu.”
Kajti poznam ga, da bo ukazal svojim otrokom in svoji družini za njim in se bodo držali Gospodove poti, da izvajajo pravičnost in sodbo, da bo Gospod nad Abrahama lahko privedel to, kar je govoril o njem.«
20 Basi Bwana akasema, “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora ni kikubwa sana na dhambi yao inasikitisha sana,
Gospod je rekel: »Ker je vpitje Sódome in Gomóre veliko in ker je njihov greh zelo boleč,
21 kwamba nitashuka nione kama waliyoyatenda ni mabaya kiasi cha kilio kilichonifikia. Kama sivyo, nitajua.”
bom torej šel dol in pogledal, ali so storili povsem glede na njihovo vpitje, ki je prišlo do mene; in če ne, bom vedel.«
22 Basi wale watu wakageuka wakaenda kuelekea Sodoma, lakini Abrahamu akabaki amesimama mbele za Bwana.
Možje so svoje obraze obrnili od tam in odšli proti Sódomi, toda Abraham je kljub temu stopil pred Gospoda.
23 Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu?
Abraham se je približal in rekel: »Hočeš prav tako uničiti pravične z zlobnimi?
24 Je, ikiwa watakuwepo watu wenye haki hamsini katika mji huo, hivi kweli utauangamiza na wala hutauacha kwa ajili ya hao watu hamsini wenye haki waliomo ndani yake?
Morda je znotraj mesta petdeset pravičnih. Hočeš prav tako uničiti kraj in mu ne prizanesti zaradi petdesetih pravičnih, ki so v njem?
25 Hilo na liwe mbali nawe, kufanya jambo kama hilo, kuwaua wenye haki pamoja na waovu, kuwatendea wenye haki sawasawa na waovu. Iwe mbali nawe! Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa?”
To bodi daleč od tebe, da storiš na ta način, da z zlobnimi pokončaš pravične in da bi bili pravični kakor zlobni, to bodi daleč od tebe. Mar ne bo Sodnik vse zemlje storil pravično?«
26 Bwana akasema, “Kama nikipata watu hamsini wenye haki katika mji wa Sodoma, nitausamehe huo mji wote kwa ajili yao.”
Gospod je rekel: »Če najdem v Sódomi, znotraj mesta, petdeset pravičnih, potem bom zaradi njih prizanesel celemu kraju.«
27 Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu;
Abraham pa je odgovoril in rekel: »Glej torej, nase, ki sem samo prah in pepel, sem vzel, da govorim Gospodu.
28 je, kama hesabu ya wenye haki imepungua watano katika hamsini, utauangamiza huo mji wote kwa ajili ya hao watano waliopungua?” Bwana akamwambia, “Kama nikiwakuta huko watu arobaini na watano, sitauangamiza.”
Morda jih bo manjkalo pet do petdesetih pravičnih. Hočeš mesto uničiti zaradi pomanjkanja petih?« On pa je rekel: »Če jih najdem tam petinštirideset, ga ne bom uničil.«
29 Abrahamu akazungumza naye kwa mara nyingine, “Je, kama huko watapatikana watu arobaini tu?” Akamjibu, “Kwa ajili ya hao arobaini, sitauangamiza.”
Ponovno mu je spregovoril in rekel: »Morda jih bo tam najdenih štirideset.« On pa je rekel: » Tega ne bom storil zaradi štiridesetih.«
30 Ndipo akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze. Je, kama huko watakuwepo thelathini tu?” Akajibu, “Sitapaangamiza ikiwa nitawakuta huko watu thelathini.”
Rekel mu je: »Oh naj moj Gospod ne bo jezen, jaz pa bom govoril: ›Morda jih bo tam najdenih trideset.‹« On pa je rekel: » Tega ne bom storil, če jih tam najdem trideset.«
31 Abrahamu akasema, “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri sana kuzungumza na Bwana, je, kama wakipatikana huko watu ishirini tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao ishirini, sitauangamiza.”
Rekel je: »Glej torej, vzel sem nase, da govorim Gospodu: ›Morda jih bo tam najdenih dvajset.‹« On pa je rekel: »Ne bom ga uničil zaradi dvajsetih.«
32 Abrahamu akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze tena mara moja tu. Itakuwaje kama watapatikana huko watu kumi tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao kumi, sitauangamiza.”
Rekel je: »Oh naj Gospod ne bo jezen, jaz pa bom govoril samo še tokrat: ›Morda jih bo tam najdenih deset.‹« On pa je rekel: »Ne bom ga uničil zaradi desetih.«
33 Bwana alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, akaondoka, naye Abrahamu akarudi nyumbani kwake.
Gospod je odšel svojo pot takoj, ko je prenehal govoriti z Abrahamom. Abraham pa se je vrnil na svoj kraj.