< Mwanzo 28 >
1 Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani.
Izak je poklical Jakoba, ga blagoslovil, mu naročil ter mu rekel: »Ne boš si vzel žene izmed Kánaanovih hčera.
2 Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako.
Vstani, pojdi v Padan–aram, k hiši Betuéla, očeta tvoje matere in od tam si vzemi ženo izmed hčera Labána, brata tvoje matere.
3 Mungu Mwenyezi na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu.
Bog Vsemogočni naj te blagoslovi in te naredi rodovitnega in te namnoži, da boš lahko postal množica ljudstva
4 Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.”
in ti da Abrahamov blagoslov, tebi in tvojemu semenu s teboj, da boš lahko podedoval deželo, v kateri si tujec, ki jo je Bog dal Abrahamu.«
5 Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.
Izak je odposlal Jakoba in ta je odšel v Padan–aram, k Labánu, sinu Sirca Betuéla, brata Jakobove in Ezavove matere Rebeke.
6 Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,”
Ko je Ezav videl, da je Izak blagoslovil Jakoba in ga odposlal v Padan–aram, da si od tam vzame ženo in da mu je med blagoslovom dal naročilo, rekoč: »Ne boš si vzel žene izmed Kánaanovih hčera, «
7 tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu.
in da je Jakob ubogal svojega očeta in svojo mater ter odšel v Padan–aram,
8 Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani.
je Ezav videl, da Kánaanove hčere njegovemu očetu Izaku niso ugajale
9 Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.
in je Ezav potem odšel k Izmaelu in si k ženama, ki ju je imel, vzel Mahaláto, hčer Abrahamovega sina Izmaela, Nebajótovo sestro, da postane njegova žena.
10 Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani.
Jakob pa je odšel iz Beeršébe in odšel proti Haránu.
11 Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi.
Ker pa je sonce zašlo, se je spustil na nek kraj in se tam vso noč zadrževal in vzel je kamne tega kraja in jih položil za svoje blazine in se ulegel na ta kraj, da zaspi.
12 Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake.
Sanjal je in glej lestev, postavljeno na zemljo in njen vrh je segal do nebes. In glej, Božji angeli so se vzpenjali in spuščali po njej.
13 Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
In glej, Gospod je stal nad njo ter rekel: »Jaz sem Gospod, Bog tvojega očeta Abrahama in Izakov Bog. Deželo, na kateri ležiš, bom dal tebi in tvojemu semenu.
14 Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa.
Tvojega semena bo kakor zemeljskega prahu in razširjen boš na zahod, na vzhod, na sever in na jug. In v tebi in v tvojem semenu bodo blagoslovljene vse družine zemlje.
15 Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”
Glej, jaz sem s teboj in varoval te bom na vseh krajih, kamor greš in ponovno te bom privedel v to deželo, kajti ne bom te zapustil, dokler ne storim tega, o čemer sem ti govoril.«
16 Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.”
Jakob se je zbudil iz svojega spanja in rekel: »Zagotovo je na tem kraju Gospod, jaz pa tega nisem vedel.«
17 Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”
Bil je prestrašen in rekel: »Kako grozen je ta kraj! To ni nič drugega kakor Božja hiša in to so velika nebeška vrata.«
18 Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
Jakob je zgodaj zjutraj vstal in vzel kamen, ki ga je podstavil za svoje blazine in ga postavil za steber in nanj, na njegov vrh, izlil olje.
19 Mahali pale akapaita Betheli, ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.
Ime tega kraja je imenoval Betel, toda ime tega kraja je bilo najprej imenovano Luz.
20 Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae
Jakob se je zaobljubil, rekoč: »Če bo Bog z menoj in me bo varoval na tej poti, ki jo hodim in mi bo dal za jesti kruha in oblačilo, da ga oblečem,
21 na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu,
tako da ponovno v miru pridem k hiši svojega očeta, potem bo Gospod moj Bog.
22 nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”
In ta kamen, ki sem ga postavil za steber, bo Božja hiša. Od vsega, kar mi boš dal, ti bom zagotovo dajal desetino.«