< Mwanzo 10 >

1 Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
These ben the generaciouns of the sones of Noe, Sem, Cham, and Jafeth. And sones weren borun to hem aftir the greet flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
The sones of Jafeth weren Gomer, and Magog, and Madai, and Jauan, and Tubal, and Mosoth, and Thiras.
3 Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
Forsothe the sones of Gomer weren Asseneth, and Rifath, and Thogorma.
4 Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
Forsothe the sones of Jauan weren Helisa, and Tharsis, Cethym, and Dodanym;
5 (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
of these sones the ylis of hethen men weren departid in her cuntrees, ech bi his langage and meynees, in hise naciouns.
6 Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
Sotheli the sones of Cham weren Thus, and Mesraym, and Futh, and Chanaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
Forsothe the sones of Thus weren Saba, and Euila, and Sabatha, and Regma, and Sabatacha. The sones of Regma weren Saba, and Dadan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
Forsothe Thus gendride Nemroth; he bigan to be myyti in erthe,
9 Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
and he was a strong huntere of men bifore the Lord; of hym a prouerbe yede out, as Nemroth, a strong huntere bifore the Lord.
10 Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
Sotheli the bigynnyng of his rewme was Babiloyne, and Arach, and Archad, and Thalamye, in the lond of Sennaar.
11 Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
Assur yede out of that lond, and bildide Nynyue, `and stretis of the citee,
12 na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
and Chale, and Resen bitwixe Nynyue and Chale; this is a greet citee.
13 Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
And sotheli Mesraym gendride Ludym, and Anamym, and Laabym, Neptuym, and Ferrusym, and Cesluym;
14 Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
of which the Filisteis and Capturym camen forth.
15 Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
Forsothe Chanaan gendride Sidon, his firste gendride sone, Ethei, and Jebusei,
16 Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
and Amorrei, Gergesei,
17 Wahivi, Waariki, Wasini,
Euei, and Arathei,
18 Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
Ceney, and Aradie, Samarites, and Amathei; and puplis of Chananeis weren sowun abrood bi these men.
19 na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
And the termes of Chanaan weren maad to men comynge fro Sidon to Gerara, til to Gasa, til thou entre in to Sodom and Gomore, and Adama, and Seboyne, til to Lesa.
20 Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These weren the sones of Cham, in her kynredis, and langagis, and generaciouns, and londis, and folkis.
21 Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
Also of Sem weren borun the fadris of alle the sones of Heber, and Japhet was the more brother.
22 Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
The sones of Sem weren Elam, and Assur, and Arfaxath, and Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
The sones of Aram weren Vs, and Hul, and Gether, and Mes.
24 Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
And sotheli Arfaxath gendride Sale, of whom Heber was borun.
25 Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
And twei sones weren borun to Heber, the name to o sone was Faleg, for the lond was departid in hise daies; and the name of his brothir was Jectan.
26 Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
And thilke Jectan gendride Elmodad, and Salech,
27 Hadoramu, Uzali, Dikla,
and Asamoth, Jare, and Adhuram, and Vsal,
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
and Deda, and Ebal, and Abymahel, Saba, and Ofir, and Euila, and Jobab;
29 Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
alle these weren the sones of Jectan.
30 Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
And the habitacioun of hem was maad fro Messa, as `me goith til to Sefar, an hil of the eest.
31 Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
These ben the sones of Sem, bi kynredis, and langagis, and cuntrees, in her folkis.
32 Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
These ben the meynees of Noe, bi her puplis and naciouns; folkis in erthe weren departid of these aftir the greet flood.

< Mwanzo 10 >