< Mwanzo 12 >

1 Bwana akawa amemwambia Abramu, “Ondoka kutoka nchi yako, uache jamii yako na nyumba ya baba yako, uende hadi nchi nitakayokuonyesha.
Forsothe the Lord seide to Abram, Go thou out of thi lond, and of thi kynrede, and of the hous of thi fadir, and come thou in to the lond which Y schal schewe to thee;
2 “Mimi nitakufanya taifa kubwa na nitakubariki, Nitalikuza jina lako, nawe utakuwa baraka.
and Y schal make thee in to a greet folk, and Y schal blisse thee, and Y schal magnyfie thi name, and thou schalt be blessid;
3 Nitawabariki wale wanaokubariki, na yeyote akulaaniye nitamlaani; na kupitia kwako mataifa yote duniani yatabarikiwa.”
Y schal blesse hem that blessen thee, and Y schal curse hem that cursen thee; and alle kynredis of erthe schulen be blessid in thee.
4 Hivyo Abramu akaondoka kama Bwana alivyokuwa amemwambia; naye Loti akaondoka pamoja naye. Wakati Abramu alipoitwa aondoke Harani, alikuwa na miaka sabini na mitano.
And so Abram yede out, as the Lord comaundide hym, and Loth yede with hym. Abram was of `thre scoor yeer and fiftene whanne he yede out of Aran.
5 Abramu akamchukua Sarai mkewe pamoja na Loti mwana wa ndugu yake, mali zote walizokuwa nazo pamoja na watu aliokuwa amewapata huko Harani, wakasafiri mpaka nchi ya Kanaani, wakafika huko.
And he took Saray, his wijf, and Loth, the sone of his brother, and al the substaunce which thei hadden in possessioun, and the men whiche thei hadden bigete in Aran; and thei yeden out that thei `schulen go in to the loond of Chanaan. And whanne they camen in to it,
6 Abramu akasafiri katika nchi hiyo akafika huko Shekemu, mahali penye mti wa mwaloni ulioko More. Wakati huo Wakanaani walikuwa wanaishi katika nchi hiyo.
Abram passide thorou the lond til to the place of Sichem, and til to the noble valey. Forsothe Chananei was thanne in the lond.
7 Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, “Nitawapa uzao wako nchi hii.” Hivyo hapa akamjengea madhabahu Bwana aliyekuwa amemtokea.
Sotheli the Lord apperide to Abram, and seide to hym, Y schal yyue this lond to thi seed. And Abram bildide there an auter to the Lord, that apperide to hym.
8 Kutoka huko Abramu akasafiri kuelekea kwenye vilima mashariki ya Betheli, naye akapiga hema huko, Betheli ikiwa upande wa magharibi na Ai upande wa mashariki. Huko alimjengea Bwana madhabahu na akaliitia jina la Bwana.
And fro thennus he passide forth to the hil Bethel, that was ayens the eest, and settide there his tabernacle, hauynge Bethel fro the west, and Hay fro the eest. And he bildide also there an auter to the Lord, and inwardli clepide his name.
9 Kisha Abramu akasafiri kuelekea upande wa Negebu.
And Abram yede goynge and goynge forth ouer to the south.
10 Basi kulikuwako na njaa katika nchi, naye Abramu akashuka kwenda Misri kukaa huko kwa muda, kwa maana njaa ilikuwa kali.
Sotheli hungur was maad in the lond; and Abram yede doun in to Egipt, to be a pilgrime ther, for hungur hadde maistrie in the lond.
11 Alipokuwa karibu kuingia Misri, akamwambia Sarai mkewe, “Ninajua ya kwamba wewe ni mwanamke mzuri wa sura.
And whanne he was nyy to entre in to Egipt, he seide to Saray, his wijf, Y knowe that thou art a fair womman,
12 Wakati Wamisri watakapokuona, watasema, ‘Huyu ni mke wake.’ Ndipo wataniua, lakini wewe watakuacha hai.
and that whanne Egipcians schulen se thee, thei schulen seie, it is his wijf, and thei schulen sle me, and `schulen reserue thee.
13 Sema wewe ni dada yangu, ili nitendewe mema kwa ajili yako, na maisha yangu yatahifadhiwa kwa sababu yako.”
Therfor, Y biseche thee, seie thou, that thou art my sistir, that it be wel to me for thee, and that my lijf lyue for loue of thee.
14 Abramu alipoingia Misri, Wamisri wakamwona Sarai kuwa ni mwanamke mzuri sana wa sura.
And so whanne Abram hadde entrid in to Egipt, Egipcians sien the womman that sche was ful fair; and the prynces telden to Farao, and preiseden hir anentis him;
15 Maafisa wa Farao walipomwona, wakamsifia kwa Farao; ndipo Sarai akapelekwa kwa nyumba ya mfalme.
and the womman was takun vp in to the hous of Farao.
16 Kwa ajili ya Sarai, Farao akamtendea Abramu mema, naye Abramu akapata kondoo, ngʼombe, punda, ngamia na watumishi wa kiume na wa kike.
Forsothe thei vsiden wel Abram for hir; and scheep, and oxun, and assis, and seruauntis, and seruauntessis, and sche assis, and camels weren to hym.
17 Lakini Bwana akamwadhibu Farao na nyumba yake kwa maradhi ya kufisha kwa sababu ya kumchukua Sarai, mke wa Abramu.
Forsothe the Lord beet Farao and his hous with moste veniaunces, for Saray, the wijf of Abram.
18 Ndipo Farao akamwita Abramu, akamuuliza, “Umenifanyia nini? Kwa nini hukuniambia ni mke wako?
And Farao clepide Abram, and seide to hym, What is it that thou hast do to me? whi schewidist thou not to me, that sche was thi wijf?
19 Kwa nini ulisema, ‘Yeye ni dada yangu,’ hata nikamchukua kuwa mke wangu? Sasa basi, mke wako huyu hapa. Mchukue uende zako!”
for what cause seidist thou, that sche was thi sister, that Y schulde take hir in to wife to me? Now therfor lo! thi wiif; take thou hir, and go.
20 Kisha Farao akawapa watu wake amri kuhusu Abramu, wakamsindikiza pamoja na mke wake na kila alichokuwa nacho.
And Farao comaundide to men on Abram, and thei ledden forth hym, and his wijf, and alle thingis that he hadde.

< Mwanzo 12 >