< Torati 16 >

1 Shikeni mwezi wa Abibu, na kuiadhimisha Pasaka ya Bwana Mungu wenu, kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Mungu aliwatoa Misri usiku.
to keep: obey [obj] month [the] Abib and to make: do Passover to/for LORD God your for in/on/with month [the] Abib to come out: send you LORD God your from Egypt night
2 Mtatoa dhabihu ya Pasaka ya mnyama kwa Bwana Mungu wenu kutoka kundi lenu la mbuzi na kondoo au la ngʼombe, mahali pale ambapo Bwana atapachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake.
and to sacrifice Passover to/for LORD God your flock and cattle in/on/with place which to choose LORD to/for to dwell name his there
3 Msile nyama hiyo pamoja na mikate iliyotiwa chachu, lakini kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu, mikate ya kujitesa, kwa sababu mliondoka Misri kwa haraka, ili kwamba siku zote za maisha yenu mpate kukumbuka wakati wenu wa kuondoka Misri.
not to eat upon him leaven seven day to eat upon him unleavened bread food: bread affliction for in/on/with haste to come out: come from land: country/planet Egypt because to remember [obj] day to come out: come you from land: country/planet Egypt all day life your
4 Chachu isionekane katika mali zenu katika nchi yenu yote kwa siku saba. Nyama yoyote ya dhabihu mtakayotoa jioni ya siku ya kwanza isibakizwe mpaka asubuhi.
and not to see: see to/for you leaven in/on/with all border: area your seven day and not to lodge from [the] flesh which to sacrifice in/on/with evening in/on/with day [the] first to/for morning
5 Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mungu wenu amewapa,
not be able to/for to sacrifice [obj] [the] Passover in/on/with one gate: town your which LORD God your to give: give to/for you
6 isipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri.
that if: except if: except to(wards) [the] place which to choose LORD God your to/for to dwell name his there to sacrifice [obj] [the] Passover in/on/with evening like/as to come (in): (sun)set [the] sun meeting: time appointed to come out: come you from Egypt
7 Okeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu.
and to boil and to eat in/on/with place which to choose LORD God your in/on/with him and to turn in/on/with morning and to go: went to/for tent your
8 Kwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mungu wenu na msifanye kazi.
six day to eat unleavened bread and in/on/with day [the] seventh assembly to/for LORD God your not to make: do work
9 Mhesabu majuma saba tangu wakati mnapoanza kuchukua mundu kuvuna nafaka.
seven week to recount to/for you from to profane/begin: begin sickle in/on/with standing grain to profane/begin: begin to/for to recount seven week
10 Kisha msherehekee Sikukuu ya Majuma kwa Bwana Mungu wenu kwa kutoa sadaka ya hiari kwa kadiri ya baraka ambayo Bwana Mungu wenu amewapa.
and to make: do feast Weeks to/for LORD God your payment voluntariness hand your which to give: give like/as as which to bless you LORD God your
11 Shangilieni mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua kama makao ya Jina lake, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi walio katika miji yenu, na wageni, yatima na wajane waishio miongoni mwenu.
and to rejoice to/for face: before LORD God your you(m. s.) and son: child your and daughter your and servant/slave your and maidservant your and [the] Levi which in/on/with gate: town your and [the] sojourner and [the] orphan and [the] widow which in/on/with entrails: among your in/on/with place which to choose LORD God your to/for to dwell name his there
12 Kumbukeni kwamba mlikuwa watumwa kule Misri na mfuate amri hizi kwa uangalifu.
and to remember for servant/slave to be in/on/with Egypt and to keep: careful and to make: do [obj] [the] statute: decree [the] these
13 Adhimisheni sikukuu ya vibanda kwa siku saba baada ya kukusanya mazao yenu ya nafaka na kukamua zabibu.
feast [the] booth to make: do to/for you seven day in/on/with to gather you from threshing floor your and from wine your
14 Mfurahie sikukuu yenu, ninyi, wana wenu, binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, Walawi, wageni, yatima na wajane ambao wanaishi katika miji yenu.
and to rejoice in/on/with feast your you(m. s.) and son: child your and daughter your and servant/slave your and maidservant your and [the] Levi and [the] sojourner and [the] orphan and [the] widow which in/on/with gate: town your
15 Kwa siku saba mtaiadhimisha sikukuu ya Bwana Mungu wenu katika mahali atakapopachagua Bwana. Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki katika mavuno yenu na katika kazi zote za mikono yenu na furaha yenu itakamilika.
seven day to celebrate to/for LORD God your in/on/with place which to choose LORD for to bless you LORD God your in/on/with all produce your and in/on/with all deed: work hand your and to be surely glad
16 Wanaume wenu wote lazima wajitokeze mara tatu kwa mwaka mbele za Bwana Mungu wenu mahali atakapopachagua: kwa ajili ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda. Hakuna mtu atakayejitokeza mbele za Bwana mikono mitupu:
three beat in/on/with year to see: see all male your with face: before LORD God your in/on/with place which to choose in/on/with feast [the] unleavened bread and in/on/with feast [the] Weeks and in/on/with feast [the] booth and not to see: see with face: before LORD emptily
17 Kila mmoja wenu ni lazima alete zawadi kulingana na jinsi ambavyo Bwana Mungu wenu alivyowabariki.
man: anyone like/as gift hand: power his like/as blessing LORD God your which to give: give to/for you
18 Wateue waamuzi na maafisa kwa kila kabila lenu katika kila mji ambao Bwana Mungu wenu anawapa, nao watawaamua watu kwa usawa.
to judge and official to give: put to/for you in/on/with all gate: town your which LORD God your to give: give to/for you to/for tribe your and to judge [obj] [the] people justice: judgement righteousness
19 Msipotoshe haki wala msifanye upendeleo. Msikubali rushwa kwa sababu rushwa hupofusha macho ya wenye busara na kugeuza maneno ya wenye haki.
not to stretch justice not to recognize face: kindness and not to take: recieve bribe for [the] bribe to blind eye wise and to pervert word: case righteous
20 Mfuate haki na haki peke yake, ili mweze kuishi na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa.
righteousness righteousness to pursue because to live and to possess: take [obj] [the] land: country/planet which LORD God your to give: give to/for you
21 Msisimamishe nguzo yoyote ya Ashera kando ya madhabahu mliyomjengea Bwana Mungu wenu,
not to plant to/for you Asherah all tree beside altar LORD God your which to make to/for you
22 wala msisimamishe jiwe la kuabudu, kwa maana Bwana Mungu wenu anavichukia vitu hivi.
and not to arise: establish to/for you pillar which to hate LORD God your

< Torati 16 >