< Torati 10 >
1 Wakati ule Bwana aliniambia, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza uje kwangu juu mlimani. Pia utengeneze Sanduku la mbao.
En ce temps-là, Yahvé me dit: « Coupe deux tables de pierre comme les premières, et monte vers moi sur la montagne, et fais une arche de bois.
2 Nitaandika juu ya vibao maneno yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza, ambavyo ulivivunja. Kisha utaviweka ndani ya Sanduku.”
J'écrirai sur ces tablettes les paroles qui étaient sur les premières tablettes que tu as brisées, et tu les mettras dans l'arche. »
3 Hivyo nikatengeneza Sanduku kwa mti wa mshita, nikachonga pia vibao vya mawe kama vile vya kwanza, kisha nikakwea mlimani nikiwa na vibao viwili mikononi mwangu.
Je fis donc une arche de bois d'acacia, je taillai deux tablettes de pierre comme les premières, et je montai sur la montagne, les deux tablettes à la main.
4 Bwana akaandika juu ya hivi vibao kile alichokuwa amekiandika kabla, Amri Kumi alizokuwa amewatangazia juu mlimani, kutoka kwenye moto siku ile ya kusanyiko. Bwana akanikabidhi.
Il écrivit sur les tables, selon la première écriture, les dix commandements dont Yahvé vous a parlé sur la montagne, du milieu du feu, le jour de l'assemblée; et Yahvé me les donna.
5 Kisha nikashuka kutoka mlimani na kuweka vibao ndani ya Sanduku nililokuwa nimelitengeneza, kama Bwana alivyoniagiza, navyo viko huko sasa.
Je me suis retourné et je suis descendu de la montagne, et j'ai mis les tables dans l'arche que j'avais faite; et elles y sont comme l'Éternel me l'a ordonné.
6 (Waisraeli walisafiri kutoka visima vya Yaakani hadi Mosera. Huko Aroni alifariki na kuzikwa, naye Eleazari mwanawe akachukua nafasi yake kama kuhani.
(Les enfants d'Israël partirent de Beeroth Bene Jaakan pour se rendre à Mosérah. C'est là qu'Aaron mourut et qu'il fut enterré, et son fils Éléazar exerça le sacerdoce à sa place.
7 Kutoka pale, walisafiri hadi Gudgoda wakaendelea mpaka Yotbatha, nchi yenye vijito vya maji.
De là, ils partirent pour Gudgoda, et de Gudgoda pour Jotbatha, pays de ruisseaux.
8 Wakati huo Bwana aliteua kabila la Lawi kulibeba Sanduku la Agano la Bwana, kusimama mbele za Bwana ili kutoa huduma, na kutangaza baraka kwa Jina lake, kama wanavyofanya mpaka leo.
En ce temps-là, Yahvé mit à part la tribu de Lévi pour porter l'arche de l'alliance de Yahvé, pour se tenir devant Yahvé, pour le servir et pour bénir en son nom, jusqu'à ce jour.
9 Hiyo ndiyo sababu ya Walawi kutokuwa na sehemu wala urithi miongoni mwa ndugu zao; Bwana ndiye urithi wao, kama Bwana Mungu wao alivyowaambia.)
C'est pourquoi Lévi n'a ni part ni héritage avec ses frères; son héritage, c'est Yahvé, selon ce que Yahvé ton Dieu lui a dit).
10 Basi nilikaa mlimani kwa siku arobaini usiku na mchana, kama nilivyofanya mara ya kwanza, pia Bwana alinisikiliza hata wakati huu. Haikuwa nia yake kuwaangamiza.
Je suis resté sur la montagne, comme la première fois, quarante jours et quarante nuits, et l'Éternel m'a écouté cette fois-là aussi. L'Éternel n'a pas voulu te détruire.
11 Bwana akaniambia, “Nenda, ukawaongoze watu katika njia yao ili kwamba waweze kuingia na kuimiliki nchi ile niliyowaapia baba zao kuwapa.”
Yahvé me dit: « Lève-toi, pars devant le peuple, et ils entreront en possession du pays que j'ai juré à leurs pères de leur donner. »
12 Na sasa, ee Israeli, Bwana Mungu wako anataka nini kwako ila kumcha Bwana Mungu wako, kwenda katika njia zake, kumpenda na kumtumikia Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote,
Maintenant, Israël, qu'est-ce que l'Éternel, ton Dieu, exige de toi, sinon que tu craignes l'Éternel, ton Dieu, que tu marches dans toutes ses voies, que tu l'aimes et que tu serves l'Éternel, ton Dieu, de tout ton cœur et de toute ton âme,
13 na kuyashika maagizo ya Bwana na amri zake ninazokupa leo kwa mafanikio yako mwenyewe?
en observant les commandements et les lois de l'Éternel, que je te prescris aujourd'hui pour ton bien?
14 Mbingu, hata mbingu za juu sana, dunia na kila kitu kilichomo ndani yake, ni mali ya Bwana Mungu wako.
Voici, à l'Éternel, ton Dieu, appartiennent le ciel, le ciel des cieux, et la terre, avec tout ce qu'elle contient.
15 Hata hivyo Bwana alikuwa na shauku na baba zako, akawapenda na akawachagua ninyi, wazao wao, kuliko mataifa yote, kama ilivyo leo.
Seulement, l'Éternel a pris plaisir à vos pères pour les aimer, et il a choisi leur descendance après eux, même vous par-dessus tous les peuples, comme il en est aujourd'hui.
16 Kwa hiyo tahirini mioyo yenu, na msiwe na shingo ngumu tena.
Circoncise donc le prépuce de ton cœur, et ne sois plus un cou rigide.
17 Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa mabwana, Mungu mkuu, mwenye uweza na wa kutisha, ambaye hana upendeleo na hapokei rushwa.
Car Yahvé, ton Dieu, est le Dieu des dieux et le Seigneur des seigneurs, le grand Dieu, le puissant et l'imposant, qui ne respecte pas les personnes et n'accepte pas les pots-de-vin.
18 Huwapigania yatima na wajane, humpenda mgeni, akimpa chakula na mavazi.
Il fait justice à l'orphelin et à la veuve, et il aime l'étranger en lui donnant nourriture et vêtement.
19 Nanyi wapendeni wageni, kwa kuwa ninyi wenyewe mlikuwa wageni huko Misri.
C'est pourquoi, aimez l'étranger, car vous avez été étrangers au pays d'Égypte.
20 Mche Bwana Mungu wako na umtumikie yeye. Shikamana naye kwa uthabiti na kuapa kwa jina lake.
Tu craindras Yahvé, ton Dieu. Tu le serviras. Tu t'attacheras à lui et tu jureras par son nom.
21 Yeye ni sifa yako; yeye ni Mungu wako, ambaye alikutendea yale maajabu makubwa na ya kutisha uliyoyaona kwa macho yako mwenyewe.
C'est lui qui te loue et c'est lui qui est ton Dieu, qui a fait pour toi ces choses grandes et impressionnantes que tes yeux ont vues.
22 Baba zako walioshuka kwenda Misri jumla yao walikuwa sabini, na sasa Bwana Mungu wako amekufanya wengi kama nyota za angani.
Tes pères sont descendus en Égypte avec soixante-dix personnes; et maintenant Yahvé ton Dieu t'a rendu comme les étoiles du ciel pour la multitude.