< Torati 12 >
1 Hizi ndizo amri na sheria ambazo ni lazima mwe waangalifu kuzifuata katika nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa kumiliki, kwa muda wote mtakaoishi katika nchi.
Voici les lois et les ordonnances que vous observerez et que vous mettrez en pratique dans le pays que l'Éternel, le Dieu de vos pères, vous donne en possession tous les jours que vous vivrez sur la terre.
2 Haribuni kabisa kila mahali pao pa kuabudia kwenye milima mirefu, vilima na chini ya kila mti mkubwa ambamo mataifa haya mnayokwenda kuchukua ardhi yao huabudia miungu yao.
Vous détruirez tous les lieux où les nations que vous allez déposséder servaient leurs dieux, sur les hautes montagnes, sur les collines et sous tout arbre vert.
3 Bomoeni madhabahu zao, vunjeni yale mawe wanayoabudu, chomeni moto nguzo zao za Ashera; katilieni mbali sanamu za miungu yao na mfute majina yao mahali hapo.
Tu briseras leurs autels, tu mettras en pièces leurs colonnes et tu brûleras au feu leurs mâts d'ashère. Tu abattras les images gravées de leurs dieux. Tu détruiras leur nom hors de ce lieu.
4 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kama wanavyoabudu wao.
Tu n'agiras pas ainsi à l'égard de Yahvé, ton Dieu.
5 Bali mtatafuta mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua katika makabila yenu yote ili aliweke jina lake huko kuwa makao yake. Mahali hapo ndipo iwapasapo kwenda;
Mais au lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira parmi toutes tes tribus pour y placer son nom, tu chercheras sa demeure, et tu y viendras.
6 hapo ndipo mtakapoleta sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo zenu, kile ulichoweka nadhiri kutoa, sadaka zenu za hiari na malimbuko ya makundi yenu ya ngʼombe pamoja na mbuzi na kondoo.
Tu y apporteras tes holocaustes, tes sacrifices, tes dîmes, l'offrande de ta main, tes vœux, tes offrandes volontaires, et les premiers-nés de ton gros et de ton menu bétail.
7 Hapo, katika uwepo wa Bwana Mungu wenu, ninyi pamoja na jamaa zenu, mtakula na kufurahia kila kitu ambacho mmegusa kwa mikono yenu, kwa sababu Bwana Mungu wenu amewabariki.
C'est là que tu mangeras devant l'Éternel, ton Dieu, et que tu te réjouiras de tout ce que tu auras entrepris, toi et tes familles, et pour lequel l'Éternel, ton Dieu, t'aura béni.
8 Msifanye kama tunavyofanya hapa leo, kila mtu anavyopenda mwenyewe,
Vous ne ferez pas toutes les choses que nous faisons ici aujourd'hui, chacun faisant ce qui est juste à ses propres yeux;
9 kwa kuwa bado hamjafikia mahali pa mapumziko na urithi ambao Bwana Mungu wenu anawapa.
car vous n'êtes pas encore arrivés au repos et à l'héritage que l'Éternel, votre Dieu, vous donne.
10 Lakini mtavuka Yordani na kuishi katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kama urithi, naye atawapa pumziko kutokana na adui zenu wote wanaowazunguka ili ninyi mpate kuishi kwa salama.
Mais quand tu auras passé le Jourdain et que tu seras établi dans le pays que l'Éternel, ton Dieu, te donne en héritage, quand il t'aura délivré de tous tes ennemis qui t'entourent et que tu habiteras en sécurité,
11 Kisha kuhusu mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua kuwa mahali pa makao ya Jina lake, hapo ndipo inapowapasa kuleta kila kitu ninachowaamuru: sadaka zenu za kuteketezwa na dhabihu, zaka zenu na changizo, pamoja na vitu vyote vyenye thamani ambavyo mmeweka nadhiri kumtolea Bwana.
alors, au lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y faire résider son nom, tu apporteras tout ce que je t'ordonnerai: tes holocaustes, tes sacrifices, tes dîmes, l'offrande de ta main, et tous les vœux que tu feras à l'Éternel.
12 Hapo furahini mbele za Bwana Mungu wenu, ninyi, wana wenu na binti zenu, watumishi wenu wa kiume na wa kike, pamoja na Walawi kutoka miji yenu ambao hawana mgawo wala urithi wao wenyewe.
Tu te réjouiras devant l'Éternel, ton Dieu, toi, tes fils, tes filles, tes serviteurs, tes servantes, et le Lévite qui est dans tes portes, car il n'a ni part ni héritage avec toi.
13 Kuweni waangalifu, msitoe dhabihu zenu za kuteketezwa mahali popote mnapopapenda.
Prends garde de ne pas offrir tes holocaustes dans tous les lieux que tu verras;
14 Mtazitoa tu mahali pale ambapo Bwana atachagua katika mojawapo ya makabila yenu, nanyi hapo zingatieni kila jambo ninalowaamuru.
mais dans le lieu que l'Éternel choisira dans l'une de tes tribus, là tu offriras tes holocaustes, et là tu feras tout ce que je te commanderai.
15 Hata hivyo, mnaweza kuwachinja wanyama wenu katika miji yenu yoyote ile na kula nyama nyingi mpendavyo kama vile mmemchinja paa au kulungu, kulingana na baraka mtakazojaliwa na Bwana Mungu wenu. Watu walio najisi au walio safi wanaweza kula.
Mais tu pourras tuer et manger de la viande dans toutes tes portes, selon tous les désirs de ton âme, selon la bénédiction que Yahvé ton Dieu t'a accordée. L'impur et le pur pourront en manger, comme de la gazelle et du cerf.
16 Lakini kamwe usinywe damu; imwage juu ya ardhi kama maji.
Seulement, tu ne mangeras pas le sang. Tu le répandras sur la terre comme de l'eau.
17 Hamruhusiwi kula katika miji yenu zaka yenu ya nafaka, ya divai mpya na ya mafuta, au mzaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na makundi yenu ya mbuzi na kondoo, wala chochote ambacho mmeweka nadhiri kukitoa, au sadaka zako za hiari, wala matoleo maalum.
Tu ne mangeras pas dans tes portes la dîme de ton blé, de ton moût ou de ton huile, ni les premiers-nés de ton gros et de ton menu bétail, ni les vœux que tu fais, ni les offrandes volontaires, ni l'offrande de ta main.
18 Badala yake, mtakula vitu hivyo katika uwepo wa Bwana Mungu wenu mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua: wewe, wana wako na binti zako, watumishi wako wa kiume na wa kike, na Walawi kutoka miji yenu. Mnatakiwa mfurahi mbele za Bwana Mungu wenu kwa kula kitu mtakachoweka mikono yenu.
Mais tu les mangeras devant Yahvé ton Dieu, dans le lieu que choisira Yahvé ton Dieu, toi, ton fils, ta fille, ton serviteur, ta servante, et le Lévite qui sera dans tes portes. Tu te réjouiras devant l'Éternel, ton Dieu, de tout ce que tu entreprendras.
19 Mwe waangalifu msiwapuuze Walawi kwa muda wote mnaoishi katika nchi yenu.
Prends garde de ne pas abandonner le Lévite tant que tu vivras dans ton pays.
20 Bwana Mungu wenu atakapokuwa ameongeza nchi yenu kama alivyowaahidi, nanyi mkitamani nyama na mkisema, “Ningependa nyama,” hapo unaweza kula nyingi upendavyo.
Lorsque l'Éternel, ton Dieu, aura agrandi ton territoire, comme il te l'a promis, et que tu diras: « Je veux manger de la viande », parce que ton âme désire manger de la viande, tu pourras manger de la viande, selon le désir de ton âme.
21 Kama mahali ambapo Bwana Mungu wenu atapachagua kuweka Jina lake ni mbali sana kutoka kwenu, unaweza kuchinja wanyama kutoka makundi yenu ya ngʼombe, ya mbuzi na ya kondoo ambayo Bwana amewapa, kama nilivyokuamuru, na mkiwa katika miji yenu wenyewe mnaweza kula nyingi mtakavyo.
Si le lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y placer son nom est trop éloigné de toi, tu tueras de ton troupeau et de ton menu bétail, que l'Éternel t'a donnés, comme je te l'ai ordonné, et tu mangeras dans tes portes, selon le désir de ton âme.
22 Mle kama vile mngekula paa na kulungu. Wote walio najisi kiibada na walio safi mwaweza kula.
Vous en mangerez comme on mange de la gazelle et du cerf. L'impur et le pur pourront en manger de la même manière.
23 Lakini hakikisheni kwamba hamkunywa damu, kwa sababu damu ni uhai, kamwe msile uhai pamoja na nyama.
Veille seulement à ne pas manger le sang, car le sang est la vie. Vous ne mangerez pas la vie avec la viande.
24 Hamruhusiwi kamwe kunywa damu; imwageni juu ya ardhi kama maji.
Vous ne le mangerez pas. Vous le répandrez sur la terre comme de l'eau.
25 Msinywe damu, ili mweze kufanikiwa ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo haki machoni pa Bwana.
Vous n'en mangerez pas, afin qu'il vous soit agréable, à vous et à vos enfants après vous, de faire ce qui est bien aux yeux de l'Éternel.
26 Lakini vichukueni vitu vyenu vilivyowekwa wakfu pamoja na vile mlivyoweka nadhiri, mwende mahali pale Bwana atakapopachagua.
Tu ne prendras que tes objets sacrés et tes vœux, et tu iras au lieu que choisira l'Éternel.
27 Leteni sadaka zenu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, vyote nyama na damu. Damu ya dhabihu zenu lazima imiminwe kando ya madhabahu ya Bwana Mungu wenu, lakini nyama mnaweza kula.
Tu offriras tes holocaustes, la viande et le sang, sur l'autel de l'Éternel, ton Dieu. Tu verseras le sang de tes sacrifices sur l'autel de l'Éternel, ton Dieu, et tu mangeras la viande.
28 Mwe waangalifu kutii masharti haya yote ninayowapa, ili kwamba siku zote mweze kufanikiwa, ninyi pamoja na watoto wenu baada yenu, kwa sababu mtakuwa mkifanya lililo jema na sahihi mbele za macho ya Bwana Mungu wenu.
Observe et écoute toutes ces paroles que je te prescris, afin que tout aille bien pour toi et pour tes enfants après toi, à perpétuité, si tu fais ce qui est bon et droit aux yeux de l'Éternel, ton Dieu.
29 Bwana Mungu wenu atayakatilia mbali mbele yenu mataifa ambayo punde kidogo mtayavamia na kuyaondoa. Lakini mtakapokuwa mmeyafukuza na kuishi katika nchi yao,
Lorsque Yahvé, ton Dieu, aura exterminé devant toi les nations que tu auras dépossédées, que tu les auras dépossédées et que tu auras habité leur pays,
30 na baada ya kuangamizwa mbele yenu, mwe waangalifu msijiingize katika tanzi kwa kuuliza habari za miungu yao, mkisema, “Je, mataifa haya hutumikiaje miungu yao? Nasi tutafanya vivyo hivyo.”
prends garde de ne pas te laisser entraîner à les suivre après qu'elles auront été détruites devant toi, et de ne pas rechercher leurs dieux en disant: « Comment ces nations servent-elles leurs dieux? Je ferai de même. »
31 Kamwe msimwabudu Bwana Mungu wenu kwa njia wanayoabudu miungu yao, kwa sababu katika kuabudu miungu yao, wanafanya aina zote za machukizo anayoyachukia Bwana. Hata huwateketeza wana wao na binti zao kwa moto kama kafara kwa miungu yao.
Vous n'agirez pas ainsi à l'égard de Yahvé, votre Dieu, car ils ont fait à leurs dieux toutes les abominations que Yahvé déteste; ils brûlent même au feu leurs fils et leurs filles pour leurs dieux.
32 Angalieni kwamba mnafanya yote niliyowaamuru; msiongeze kitu wala msipunguze kitu.
Tout ce que je te commanderai, tu auras soin de le mettre en pratique. Tu n'y ajouteras rien et tu n'en retrancheras rien.