< Danieli 12 >

1 “Katika wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa.
Forsothe in that tyme Miyhel, the greet prince, schal rise, that stondith for the sones of thi puple. And tyme schal come, what maner tyme was not, fro that tyme fro which folkis bigunnen to be, `vn to that tyme. And in that tyme thi puple schal be saued, ech that is foundun writun in the book of life.
2 Wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele, wengine kwa aibu na kudharauliwa milele.
And many of hem that slepen in the dust of erthe, schulen awake fulli, summe in to euerlastynge lijf, and othere in to schenschipe, that thei se euere.
3 Wale wenye hekima watangʼaa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao huwaongoza wengi kutenda haki, watangʼaa kama nyota milele na milele.
Forsothe thei that ben tauyt, schulen schyne as the schynyng of the firmament, and thei that techen many men to riytfulnesse, schulen schyne as sterris in to euerlastynge euerlastyngnessis.
4 Lakini wewe Danieli, yafunge na kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda huku na huko, na maarifa yataongezeka.”
But thou, Danyel, close the wordis, and aseele the book, til to the tyme ordeyned; ful many men schulen passe, and kunnyng schal be many fold.
5 Ndipo mimi Danieli nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo huu wa mto, na mwingine ukingo wa pili wa mto.
And Y, Danyel, siy, and lo! as tweyne othere men stood; oon stood on this side, on the brenk of the flood, and another on that side, on the tother part of the flood.
6 Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza hayajatimizwa?”
And Y seide to the man, that was clothid in lynnun clothis, that stood on the watris of the flood, Hou long schal be the ende of these merueils?
7 Kisha mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa jina lake yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili, na nusu wakati. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo mambo haya yote yatakapotimizwa.”
And Y herde the man, that was clothid in lynnun clothis, that stood on the watris of the flood, whanne he hadde reisid his riythond and lefthond to heuene, and hadde sworun by hym that lyueth with outen ende, For in to a tyme, and tymes, and the half of tyme. And whanne the scateryng of the hoond of the hooli puple is fillid, alle these thingis schulen be fillid.
8 Nilisikia, lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote yatakuwa nini?”
And Y herde, and vndurstood not; and Y seide, My lord, what schal be aftir these thingis?
9 Akajibu, “Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka wakati wa mwisho.
And he seide, Go thou, Danyel, for the wordis ben closid and aseelid, til to the tyme determyned.
10 Wengi watatakaswa, na kuondolewa mawaa na kufanywa safi, lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu, lakini wale wenye hekima watafahamu.
Many men schulen be chosun, and schulen be maad whijt, and schulen be preued as fier, and wickid men schulen do wickidli, nether alle wickid men schulen vndurstonde; certis tauyt men schulen vndurstonde.
11 “Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu, kutakuwako siku 1,290.
And fro the tyme whanne contynuel sacrifice is takun awei, and abhomynacioun is set in to discoumfort, schulen be a thousynde daies two hundrid and nynti.
12 Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335.
He is blessid, that abideth, and cometh fulli, til a thousynde daies thre hundrid and fyue and thritti.
13 “Lakini wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku utafufuka ili kuupokea urithi uliowekewa.”
But go thou, Danyel, to the tyme determyned; and thou schalt reste, and stonde in thi part, in the ende of daies.

< Danieli 12 >