< Hosea 2 >

1 “Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’
Sei ye to youre britheren, Thei ben my puple; and to youre sister that hath gete merci,
2 “Mkemeeni mama yenu, mkemeeni, kwa maana yeye si mke wangu, nami si mume wake. Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake na uzinzi kati ya matiti yake.
Deme ye youre modir, deme ye, for sche is not my wijf, and Y am not hir hosebonde. Do sche awey hir fornicaciouns fro hir face, and hir auowtries fro the myddis of hir brestis;
3 Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa. Nitamfanya kama jangwa, nitamgeuza awe nchi ya kiu, nami nitamuua kwa kiu.
lest perauenture Y spuyle hir nakid, and sette hir nakid bi the dai of hir natyuyte. And Y schal sette hir as a wildirnesse, and Y schal ordeyne hir as a lond with out weie, and Y schal sle hir in thirst.
4 Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake, kwa sababu ni watoto wa uzinzi.
And Y schal not haue merci on the sones of hir, for thei ben sones of fornicaciouns;
5 Mama yao amekosa uaminifu na amewachukua mimba katika aibu. Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu, ambao hunipa chakula changu na maji yangu, sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu na kinywaji changu.’
for the modir of hem dide fornicacioun, sche is schent that conseyuede hem, for sche seide, Y schal go after my louyeris that yeuen looues to me, and my watris, and my wolle, and my flex, and myn oile, and my drynke.
6 Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake kwa vichaka vya miiba, nitamjengea ukuta ili kwamba asiweze kutoka.
For this thing lo! Y schal hegge thi weie with thornes, and Y schal hegge it with a wal, and sche schal not fynde hir pathis.
7 Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata; atawatafuta lakini hatawapata. Kisha atasema, ‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza, kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi kuliko sasa.’
And sche schal sue hir louyeris, and schal not take hem, and sche schal seke hem, and schal not fynde; and sche schal seie, Y schal go, and turne ayen to my formere hosebonde, for it was wel to me thanne more than now.
8 Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta, niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia kwa kumtumikia Baali.
And this Jerusalem wiste not, that Y yaf to hir wheete, wyn, and oile; and Y multiplied siluer and gold to hir, whiche thei maden to Baal.
9 “Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari. Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu iliyokusudiwa kufunika uchi wake.
Therfor Y schal turne, and take my wheete in his tyme, and my wiyn in his tyme; and Y schal delyuere my wolle, and my flex, bi which thei hiliden the schenschipe therof.
10 Basi sasa nitaufunua ufisadi wake mbele ya wapenzi wake; hakuna yeyote atakayemtoa mikononi mwangu.
And now Y schal schewe the foli of hir bifore the iyen of hir louyeris, and a man schal not delyuere hir fro myn hond;
11 Nitakomesha furaha na macheko yake yote: sikukuu zake za mwaka, sikukuu za Miandamo ya Mwezi, siku zake za Sabato, sikukuu zake zote zilizoamriwa.
and Y schal make to ceesse al the ioye therof, the solempnyte therof, the neomenye therof, the sabat therof, and alle the feeste tymes therof.
12 Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake, ambayo alisema yalikuwa malipo yake kutoka kwa wapenzi wake; nitaifanya kuwa kichaka, nao wanyama pori wataila.
And Y schal distrie the vyner therof, of whiche sche seide, These ben myn hiris, whiche my louyeris yauen to me; and Y schal sette it in to a forest, and a beeste of the feeld schal ete it.
13 Nitamwadhibu kwa ajili ya siku alizowafukizia uvumba Mabaali; alipojipamba kwa pete na kwa vito vya thamani, na kuwaendea wapenzi wake, lakini mimi alinisahau,” asema Bwana.
And Y schal visite on it the daies of Baalym, in whiche it brente encense, and was ourned with hir eere ryng, and hir broche, and yede after hir louyeris, and foryat me, seith the Lord.
14 “Kwa hiyo sasa nitamshawishi; nitamwongoza hadi jangwani na kuzungumza naye kwa upole.
For this thing lo! Y schal yyue mylk to it, and Y schal brynge it in to wildirnesse, and Y schal speke to the herte therof.
15 Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu, nami nitalifanya Bonde la Akori mlango wa matumaini. Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama siku zile alizotoka Misri.
And Y schal yyue to it vyn tilieris therof of the same place, and the valei of Achar, that is, of disturblyng, for to opene hope. And it schal synge there bi the daies of hir yongthe, and bi the daies of hir stiyng fro the lond of Egipt.
16 “Katika siku ile,” asema Bwana, “utaniita mimi ‘Mume wangu’; hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’
And it schal be in that dai, seith the Lord, sche schal clepe me Myn hosebonde, and sche schal no more clepe me Baalym;
17 Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake, wala hataomba tena kwa majina yao.
and Y schal take awei the names of Baalym fro hir mouth, and sche schal no more haue mynde of the name of tho.
18 Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani, na viumbe vile vitambaavyo ardhini. Upinde, upanga na vita, nitaondolea mbali katika nchi, ili kwamba wote waweze kukaa salama.
And Y schal smyte to hem a boond of pees in that dai with the beeste of the feeld, and with the brid of the eir, and with the crepynge beeste of erthe. And Y schal al to-breke bowe, and swerd, and batel fro erthe; and Y schal make hem to slepe tristili.
19 Nitakuposa uwe wangu milele; nitakuposa kwa uadilifu na haki, kwa upendo na huruma.
And Y schal spouse thee to me withouten ende; and Y schal spouse thee to me in riytfulnesse, and in dom, and in merci, and in merciful doyngis.
20 Nitakuposa kwa uaminifu, nawe utamkubali Bwana.
And Y schal spouse thee to me in feith; and thou schalt wite, that Y am the Lord.
21 “Katika siku ile nitajibu,” asema Bwana, “nitajibu kwa anga, nazo anga zitajibu kwa nchi;
And it schal be, in that dai Y schal here, seith the Lord, and Y schal here heuenes, and tho schulen here the erthe;
22 nayo nchi itajibu kwa nafaka, divai mpya na mafuta, navyo vitajibu kwa Yezreeli.
and the erthe schal here wheete, and wyn, and oile, and these schulen here Jesrael.
23 Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe; nami nitaonyesha pendo langu kwake yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.’ Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’ ‘Ninyi ni watu wangu’; nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’”
And Y schal sowe it to me in to a lond, and Y schal haue merci on it that was with out merci. And Y schal seie to that, that is not my puple, Thou art my puple, and it schal seie, Thou art my God.

< Hosea 2 >