< Amosi 3 >

1 Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
Sones of Israel, here ye the word which the Lord spak on you, and on al the kynrede, which Y ledde out of the lond of Egipt,
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
and seide, Oneli Y knewe you of alle the kynredis of erthe; therfor Y schal visite on you alle youre wickidnessis.
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
Whether tweyne schulen go togidere, no but it acorde to hem?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
Whether a lioun schal rore in a forest, no but he haue prey? Whether the whelp of a lioun schal yyue vois fro his denne, no but he take ony thing?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
Whether a brid schal falle in to a snare of erthe, with outen a foulere? Whether a snare schal be takun awei fro erthe, bifor that it tak sum thing?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
Whether a trumpe schal sowne in a citee, and the puple schal not drede? Whether yuel schal be in a citee, which yuel the Lord schal not make?
7 Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
For the Lord God schal not make a word, no but he schewe his priuyte to hise seruauntis profetis.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
A lioun schal rore, who schal not drede? the Lord God spak, who schal not profesie?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
Make ye herd in the housis of Azotus, and in the housis of the lond of Egipt; and seie ye, Be ye gaderid togidere on the hillis of Samarye, and se ye many woodnessis in the myddis therof, and hem that suffren fals calenge in the priuy places therof.
10 Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
And thei kouden not do riytful thing, seith the Lord, and tresouriden wickidnesse and raueyn in her housis.
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
Therfor the Lord God seith these thingis, The lond schal be troblid, and be cumpassid; and thi strengthe schal be drawun doun of thee, and thin housis schulen be rauyschid.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
The Lord God seith these thingis, As if a schepherd rauyschith fro the mouth of a lioun tweyne hipis, ether the laste thing of the eere, so the children of Israel schulen be rauyschid, that dwellen in Samarie, in the cuntrei of bed, and in the bed of Damask.
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Here ye, and witnesse ye in the hous of Jacob, seith the Lord God of oostis.
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
For in the dai, whanne Y schal bigynne to visite the trespassyngis of Israel on hym, Y schal visite also on the auteris of Bethel; and the hornes of the auter schulen be kit awei, and schulen falle doun in to erthe.
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.
And Y schal smyte the wynter hous with the somer hous, and the housis of yuer schulen perische, and many housis schulen be distried, seith the Lord.

< Amosi 3 >