< Hosea 10 >

1 Israeli alikuwa mzabibu uliostawi sana, alijizalia matunda mwenyewe. Kadiri matunda yake yalivyoongezeka, alijenga madhabahu zaidi; kadiri nchi yake ilivyostawi, alipamba mawe yake ya ibada.
Israel was a vyne ful of bowis, fruyt was maad euene to hym; bi the multitude of his fruyt he multipliede auteris, bi the plente of his lond he was plenteuouse.
2 Moyo wao ni mdanganyifu, nao sasa lazima wachukue hatia yao. Bwana atabomoa madhabahu zao na kuharibu mawe yao ya ibada.
In simylacris the herte of hem is departid, now thei schulen perische. He schal breke the simylacris of hem, he schal robbe the auteris of hem.
3 Kisha watasema, “Hatuna mfalme kwa sababu hatukumheshimu Bwana. Lakini hata kama tungelikuwa na mfalme, angeweza kutufanyia nini?”
For thanne thei schulen seie, A kyng is not to vs, for we dreden not the Lord. And what schal a kyng do to vs?
4 Wanaweka ahadi nyingi, huapa viapo vya uongo wanapofanya mapatano; kwa hiyo mashtaka huchipuka kama magugu ya sumu katika shamba lililolimwa.
Speke ye wordis of vnprofitable visioun, and ye schulen smyte boond of pees with leesyng; and doom as bittirnesse schal burioune on the forewis of the feeld.
5 Watu wanaoishi Samaria huogopa kwa ajili ya sanamu ya ndama ya Beth-Aveni. Watu wake wataiombolezea, vivyo hivyo kuhani wake wa kuabudu sanamu, wale waliokuwa wamefurahia fahari yake, kwa sababu itaondolewa kutoka kwao kwenda uhamishoni.
The dwelleris of Samarie worschipiden the kien of Bethauen. For the puple therof mourenyde on that calf, and the keperis of the hous therof; thei maden ful out ioye on it in the glorie therof, for it passide fro that puple.
6 Itachukuliwa kwenda Ashuru kama ushuru kwa mfalme mkuu. Efraimu atafedheheshwa; Israeli ataaibika kwa ajili ya sanamu zake za mti.
For also it was borun to Assur, a yifte to the king veniere. Confusioun schal take Effraym, and Israel schal be schent in his wille.
7 Samaria na mfalme wake wataelea kama kijiti juu ya uso wa maji.
Samarie made his kyng to passe, as froth on the face of water. And the hiy thingis of idol, the synne of Israel, schulen be lost.
8 Mahali pa kuabudia sanamu pa uovu pataharibiwa: ndiyo dhambi ya Israeli. Miiba na mibaruti itaota na kufunika madhabahu zao. Kisha wataiambia milima, “Tufunikeni!” na vilima, “Tuangukieni!”
A cloote and a brere schal stie on the auters of hem. And thei schulen seie to mounteyns, Hile ye vs, and to litle hillis, Falle ye doun on vs.
9 “Tangu siku za Gibea, mmetenda dhambi, ee Israeli, huko ndiko mlikobaki. Je, vita havikuwapata watenda mabaya huko Gibea?
Fro the daies of Gabaa Israel synnede; there thei stoden. Batel schal not take hem in Gabaa,
10 Wakati nitakapopenda, nitawaadhibu; mataifa yatakusanywa dhidi yao ili kuwaweka katika vifungo kwa ajili ya dhambi zao mbili.
on the sones of wickidnesse. Bi my desir Y schal chastise hem; puplis schulen be gaderid togidere on hem, whanne thei schulen be chastisid for her twei wickidnessis.
11 Efraimu ni mtamba wa ngʼombe aliyefundishwa ambaye hupenda kupura, hivyo nitamfunga nira juu ya shingo yake nzuri. Nitamwendesha Efraimu, Yuda lazima alime, naye Yakobo lazima avunjavunje mabonge ya udongo.
Effraym is a cow calf, tauyt for to loue threischyng; and Y yede on the fairenesse of the necke therof. Y schal stie on Effraym. Judas schal ere, and Jacob schal breke forewis to hym silf.
12 Jipandieni wenyewe haki, vuneni matunda ya upendo usio na kikomo, vunjeni ardhi yenu isiyolimwa; kwa kuwa ni wakati wa kumtafuta Bwana, mpaka atakapokuja na kuwanyeshea juu yenu haki.
Sowe ye to you riytfulnesse in treuthe, and repe ye in the mouthe of merci, and make ye newe to you a feld newli brouyte to tilthe. Forsothe tyme is to seke the Lord, whanne he cometh, that schal teche you riytfulnesse.
13 Lakini mmepanda uovu, mkavuna ubaya, mmekula tunda la udanganyifu. Kwa sababu mmetegemea nguvu zenu wenyewe na wingi wa mashujaa wenu,
Ye han erid vnfeithfulnesse, ye han rope wickidnesse, ye han ete the corn of leesyng. For thou tristydist in thi weles, and in the multitude of thi stronge men.
14 mngurumo wa vita utainuka dhidi ya watu wako, ili kwamba ngome zako zote zitaharibiwa: kama Shalmani alivyoharibu Beth-Arbeli katika siku ile ya vita, wakati mama pamoja na watoto wao walipotupwa kwa nguvu ardhini.
Noise schal rise in thi puple, and alle thi stronge holdis schulen be distried; as Salmana was distried of the hous of hym, that took veniaunce on Baal; in the dai of batel, whanne the modir was hurlid doun on the sones.
15 Ndivyo itakavyotokea kwako, ee Betheli, kwa sababu uovu wako ni mkuu. Siku ile itakapopambazuka, mfalme wa Israeli ataharibiwa kabisa.
So Bethel dide to you, for the face of malice of youre wickidnessis.

< Hosea 10 >