< Matendo 28 >

1 Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta.
And after we had escaped, we then realized that the island was called Malta. Yet truly, the natives offered us no small amount of humane treatment.
2 Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi.
For they refreshed us all by kindling a fire, because rain was imminent and because of the cold.
3 Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake.
But when Paul had gathered together a bundle of twigs, and had placed them on the fire, a viper, which had been drawn to the heat, fastened itself to his hand.
4 Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.”
And truly, when the natives saw the beast hanging from his hand, they were saying to one another: “Certainly, this man must be a murderer, for though he escaped from the sea, vengeance will not permit him to live.”
5 Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote.
But shaking off the creature into the fire, he indeed suffered no ill effects.
6 Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.
But they were supposing that he would soon swell up, and then would suddenly fall down and die. But having waited a long time, and seeing no ill effects in him, they changed their minds and were saying that he was a god.
7 Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu.
Now among these places were estates owned by the ruler of the island, named Publius. And he, taking us in, showed us kind hospitality for three days.
8 Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya.
Then it happened that the father of Publius lay ill with a fever and with dysentery. Paul entered to him, and when he had prayed and had laid his hands on him, he saved him.
9 Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa.
When this had been done, all who had diseases on the island approached and were cured.
10 Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.
And then they also presented us with many honors. And when we were ready to set sail, they gave us whatever we needed.
11 Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi.
And so, after three months, we sailed in a ship from Alexandria, whose name was ‘the Castors,’ and which had wintered at the island.
12 Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu.
And when we had arrived at Syracuse, we were delayed there for three days.
13 Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli.
From there, sailing close to the shore, we arrived at Rhegium. And after one day, with the south wind blowing, we arrived on the second day at Puteoli.
14 Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi.
There, after locating the brothers, we were asked to remain with them for seven days. And then we went on to Rome.
15 Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo.
And there, when the brothers had heard of us, they went to meet us as far as the Forum of Appius and the Three Taverns. And when Paul had seen them, giving thanks to God, he took courage.
16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.
And when we had arrived at Rome, Paul was given permission to stay by himself, with a soldier to guard him.
17 Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi.
And after the third day, he called together the leaders of the Jews. And when they had convened, he said to them: “Noble brothers, I have done nothing against the people, nor against the customs of the fathers, yet I was delivered as a prisoner from Jerusalem into the hands of the Romans.
18 Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo.
And after they held a hearing about me, they would have released me, because there was no case for death against me.
19 Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu.
But with the Jews speaking against me, I was constrained to appeal to Caesar, though it was not as if I had any kind of accusation against my own nation.
20 Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”
And so, because of this, I requested to see you and to speak to you. For it is because of the hope of Israel that I am encircled with this chain.”
21 Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako.
But they said to him: “We have not received letters about you from Judea, nor have any of the other new arrivals among the brothers reported or spoken anything evil against you.
22 Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”
But we are asking to hear your opinions from you, for concerning this sect, we know that it is being spoken against everywhere.”
23 Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii.
And when they had appointed a day for him, very many persons went to him at his guest quarters. And he discoursed, testifying to the kingdom of God, and persuading them about Jesus, using the law of Moses and the Prophets, from morning until evening.
24 Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini.
And some believed the things that he was saying, yet others did not believe.
25 Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:
And when they could not agree among themselves, they departed, while Paul was speaking this one word: “How well did the Holy Spirit speak to our fathers through the prophet Isaiah,
26 “‘Nenda kwa watu hawa na useme, “Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama, lakini hamtaona.”
saying: ‘Go to this people and say to them: Hearing, you shall hear and not understand, and seeing, you shall see and not perceive.
27 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
For the heart of this people has grown dull, and they have listened with reluctant ears, and they have closed their eyes tightly, lest perhaps they might see with the eyes, and hear with the ears, and understand with the heart, and so be converted, and I would heal them.’
28 “Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [
Therefore, let it be known to you, that this salvation of God has been sent to the Gentiles, and they shall listen to it.”
29 Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]
And when he had said these things, the Jews went away from him, though they still had many questions among themselves.
30 Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona.
Then he remained for two whole years in his own rented lodgings. And he received all who went in to him,
31 Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.
preaching the kingdom of God and teaching the things which are from the Lord Jesus Christ, with all faithfulness, without prohibition.

< Matendo 28 >