< Matendo 26 >

1 Ndipo Agripa akamwambia Paulo, “Unayo ruhusa kujitetea.” Hivyo Paulo akawaashiria kwa mkono wake, akaanza kujitetea, akasema:
So Agrippa said to Paul, “You may speak for yourself.” Then Paul stretched out his hand and made his defense.
2 “Mfalme Agripa, najiona kuwa na heri kusimama mbele yako leo ninapojitetea kuhusu mashtaka yote ya Wayahudi,
“I regard myself as happy, King Agrippa, to make my case before you today against all the accusations of the Jews;
3 hasa kwa sababu unajua vyema desturi zote za Kiyahudi na ya kuwa wewe unajua kwa undani mila na masuala ya mabishano. Kwa hiyo, nakusihi unisikilize kwa uvumilivu.
especially, because you are an expert in all the Jewish customs and questions. So I ask you to hear me patiently.
4 “Wayahudi wote wanajua jinsi nilivyoishi tangu nilipokuwa mtoto, kuanzia mwanzo wa maisha yangu katika nchi yangu na pia huko Yerusalemu.
Truly, all the Jews know how I lived from my youth in my own nation and at Jerusalem.
5 Wao wamefahamu kwa muda mrefu na wanaweza kushuhudia kama wakipenda, ya kwamba kutokana na misimamo mikali sana ya dhehebu letu kwenye dini yetu, niliishi nikiwa Farisayo.
They knew me from the beginning and they should admit that I lived as a Pharisee, the strictest party of our religion.
6 Nami sasa ni kwa sababu ya tumaini langu katika kile ambacho Mungu aliwaahidi baba zetu, ninashtakiwa leo.
Now I stand here to be judged because of my certain hope in the promise made by God to our fathers.
7 Hii ndiyo ahadi ambayo makabila yetu kumi na mawili yanatarajia kuiona ikitimizwa wanapomtumikia Mungu kwa bidii usiku na mchana. Ee mfalme, ninashtakiwa na Wayahudi kwa ajili ya tumaini hili.
For this is the promise that our twelve tribes sought to receive as they earnestly worshiped God night and day. It is for this certain hope, King Agrippa, that the Jews accuse me.
8 Kwa nini yeyote miongoni mwenu afikiri kwamba ni jambo lisilosadikika Mungu kufufua wafu?
Why should any of you think it is unbelievable that God raises the dead?
9 “Mimi pia nilikuwa nimeshawishika kwamba imenipasa kufanya yote yale yaliyowezekana kupinga Jina la Yesu wa Nazareti.
Now indeed, I myself thought that I should do many things against the name of Jesus of Nazareth.
10 Nami hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Kwa mamlaka ya viongozi wa makuhani, niliwatia wengi wa watakatifu gerezani na walipokuwa wakiuawa, nilipiga kura yangu kuunga mkono.
I did these in Jerusalem. I locked up many of the saints in prison by the authority I received from the chief priests, and when they were killed, I cast my vote against them.
11 Mara nyingi nilikwenda kutoka sinagogi moja hadi ingine nikiamuru waadhibiwe, nami nilijaribu kuwalazimisha wakufuru. Katika shauku yangu dhidi yao, hata nilikwenda miji ya kigeni ili kuwatesa.
I punished them many times in all the synagogues and I tried to force them to blaspheme. I was furiously enraged against them and I persecuted them even to foreign cities.
12 “Siku moja nilipokuwa katika mojawapo ya safari hizi nikiwa ninakwenda Dameski, nilikuwa na mamlaka na agizo kutoka kwa kiongozi wa makuhani.
While I was doing this, I went to Damascus with authority and orders from the chief priests;
13 Ilikuwa yapata adhuhuri, ee mfalme, nilipokuwa njiani, niliona nuru kutoka mbinguni kali kuliko jua, ikingʼaa kunizunguka pande zote mimi na wale niliokuwa pamoja nao.
and on the way there, at midday, King, I saw a light from heaven that was brighter than the sun and it shone around both me and the men who were traveling with me.
14 Wote tulipokuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya Kiebrania, ‘Sauli, Sauli, mbona unanitesa? Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo.’
When we all fell to the ground, I heard a voice speaking to me that said in the Hebrew language, 'Saul, Saul, why do you persecute me? It is hard for you to kick a goad.'
15 “Nikauliza, ‘Ni nani wewe, Bwana?’ “Naye Bwana akajibu, ‘Ni Mimi Yesu unayemtesa.
Then I said, 'Who are you, Lord?' The Lord replied, 'I am Jesus whom you persecute.
16 Sasa inuka usimame kwa miguu yako. Nimekutokea ili nikuteue uwe mtumishi na shahidi wa mambo ambayo umeyaona, na yale nitakayokuonyesha.
Now get up and stand on your feet; because for this purpose I appeared to you, to appoint you to be a servant and a witness concerning the things that you know about me now and the things that I will show to you later;
17 Nitakuokoa kutoka kwa watu wako na watu wa Mataifa ambao ninakutuma kwao,
and I will rescue you from the people and from the Gentiles to whom I am sending you,
18 uyafumbue macho yao ili wageuke kutoka gizani waingie nuruni, na kutoka kwenye nguvu za Shetani wamgeukie Mungu, ili wapate msamaha wa dhambi na sehemu miongoni mwa wale waliotakaswa kwa kuniamini mimi.’
to open their eyes and to turn them from darkness to light and from the power of Satan to God, so that they may receive from God the forgiveness of sins and the inheritance that I give to them who are sanctified by faith in me.'
19 “Hivyo basi, Mfalme Agripa, sikuacha kuyatii yale maono yaliyotoka mbinguni,
Therefore, King Agrippa, I did not disobey the heavenly vision;
20 bali niliyatangaza kwanza kwa wale wa Dameski, kisha Yerusalemu na katika vijiji vyote vya Uyahudi na pia kwa watu wa Mataifa, kwamba inawapasa kutubu na kumgeukia Mungu na kuthibitisha toba yao kwa matendo yao.
but, to those in Damascus first, and then at Jerusalem, and throughout all the country of Judea, and also to the Gentiles, I gave them the message that that they should repent and turn to God, doing deeds worthy of repentance.
21 Ni kwa sababu hii Wayahudi walinikamata nilipokuwa Hekaluni, wakataka kuniua.
For this cause the Jews arrested me in the temple and tried to kill me.
22 Hadi leo nimepata msaada kutoka kwa Mungu, na hivyo nasimama hapa nikishuhudia kwa wakubwa na wadogo. Sisemi chochote zaidi ya yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia:
God has helped me until now, so I stand and testify to the common people and to the great ones about nothing more than what the prophets and Moses said would happen—
23 kwamba Kristo atateswa, na kwamba yeye atakuwa wa kwanza kufufuka kutoka kwa wafu, na atatangaza nuru kwa watu wake na kwa watu wa Mataifa.”
that Christ must suffer and that by being the first to rise from the dead, he would proclaim light to our own people and to the Gentiles.”
24 Paulo alipokuwa akifanya utetezi huu, Festo akasema kwa sauti kubwa, “Paulo, wewe umerukwa na akili! Kusoma kwingi kunakufanya uwe kichaa!”
As Paul completed his defense, Festus said with a loud voice, “Paul, you are insane; your great learning makes you insane.”
25 Lakini Paulo akajibu, “Mimi sijarukwa na akili, mtukufu sana Festo, bali nanena kweli nikiwa na akili zangu timamu.
But Paul said, “I am not insane, most excellent Festus, but what I am declaring is true and rational.
26 Naam, Mfalme anajua kuhusu mambo haya yote, nami nasema naye kwa uhuru. Kwa sababu nina hakika kwamba hakuna hata mojawapo ya mambo haya asilolijua, kwa kuwa hayakufanyika mafichoni.
For the king knows about these things; and so, I speak freely to him, for I am persuaded that none of this is hidden from him; for this has not been done in a corner.
27 Mfalme Agripa, je, unaamini manabii? Najua kuwa unaamini.”
Do you believe the prophets, King Agrippa? I know that you believe.”
28 Agripa akamwambia Paulo, “Je, unanishawishi kwa haraka namna hii niwe Mkristo?”
Agrippa said to Paul, “In a short time would you persuade me and make me a Christian?”
29 Paulo akasema, “Ikiwa ni kwa haraka au la, namwomba Mungu, si wewe peke yako bali pia wale wote wanaonisikiliza leo, wawe kama mimi nilivyo, kasoro minyororo hii.”
Paul said, “I pray to God, that whether in a short or long time, not you only, but also all that hear me today, would be like me, but without these prison chains.”
30 Baada ya kusema hayo, mfalme akainuka pamoja na mtawala na Bernike na wale waliokuwa wameketi pamoja nao.
Then the king stood up, and the governor, and Bernice also, and those who were sitting with them;
31 Walipokuwa wakiondoka, wakaambiana, “Mtu huyu hafanyi jambo lolote linalostahili kufa au kufungwa.”
when they left the hall, they talked to one another and said, “This man does nothing worthy of death or of bonds.”
32 Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeachwa huru kama hangekuwa amekata rufaa kwa Kaisari.”
Agrippa said to Festus, “This man could have been freed if he had not appealed to Caesar.”

< Matendo 26 >