< Matendo 12 >
1 Wakati huo huo Mfalme Herode Agripa aliwakamata baadhi ya watu wa kanisa.
Now at the same time, king Herod extended his hand, in order to afflict some from the Church.
2 Akaamuru Yakobo, ndugu yake Yohana, auawe kwa upanga.
Then he killed James, the brother of John, with the sword.
3 Alipoona jambo hilo limewapendeza Wayahudi, akaendelea, akamkamata pia Petro. Hii ilitokea wakati wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.
And seeing that it pleased the Jews, he set out next to apprehend Peter also. Now it was the days of Unleavened Bread.
4 Baada ya kumkamata alimtia gerezani, chini ya ulinzi wa vikundi vinne vya askari, vyenye askari wanne kila kimoja. Herode alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka mbele ya watu baada ya Pasaka.
So when he had apprehended him, he sent him into prison, handing him over into the custody of four groups of four soldiers, intending to produce him to the people after the Passover.
5 Kwa hiyo Petro akawekwa gerezani, lakini kanisa lilikuwa likimwombea kwa Mungu kwa bidii.
And so Peter was detained in prison. But prayers were being made without ceasing, by the Church, to God on his behalf.
6 Usiku ule kabla ya siku ambayo Herode Agripa alikuwa amekusudia kumtoa na kumfanyia mashtaka, Petro alikuwa amelala kati ya askari wawili, akiwa amefungwa kwa minyororo miwili. Nao walinzi wa zamu walikuwa wakilinda penye lango la gereza.
And when Herod was ready to produce him, in that same night, Peter was sleeping between two soldiers, and was bound with two chains. And there were guards in front of the door, guarding the prison.
7 Ghafula malaika wa Bwana akatokea na nuru ikamulika mle ndani ya gereza. Yule malaika akampiga Petro ubavuni na kumwamsha, akisema, “Ondoka upesi!” Mara ile minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro.
And behold, an Angel of the Lord stood near, and a light shined forth in the cell. And tapping Peter on the side, he awakened him, saying, “Rise up, quickly.” And the chains fell from his hands.
8 Yule malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Kisha akamwambia, “Jifunge vazi lako na unifuate.”
Then the Angel said to him: “Dress yourself, and put on your boots.” And he did so. And he said to him, “Wrap your garment around yourself and follow me.”
9 Petro akatoka mle gerezani akiwa amefuatana na yule malaika. Hakujua wakati huo kuwa yaliyokuwa yakitukia yalikuwa kweli. Alidhani kuwa anaona maono.
And going out, he followed him. And he did not know this truth: that this was being done by an Angel. For he thought that he was seeing a vision.
10 Wakapita lindo la kwanza na la pili, ndipo wakafika kwenye lango la chuma linaloelekea mjini. Lango likawafungukia lenyewe, nao wakapita hapo wakatoka nje. Baada ya kutembea umbali wa mtaa mmoja, ghafula yule malaika akamwacha Petro.
And passing by the first and second guards, they came to the iron gate which leads into the city; and it opened for them by itself. And departing, they continued on along a certain side street. And suddenly the Angel withdrew from him.
11 Ndipo Petro akarudiwa na fahamu, akasema, “Sasa ninajua bila shaka yoyote kuwa Bwana amemtuma malaika wake na kuniokoa kutoka makucha ya Herode Agripa na kutoka matazamio yote ya Wayahudi.”
And Peter, returning to himself, said: “Now I know, truly, that the Lord sent his Angel, and that he rescued me from the hand of Herod and from all that the people of the Jews were anticipating.”
12 Mara Petro alipotambua hili alikwenda nyumbani kwa Maria, mama yake Yohana aliyeitwa pia Marko, ambako watu wengi walikuwa wamekutana kwa maombi.
And as he was considering this, he arrived at the house of Mary, the mother of John, who was surnamed Mark, where many were gathered and were praying.
13 Petro alipobisha hodi kwenye lango la nje, mtumishi wa kike jina lake Roda, akaja kumfungulia.
Then, as he knocked at the door of the gate, a girl went out to answer, whose name was Rhoda.
14 Alipoitambua sauti ya Petro, alifurahi mno akarudi bila kufungua na kuwaeleza kwamba, “Petro yuko langoni!”
And when she recognized the voice of Peter, out of joy, she did not open the gate, but instead, running in, she reported that Peter stood before the gate.
15 Wakamwambia yule mtumishi wa kike, “Umerukwa na akili.” Alipozidi kusisitiza kuwa ni kweli, wakasema, “Lazima awe ni malaika wake.”
But they said to her, “You are crazy.” But she reaffirmed that this was so. Then they were saying, “It is his angel.”
16 Lakini Petro aliendelea kugonga langoni, nao walipofungua lango na kumwona Petro, walistaajabu sana.
But Peter was persevering in knocking. And when they had opened, they saw him and were astonished.
17 Yeye akawaashiria kwa mkono wake wanyamaze kimya, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa gerezani. Naye akaongeza kusema, “Waelezeni Yakobo na ndugu wengine habari hizi.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
But motioning to them with his hand to be silent, he explained how the Lord had led him away from prison. And he said, “Inform James and those brothers.” And going out, he went away to another place.
18 Kulipokucha kukawa na fadhaa kubwa miongoni mwa wale askari kuhusu yaliyomtukia Petro.
Then, when daylight came, there was no small commotion among the soldiers, as to what had happened concerning Peter.
19 Baada ya Herode kuamuru atafutwe kila mahali na bila kumpata, aliwahoji wale askari walinzi kisha akatoa amri wauawe. Basi Herode Agripa akatoka Uyahudi akaenda Kaisaria, akakaa huko kwa muda.
And when Herod had requested him and did not obtain him, having had the guards interrogated, he ordered them led away. And descending from Judea into Caesarea, he lodged there.
20 Basi Herode Agripa alikuwa amekasirishwa sana na watu wa Tiro na Sidoni. Hivyo watu wa miji hiyo miwili wakaungana pamoja wakatafuta kukutana naye. Wakiisha kuungwa mkono na Blasto, mtumishi maalum wa Mfalme Herode Agripa aliyeaminika, wakaomba mapatano ya amani maana nchi zao zilitegemea nchi ya huyo mfalme kwa mahitaji yao ya chakula.
Now he was angry with those of Tyre and Sidon. But they came to him with one accord, and, having persuaded Blastus, who was over the bedchamber of the king, they petitioned for peace, because their regions were supplied with food by him.
21 Katika siku iliyochaguliwa Herode Agripa akavaa mavazi yake ya kifalme, akaketi kwenye kiti chake cha enzi na kuwahutubia watu.
Then, on the appointed day, Herod was clothed in kingly apparel, and he sat in the judgment seat, and he gave a speech to them.
22 Watu waliokuwa wamekusanyika wakapiga kelele, wakisema, “Hii si sauti ya mwanadamu, bali ni ya Mungu.”
Then the people were crying out, “The voice of a god, and not of a man!”
23 Ghafula, kwa kuwa Herode hakumpa Mungu utukufu, malaika wa Bwana akampiga, naye akaliwa na chango, akafa.
And immediately, an Angel of the Lord struck him down, because he had not given honor to God. And having been consumed by worms, he expired.
24 Lakini neno la Mungu likaendelea mbele na kuenea, nao wengi wakaambatana nalo.
But the word of the Lord was increasing and multiplying.
25 Barnaba na Sauli walipomaliza ile huduma yao iliyowapeleka, wakarudi Yerusalemu wakiwa pamoja na Yohana aitwaye Marko.
Then Barnabas and Saul, having completed the ministry, returned from Jerusalem, bringing with them John, who was surnamed Mark.