< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
Finally, brethren, pray for us in order that the word of the Lord may run and be glorified, as even unto you:
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
and in order that we may be delivered from the ungodly and wicked men; for faith does not belong to all.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
But the Lord is faithful, who will establish you and keep you from the evil one.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
And we have trusted in the Lord in your behalf, that you are doing, and will do whatsoever we command.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
And the Lord direct your hearts into the love of God, and the patience of Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
And we command you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, that you withdraw from every brother who walks about disorderly, and not according to the teaching they received from us.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
For you yourselves know how it behooves you to imitate us; because we were not disorderly among you;
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
neither did we eat bread with any one gratuitously, but with labor and toil, night and day working, that we might not burden any one of you:
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
not because we have not the right, but in order that we may give ourselves an example to you, that you may imitate us.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
For indeed when we were with you, we proclaimed this to you, that if any one does not wish to work, let him not eat.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
For we hear that there are certain ones walking about among you disorderly, doing nothing, but they are busybodies:
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
but we command such and exhort them in the Lord Jesus Christ, that with quietude working, they must eat their own bread.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
But you, brethren, be not weary doing well.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
But if any one does not obey our word through the epistle, note him; do not keep company with him; in order that he may be ashamed;
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
consider him not as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
The Lord of peace himself grant unto you peace always in every way. The Lord be with you all.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
Salutation of me Paul with my own hand, which is the token in every epistle: so I write.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.

< 2 Wathesalonike 3 >